the ultimatum
JF-Expert Member
- Dec 16, 2012
- 419
- 142
Napenda kutoa taarifa za kuhujumiwa kwa DAWASCO maeneo ya Mwananyamala Mchangani, mtaa wa Juhudi.
Mimi ni raia mwema nimeamua kutoa taarifa kwa mamlaka zinazohusika kuhusu kijana maarufu kwa jina la Mudi Chavi ambaye kwa muda mrefu sasa amekuwa akijishughurisha na uuzaji maji maeneo ya Mwananyamala Mchangani mtaa wa Juhudi.
MBINU ANAZOTUMIA KUJIPATIA MAJI.
Amekuwa akiihujumu DAWASCO kwa muda mrefu sana. Na mbinu anazotumia kujipatia maji ni kukata mipira ya maji ntakati za usiku na kuunganisha kwenye mipira yake ambayo inakwenda kujaza matank ya maji anayomiliki na baadae kuuza kwa wananchi.
HASARA ANAZOSABABISHA.
Licha ya kuwa anaharibu miundombinu ya DAWASCO lakini pia amekuwa akichangia upotevu mkubwa wa maji, kwani mara nyingi anapokuwa amekata mipira hushindwa kuifunga na kuacha maji yakitiririka muda mrefu sana all night long. Maji nyakati za usiku huwa na presha kubwa kitu ambacho kinamuwia vigumu kurejeshea mpira anaokuwa ameukata. Mpaka naandika taarifa hii leo asubuhi wakati naenda mihangaukoni nimekutana na madimbwi makubwa ya maji huku moja ya mpira ukiwa unatirirsha maji kwa kasi ya ajabu. Ninaposema madimbwi naomba nieleweke ni madimbwi kweli kweli just like public swimming pool.
MAJI YANAYOPOTEA KIMAHESABU.
Ndugu zangu ipo hivi, kwa presha ya maji nyakati za usiku makadirio ya haraka kwa mipira hii midogo ya kawaida inaweza ikatiririsha lita moja za maji kwa kila sekunde, maana yake hapa ni kwamba kila anapoacha mipira ikimwaga maji usiku hupoteza lita sitini (60) kwa kwa kila dakika moja, ni lita 3600 kwa kila saa moja, ni lita 18,000 kwa saa tano kutoka saa tisa usiku mpaka saa moja asubuhi pale wasamalia wema wanapoamua kufunga mpira wanapokuta inamwagika. Ndugu zangu ni lita 90,000 kama kitendo hicho kitatokea mara tano kwa wiki.
Unaweza ukaona ni kiasi gani cha maji kinaweza kupotezwa na huyu mtu mmoja pekee, na kama wapo watu mia moja wanaofanya vitendo hivi wanauwezo wa kupoteza lita 9,000,000 za maji kwa siku tano tu za wiki ambazo ni sawa na lita 36,000,000 za maji ndani ya siku ishirini za mwezi.
Ndugu zangu hakuna asiyejua jutihada zilizofanywa na serikali ya awamu ya tano katika upande wa maji na maeneo mengine. Pamoja na jitihada zote hizi zinazoongozwa na muheshimiwa rais Magufuli bado wanatokea watu wachache kuhujumu jitihada zote hizi. Kinachotokea hapa ni kuwa maji yanayotarajiwa yawafikie wananchi hayafiki tena, yanakuwa machache, uhaba wa maji unatokea katika vyanzo vya maji na maji kukatika katika kila wakati.
Ndugu zangu uzalendo ni pamoja na kuwa kama watch dog kuangalia mahala popote ambapo nchi inahujumiwa huu ndiyo uzalendo, uzalendo ni kuhakikisha rasilimali za nchi zinatumiwa ipasavyo na kuripoti vitendo vya hujuma kama hivi.
Muheshimiwa rais anahangaika kila siku kutuletea maendeleo badala yake wanatokea wachache kama hawa kutukwamisha.
Napenda kuomba mamlaka husika zifuatilie swala hili na wahusika wachukuliwe hatua kali ili iwe fundisho kwa wote wenye vitendo vya namna hii.
Naomba kuwasilisha,
Ni mimi mtanzania mzalendo ninaeipenda nchi yangu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi ni raia mwema nimeamua kutoa taarifa kwa mamlaka zinazohusika kuhusu kijana maarufu kwa jina la Mudi Chavi ambaye kwa muda mrefu sasa amekuwa akijishughurisha na uuzaji maji maeneo ya Mwananyamala Mchangani mtaa wa Juhudi.
MBINU ANAZOTUMIA KUJIPATIA MAJI.
Amekuwa akiihujumu DAWASCO kwa muda mrefu sana. Na mbinu anazotumia kujipatia maji ni kukata mipira ya maji ntakati za usiku na kuunganisha kwenye mipira yake ambayo inakwenda kujaza matank ya maji anayomiliki na baadae kuuza kwa wananchi.
HASARA ANAZOSABABISHA.
Licha ya kuwa anaharibu miundombinu ya DAWASCO lakini pia amekuwa akichangia upotevu mkubwa wa maji, kwani mara nyingi anapokuwa amekata mipira hushindwa kuifunga na kuacha maji yakitiririka muda mrefu sana all night long. Maji nyakati za usiku huwa na presha kubwa kitu ambacho kinamuwia vigumu kurejeshea mpira anaokuwa ameukata. Mpaka naandika taarifa hii leo asubuhi wakati naenda mihangaukoni nimekutana na madimbwi makubwa ya maji huku moja ya mpira ukiwa unatirirsha maji kwa kasi ya ajabu. Ninaposema madimbwi naomba nieleweke ni madimbwi kweli kweli just like public swimming pool.
MAJI YANAYOPOTEA KIMAHESABU.
Ndugu zangu ipo hivi, kwa presha ya maji nyakati za usiku makadirio ya haraka kwa mipira hii midogo ya kawaida inaweza ikatiririsha lita moja za maji kwa kila sekunde, maana yake hapa ni kwamba kila anapoacha mipira ikimwaga maji usiku hupoteza lita sitini (60) kwa kwa kila dakika moja, ni lita 3600 kwa kila saa moja, ni lita 18,000 kwa saa tano kutoka saa tisa usiku mpaka saa moja asubuhi pale wasamalia wema wanapoamua kufunga mpira wanapokuta inamwagika. Ndugu zangu ni lita 90,000 kama kitendo hicho kitatokea mara tano kwa wiki.
Unaweza ukaona ni kiasi gani cha maji kinaweza kupotezwa na huyu mtu mmoja pekee, na kama wapo watu mia moja wanaofanya vitendo hivi wanauwezo wa kupoteza lita 9,000,000 za maji kwa siku tano tu za wiki ambazo ni sawa na lita 36,000,000 za maji ndani ya siku ishirini za mwezi.
Ndugu zangu hakuna asiyejua jutihada zilizofanywa na serikali ya awamu ya tano katika upande wa maji na maeneo mengine. Pamoja na jitihada zote hizi zinazoongozwa na muheshimiwa rais Magufuli bado wanatokea watu wachache kuhujumu jitihada zote hizi. Kinachotokea hapa ni kuwa maji yanayotarajiwa yawafikie wananchi hayafiki tena, yanakuwa machache, uhaba wa maji unatokea katika vyanzo vya maji na maji kukatika katika kila wakati.
Ndugu zangu uzalendo ni pamoja na kuwa kama watch dog kuangalia mahala popote ambapo nchi inahujumiwa huu ndiyo uzalendo, uzalendo ni kuhakikisha rasilimali za nchi zinatumiwa ipasavyo na kuripoti vitendo vya hujuma kama hivi.
Muheshimiwa rais anahangaika kila siku kutuletea maendeleo badala yake wanatokea wachache kama hawa kutukwamisha.
Napenda kuomba mamlaka husika zifuatilie swala hili na wahusika wachukuliwe hatua kali ili iwe fundisho kwa wote wenye vitendo vya namna hii.
Naomba kuwasilisha,
Ni mimi mtanzania mzalendo ninaeipenda nchi yangu.
Sent using Jamii Forums mobile app