Kuhoji sio dhambi

Kuhoji sio dhambi

Ndenji five

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2021
Posts
1,985
Reaction score
3,120
Nakumbuka enzi za hayati rais Magufuli
Alituambia kusafiri kwenda nje kuna gharimu sana pesa

Ndio maana yeye hakutaka kusafiri
Ila sasa mambo yamekuwa tofauti utawala huu

Nauliza tu mimi kama mwananchi na sina lengo baya na kama nitakuwa tofauti tusameheane

Hivi hizi safari za huyu mheshimiwa rais wa sasa gharama anatumia zipi?

Ni hizi hizi kodi zetu au kuna misaada ya wahisani

Hivi Anapo endaga nchi za wenzetu huwa anapata mialiko au?

Msije kuninukuu vibaya mm ni mwananchi nahitaji nijue utaratibu wa nchi yangu unavyoenda

Mana haiwezekani hata kidogo nikae kimya ikiwa huyu rais yupo kwajili yangu mwananchi alafu nishinde kujua

Kama ni kodi zetu mama hapana unatuumiza sana na sio haki hata kidogo ndio ulisema unaenda kututafutia na kutuletea kwa faida ya nchi

Mheshimiwa tutaishi kwa misaada hadi lini?
 
Umuhimu wa kusafr unakuja kwenye ku close deals

Manepari na mashirika makubwa wasingependab kufanya final deal na subordinate wangependa zaidi kuongea na muhusika ili kupata uhakika wa Uwekezaji au fedha wanazotoa

Nimeona kwenye mikataba ya fedha nying wakuu wa taasisi hizo huwepo hivyo ni jambo muhimu na lenye uzito kabla mwekezaji hajajua kuleta fedha zake kuonana na Mkuu wa nchi pia inampa assurance
 
Mwache Mama airudishe Tz kimataifa, yule mzee unayefikiri wewe kwamba alikuwa hasafiri ili kubana matumizi ndiye aliyelifikisha deni la serikali kwenye Trilion 78, huku akitekeleza miradi ya wizara moja tu kati ya 27!

Tukaambiwa serikali inajenga miradi kwa fedha za ndani wakati kila uchao waziri wetu alikuwa anafuatia mikopo!

Mbona hukuhoji misafara mikubwa hadi ya kusindikizwa na helikopta, gharama zake zilikuwa ngapi? Au ni leo ndo umekuwa mwananchi wa Tz?

Mwacheni mama arudishe mahusiano yetu na dunia kwani hatuwezi kuishi kama kijiji!
 
Umuhimu wa kusafr unakuja kwenye ku close deals
Manepari na mashirika makubwa wasingependab kufanya final deal na subordinate wangependa zaidi kuongea na muhusika ili kupata uhakika wa Uwekezaji au fedha wanazotoa
Nimeona kwenye mikataba ya fedha nying wakuu wa taasisi hizo huwepo hivyo ni jambo muhimu na lenye uzito kabla mwekezaji hajajua kuleta fedha zake kuonana na Mkuu wa nchi pia inampa assurance
Je ni kwa gharama za nani?
 
Mwache Mama airudishe Tz kimataifa, yule mzee unayefikiri wewe kwamba alikuwa hasafiri ili kubana matumizi ndiye aliyelifikisha deni la serikali kwenye Trilion 78, huku akitekeleza miradi ya wizara moja tu kati ya 27!
Tukaambiwa serikali inajenga miradi kwa fedha za ndani wakati kila uchao waziri wetu alikuwa anafuatia mikopo!
Mbona hukuhoji misafara mikubwa hadi ya kusindikizwa na helikopta, gharama zake zilikuwa ngapi? Au ni leo ndo umekuwa mwananchi wa Tz?
Mwacheni mama arudishe mahusiano yetu na dunia kwani hatuwezi kuishi kama kijiji!
Pesa alikuwa anatoa wapi?
 
Ni kwa gharama za kodi yako ndiyo, na nchi zote duniani ndivyo zinavyofanya. kuna faida na hasara, huwezi kuogopa hasara wakati kuna uwezekano wa kupata faida. tafakari.
Sawa sijapinga ila safari zimezidi huku nchi hali ya maisha ikiwa tete
 
Hayati JPM aliwahi kusifia safari za JK nje ya nchi kwamba zinaleta maendeleo nchini hivyo aendelee kusafiri sana tu wenye wivu wajinyonge.
 
Hayati JPM aliwahi kusifia safari za JK nje ya nchi kwamba zinaleta maendeleo nchini hivyo aendelee kusafiri sana tu wenye wivu wajinyonge.
Shida sio kusafiri shida hizo gharama za safari pesa inatoka wapi? Mimi sijapinga kusafiri kwake
 
Hivi ilishawahi kufanyika tathmini ya safari za ndani za Mkuu wa Nchi hasa kipindi cha Mwendazake?

Ule msafara ulivyokua ma magari zaidi ya 80 mengi yakiwa ma V8 ulikua unawaf
gharimu walipa kodi wa nchi hii kiasi gani?
 
Back
Top Bottom