Kuchapisha shahada nchini ni mpango wa CCM- Lipumba

Josh Michael

JF-Expert Member
Jun 12, 2009
2,523
77
SIKU moja baada ya serikali kutangaza kuwa, itaanza kuchapisha nyaraka za kupigia kura nchini, kwenye chaguzi zijazo, wabunge na madiwani wa CUF wamedai kuwa, hiyo ni mbinu nyingine ya kukipa chama tawala ushindi wa tsunami.

Mwenyekiti wa CUF Profesa Lipumba, aliiambia Mwananchi jana kuwa, serikali imebuni mbinu hiyo baada ya kugundua kuwa, upepo wa kisiasa katika uchaguzi ujao uliopangwa kufanyika Oktoba 2010, utakuwa mbaya kwa CCM na kuwepo uwezekano wa kushindwa.

�Utaratibu huu wa kuchapisha karatasi za kura nchini, unaonyesha dhahiri kuwa unalenga kuisadia CCM na kwa mbinu hii itapata ushindi wa tsunami, tofauti na ule wa kishindo wa mwaka 2005,� alisema Prof Lipumba.

Prof Lipumba alifafanua kuwa, kitendo cha serikali kutoshirikisha vyama vya upinzani katika mazungumzo yoyote ya uanzishwaji wa utaratibu huo, kinaonyesha kuwa ina lengo la kuipendelea CCM.

�Na kwa vyovyote vile CCM itakuwa iliujua mapema mpango huu wa kuchapisha karatasi za uchaguzi nchini na kwa hiyo imeshajipanga,� alisema Prof Lipumba.

Pia Profesa Lipumba alisema ana shaka na usalama utakaokuwepo wa kuzitunza karatasi hizo.

�Sijui utunzaji wa karatasi hizi utakuwaje, maana serikali inayotawala ni ya CCM na sisi kama wapinzani hatujashirikishwa katika lolote,� alisema Prof Lipumba.

Serikali imesema itaanza kuchapa karatasi hizo ndani ya nchi, baada ya kupatikana kwa mitambo mipya na ya kisasa yenye uwezo wa kuweka alama za siri, namba na rangi katika karatasi za kura kwa usalama mkubwa na uwezo wa kuhakiki alama za siri zitakazowekwa.

Kazi hiyo itatekelezwa na Idara ya Mpigachapa Mkuu wa Serikali, ambayo iko chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu ikishirikiana na Tume ya Uchaguzi ya(Nec).
Ununuzi wa mitambo hiyo, ni mpango wa serikali wa kutaka kuimarisha idara hiyo tangu mwaka jana na serikali ilitoa zaidi ya Sh1.7 bilioni kwa ajili ya idara hiyo na mwaka huu imetenga zaidi ya Sh1 bilioni ili kutekeleza mpango huo, ambao unaondoa gharama kubwa za kuchapisha karatasi hizo nje ya nchi.
 
Lipumba ana hoja ya msingi iwapo wao kama wapinzani hawajashirikishwa.

Ila sioni ni kwa nini haelekezi malalamiko yake Tume ya Uchaguzi na badala yake anaishutumu CCM. .!!
 
Lipumba ana hoja ya msingi iwapo wao kama wapinzani hawajashirikishwa.

Ila sioni ni kwa nini haelekezi malalamiko yake Tume ya Uchaguzi na badala yake anaishutumu CCM. .!!
Tume ya uchaguzi si tume huru...na hili limekuwa likilalamikiwa mara kwa mara...kwa hiyo ni ngumu sana kutofautisha tume na chama tawala...nadhani hiyo ndio hoja ya Prof.
 
Dawa moja hapa ni Wapinzania KUDAI TUME HURU YA UCHAGUZI, HUWEZI KUTAYARISHA KARATASI ZA KUPIGIA KURA WEWE MWENYEWE WAKATI WEWE MWENYEWE NI REFA, HEKO LIPUMBA
 
Kutokana na mie kwa uchunguzi wangu mdogo na mawazo yangu,, naona hapa serikali ya CCm imebuni mpango mpya wa kuiba kura kupitia hizo shahada. Maana kama wana weza kununua shahada watashindwaje kujichapishia nyingi na kugawa kwa mamluki wao??? Ndugu zangu wanajamii hebu fikirieni hilo mkioanisha na Matukio ya Zanzibar sasa hivi.
 
Sasa hakuna haja ya kwenda kwenye uchaguzi maana utakuja kuona kuwa tayari wao wameshafanya uchaguzi
 
Kazi hiyo itatekelezwa na Idara ya Mpigachapa Mkuu wa Serikali, ambayo iko chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu ikishirikiana na Tume ya Uchaguzi ya(Nec).

Hii ndo sentensi inayotisha na ndicho Lipumba hapendi. Ofisi inayochapisha iko chini ya PM. PM ni mwanachama wa CCM. Hivyo hii inampa uwezo mkubwa wa kucheza rafu. Watatengeneza karatasi nyingi na kuziweka CCM. Kura itapigwa lakini majibu tayari. Kudadadeki! Ndo Afrika hiyo...
 
Mawazo ya kipuuzi kabisa...

Kwanzi kura zikichapishiwa nje si unaweza agiza zaidi?

Yaani kitu kikichapishwa nje ndio nini?
 
Hii ndo sentensi inayotisha na ndicho Lipumba hapendi. Ofisi inayochapisha iko chini ya PM. PM ni mwanachama wa CCM. Hivyo hii inampa uwezo mkubwa wa kucheza rafu. Watatengeneza karatasi nyingi na kuziweka CCM. Kura itapigwa lakini majibu tayari. Kudadadeki! Ndo Afrika hiyo...


Du! Kama hivi ndivyo tunavyotaka kufirikia mimi simo kwenye group la kufikiria hivyo!!1
 
Mawazo ya kipuuzi kabisa...

Kwanzi kura zikichapishiwa nje si unaweza agiza zaidi?

Yaani kitu kikichapishwa nje ndio nini?

Du! Kama hivi ndivyo tunavyotaka kufirikia mimi simo kwenye group la kufikiria hivyo!!1

U missed the point mh. Point ni kwamba katika system yetu, Chama na Serikali ni kitu kimoja. Watu hawana imani na kitu kinachofanywa na serikali kutokana na hii link. Serikali ime-abuse nguvu yake kwa muda mrefu kwa kuendeleza agenda cha chama kimoja. Mfano rais kufanyia vikao vya chama ikulu, polisi kupendelea chama kimoja, nk. Hili ni jambo la kusikitisha na ambalo inabidi lishughulikiwe. Public bodies kama hii NEC, iko biased. Swali ni nini kifanyike kuwe na uwazi zaidi?
 
Huwezi wewe mwenyewe ukawa mchezaji then wewe refa na pia wewe pia hakimu hivyo unategemea nini hapa
 
Back
Top Bottom