Kuhusu mpaka wa Zanzibar na Tanganyika

Kuhusu mpaka wa Zanzibar na Tanganyika

rasachri

Senior Member
Joined
Apr 8, 2011
Posts
145
Reaction score
35
Habari wana JF?

Inafahamika kua watanzania tuna kasumba ya kuyakuza maneno ya mtaani eidha kwa kujua ukweli wake au kwa kuyadhania tu ili mradi na sisi tuonekane tunajua.

Hili suala la mpaka wa tanganyika na znz linaleta mkanganyiko kwa baadhi ya watanzania kutokana na watu wachache ambao wamekua wakijaribu kuvumisha ni wapi ilipo mipaka ya znz na tanganyika, watu hao hawana ushahidi wowote juu ya wayasemayo kwa watu huku chini chini, cha kusikitisha ni kua baadhi ya wavumishaji hao ni maofsa na watumishi wa serikali kana kwamba hawaelewi madhara wanayoweza kutuletea kama taifa.

Rai yangu ni kwamba, watu wanaovumisha maneno chini chini haswa haya yenye maslahi kwa taifa, waache tabia hiyo kwa kua haitajenga na badala yake itabomoa kutokana na kuwaacha wanajamii njia panda, tanganyika na znz ni wamoja ndio mana tunaishi kama ndugu tangu miaka hiyo.

Ikiwa mtu anadhani anafahamu sana mambo ya nchi asimame hadharani na kuyazungumza na sio kupiga porojo mtaani ili waonekane wanajua wakati mimi kwa mtazamo wangu naona hawajui kitu. mtu anayejua anasimama na kupresent hadharani anachokijua na mwishowe ataukizwa maswali.

Nawasilisha.
 
habari wana jf?

inafahamika kua watanzania tuna kasumba ya kuyakuza maneno ya mtaani eidha kwa kujua ukweli wake au kwa kuyadhania tu ili mradi na sisi tuonekane tunajua.

hili suala la mpaka wa tanganyika na znz linaleta mkanganyiko kwa baadhi ya watanzania kutokana na watu wachache ambao wamekua wakijaribu kuvumisha ni wapi ilipo mipaka ya znz na tanganyika, watu hao hawana ushahidi wowote juu ya wayasemayo kwa watu huku chini chini, cha kusikitisha ni kua baadhi ya wavumishaji hao ni maofsa na watumishi wa serikali kana kwamba hawaelewi madhara wanayoweza kutuletea kama taifa.

rai yangu ni kwamba, watu wanaovumisha maneno chini chini haswa haya yenye maslahi kwa taifa, waache tabia hiyo kwa kua haitajenga na badala yake itabomoa kutokana na kuwaacha wanajamii njia panda, tanganyika na znz ni wamoja ndio mana tunaishi kama ndugu tangu miaka hiyo.

ikiwa mtu anadhani anafahamu sana mambo ya nchi asimame hadharani na kuyazungumza na sio kupiga porojo mtaani ili waonekane wanajua wakati mimi kwa mtazamo wangu naona hawajui kitu. mtu anayejua anasimama na kupresent hadharani anachokijua na mwishowe ataukizwa maswali.

nawasilisha.

Sasa na wewe unapotoa malalamiko bila kutoa ufafanuzi ni kuzidisha uvumi...ukweli ni kwamba ikulu ya dsm na maeneo yote ya posta ni sehemu ya zanzibar. Nyerere alilijua hili ndio maana alikua mnyenyekevu kwa zanzibar na muungano
 
Kabla ya muungano tanganyika ilikuwa mwisho wake wapi?
 
Sasa na wewe unapotoa malalamiko bila kutoa ufafanuzi ni kuzidisha uvumi...ukweli ni kwamba ikulu ya dsm na maeneo yote ya posta ni sehemu ya zanzibar. Nyerere alilijua hili ndio maana alikua mnyenyekevu kwa zanzibar na muungano

huna jipya mkuu, we ni mmoja wa mashabiki wa mashabiki wa stori za kusadikika. kama unajua huo ndio ukweli tuwekee mezani sio unatupotosha kwa kuzungumza uliyoyasikia kijiwe cha kahawa, ukikaa kijiweni ukasikia stori hutoki ukaiacha hapo hapo unaishikiria unaenda kuhadithia kwa kuongeza na chumvi.

watz tuache hizo, tuzungumze tunayoyajua kiasi kwamba ukiulizwa utaweza kutoa ushahidi ma maelezo zaidi juu ya jambo husika.

mzungu anasema, "no data no right to speak"
 
kilomita 16 za pwani yote ni himaya ya mzanzibar,hilo mbona liko wazi tu
 
naunga mkono hoja

hushangazwa sana na hawa wtu mtu unamkuta amezaliwa mwaka 93 lakini anajidai anajua vzr mambo ya muungano na uhuru ukimuuliza umepata wap oooh!! kwenye kijiwe cha kahawa sasa una ushahidi? ooooh hata marehemu babu alisema. jama naomba tuseme vitu tuvijuavyo na vyenye ushahidi wa kutosha msiwe vishazi tegemezi
 
Ukweli ni kwamba wakati wa Berlin conference 1884 /1885 Sultan said sayid alipewa zanzibar pamoja na 10 kilometers za pwani ya tanganyika history ipo hivyo, kama huamini Google au kasome vitabu vya history topic inaitwa scramble and partition of Africa.
 
Ukweli ni kwamba wakati wa Berlin conference 1884 /1885 Sultan said sayid alipewa zanzibar pamoja na 10 kilometers za pwani ya tanganyika history ipo hivyo, kama huamini Google au kasome vitabu vya history topic inaitwa scramble and partition of Africa.

mwambie sultan aje adai ardhi yake aliyopewa na wazungu kwenye mkutano huo!
 
kilomita 16 za pwani yote ni himaya ya mzanzibar,hilo mbona liko wazi tu
Kweli ni balaaa...kwahiyo kuanzia msumbiji hadi kenya pia umbali wa km 16 itakuwa zenji, na sie turudishe mipaka ya tanganyika.....rwanda na burundi zitakuwa ndani kwetu pia. Duh bonge la contradiction
 
Hawezi kuja kudai mipaka Sultan kwa sababu Sultan alipoondolewa znz ilibaki mikononi mwa wa zanzibar wenyewe kama tanganyika ilivyobaki mikononi mwa wa tanganyika na tukumbuke mipaka yote Africa na mgawanyo wa kuwepo kwa nchi hizi walizigawa wakoloni na ikabaki hivyo.
 
Kabla ya muungano tanganyika ilikuwa mwisho wake wapi?
Mbona mnaibua ya zamani na kuanza kututisha sasa! Hivi hii inahusu kilomita 10 kutoka mwisho wa bahari kuingia bara!? Na je, inakuwaje kwa yale maeneo ambao ardhi inamezwa na bahari mfano Mtwara, nako mipaka itaendelea kusogezwa bara!?

 
Ukweli ni kwamba wakati wa Berlin conference 1884 /1885 Sultan said sayid alipewa zanzibar pamoja na 10 kilometers za pwani ya tanganyika history ipo hivyo, kama huamini Google au kasome vitabu vya history topic inaitwa scramble and partition of Africa.
Hivi ni wakati huo pia ziwa Nyasa lilipotolewa kwa Malawi!?

 
Sasa na wewe unapotoa malalamiko bila kutoa ufafanuzi ni kuzidisha uvumi...ukweli ni kwamba ikulu ya dsm na maeneo yote ya posta ni sehemu ya zanzibar. Nyerere alilijua hili ndio maana alikua mnyenyekevu kwa zanzibar na muungano

Mwambie hata lile sanamu pale round about, ni mali ya Kibandamaiti
 
habari wana jf?

inafahamika kua watanzania tuna kasumba ya kuyakuza maneno ya mtaani eidha kwa kujua ukweli wake au kwa kuyadhania tu ili mradi na sisi tuonekane tunajua.

hili suala la mpaka wa tanganyika na znz linaleta mkanganyiko kwa baadhi ya watanzania kutokana na watu wachache ambao wamekua wakijaribu kuvumisha ni wapi ilipo mipaka ya znz na tanganyika, watu hao hawana ushahidi wowote juu ya wayasemayo kwa watu huku chini chini, cha kusikitisha ni kua baadhi ya wavumishaji hao ni maofsa na watumishi wa serikali kana kwamba hawaelewi madhara wanayoweza kutuletea kama taifa.

rai yangu ni kwamba, watu wanaovumisha maneno chini chini haswa haya yenye maslahi kwa taifa, waache tabia hiyo kwa kua haitajenga na badala yake itabomoa kutokana na kuwaacha wanajamii njia panda, tanganyika na znz ni wamoja ndio mana tunaishi kama ndugu tangu miaka hiyo.

ikiwa mtu anadhani anafahamu sana mambo ya nchi asimame hadharani na kuyazungumza na sio kupiga porojo mtaani ili waonekane wanajua wakati mimi kwa mtazamo wangu naona hawajui kitu. mtu anayejua anasimama na kupresent hadharani anachokijua na mwishowe ataukizwa maswali.

nawasilisha.

Chukua na usome Katiba ya Zanzibar ambayo imetanabaisha kuwa ZANZIBAR ni nchi hivyo na mipaka yake imeelezwa humo ndani. Zanzibar imejiweka wazi na kurejesha mipaka yake ya zamani kabla ya huu muungano.
 
Ndo maana baba wa taifa aling'ang'ana mji mkuu uwe dodoma.
 
Back
Top Bottom