Kuboresha elimu yetu ni pamoja na lugha ya kufundishia

Mpira wa kona

JF-Expert Member
Nov 25, 2016
350
338
Wadau wa Elimu nashindwa kuamini kuwa kweli tumeshindwa kuboresha Elimu katika Nchi Yetu.Binafsi naamini matatizo makubwa ya Elimu Yetu ni pamoja Na Lugha Rasmi ya kufundishia toka Shule ya msingi mpaka Vyuoni.

Kwa sasa Kiswahili ndio lugha rasmi ya kufundishia Shule ya msingi Kwa masomo yote isipokuwa somo la kiingereza.Shule za sekondari lugha rasmi ni kiingereza Kwa masomo yote isipokuwa kiswahili.

Hoja yangu ni kwamba kiingereza ktk Shule ya msingi hakifundishi Kwa kina hali ambayo mwanafunzi anafika sekondari hajui kuakiandika kukisoma Na kukizungumza.Na awapo sekondari anakutana na masomo yote Kwa kiingereza isipokuwa kiswahili je atayaelewa masomo hayo? Nadhani serikali iliangalie vema hili la lugha ya kufundishia
 
Nafikiri hili linatakiwa lijadiliwe bungeni na wabunge waje na nondo za kutosha ktk utetezi wa pande zote.

Binafsi ningependelea lugha ya kufundishia iwe kiingereza msingi mpk chuo
 
nafikiri hili linatakiwa lijadiliwe bungeni na wabunge waje na nondo za kutosha ktk utetezi wa pande zote.
Binafsi ningependelea lugha ya kufundishia iwe kiingereza msingi mpk chuo
Wabunge wa darasa la saba na form 4 and 6 failure, university discos,
 
Back
Top Bottom