kwa anayejuwa gharama za kuchimbiwa kisima kwa hapa Dar ni shilingi ngapi?
Kwa mfano mita 60 ni shilingi ngapi?
80, 100, 120 na 150 je? Mawasiliano pls
je na huduma ya survey inakuaje?
Mita 60--ml 3.5
-----80--ml 4
-----100--ml 6
-----120-- ml 7.2
-----150-- ml 12
Survey laki 250
Mwenye kisima atajuaje (atathibitisha vp) kuwa kisima kilichochimbwa ni 100m na siyo 63m?
Mita 60--ml 3.5
-----80--ml 4
-----100--ml 6
-----120-- ml 7.2
-----150-- ml 12
Survey laki 250
habari mkuu, naomba kuuliza hiyo gharama kwa dar ni kuchimba kisima peke yake au na vifaa vyote mpaka kisima kuwa tayari kwa matumizi? na kwa sehemu kama ifakara wilaya ya kilombero ni sh. ngapi kuchimba if possible na gharama ya mpaka kisima kuwa tayari kwa matumizi.
Hata makazini, kuna point inafikia huwa imani tu ndo inafanya kazi... Wakiamua kukuchimbia mita 80 wakati umelipia mita 100, wanaweza... Tena na yale makelele ndo utachanganyikiwa tu kuhesabu mabomba yanayozama chini..Mwenye kisima atajuaje (atathibitisha vp) kuwa kisima kilichochimbwa ni 100m na siyo 63m?
Ni gharama za kuchimba kisima tu pump na vifaa vingine utanunua mwenyewe sbb gharama zinatofautiana kutokana na ubora hivyo sisi tutakupashauri ununue pump ya uwezo gani kufatana na wingi wa maji yatakayopatikana
mkuu ahsante sana tuko wengi! mfano kwa siku natumia litre 30,000 je? kitaweza kuhimili matumizi haya kwa mda gani kabla ya kukauka?
Mita 60--ml 3.5
-----80--ml 4
-----100--ml 6
-----120-- ml 7.2
-----150-- ml 12
Survey laki 250
Unaweza kutumia wiki nzima mfukukizo bika kuzima pump na yasipungue hata kidogo Kisima hakikauki kirahisi labda kiwe kifupi lkn ni nadra sana kisima kirefu kukauka labda iwe miujiza sbb ya mungu mengi
Sehemu zote tunachimba ila lazima ufanye survey ila kwa maeneo yenye miamba migumu inaweza kufika mpaka laki 150 kwa mita
Pumpu nzuri inaweza kufika mpaka ml 1.6 kwa brand za kitaliano na denmark
Mkuu hebu dadavua kidogo: Je wakati wa survey unaweza jua iwapo maji yatakayopatikana hapo yatakuwa baridi au ya chumvi? Na je wawezajua wingi wa maji yaliyoko?
Kuna sehemu moja kule mkoa wa Pwani ambapo kuna attempt 3 za kuchimba maji zimefanyika katika eneo fulani bila mafanikio. Ninacho kijua ni kuwa kabla ya kila uchimbaji kulikuwa na survey na jamaa walijinasibu kuwa maji yatapatikana lakini wapi. Na mimi nahitaji kuchimba kisima changu huko ila naogopa sana nisije nikapoteza pesa zangu. Je unanishaurije ili angalau niwe na matumaini kuwa pesa yangu haitapotea bure? Kisima nahitaji.
Sasa kama ni hivyo hiyo survey ni ya nini au ni ya kujua gharama za uchimbaji kama hapa pagumu pana mwamba au laPwani sehemu gani
Survey haiwezi kujua kama ni baridi au chumvi wala kujua kwa uhakika utapata liter ngapi labda ungesema ni eneo gani inawezekana tukapata ufumbuzi
Sasa kama ni hivyo hiyo survey ni ya nini au ni ya kujua gharama za uchimbaji kama hapa pagumu pana mwamba au la