Kuagiza mbwa toka SA

Kuagiza mbwa toka SA

Buza

Member
Joined
Aug 7, 2011
Posts
57
Reaction score
14
Naulizia anayefahamu utaratibu wa kuagiza mbwa kutoka South Africa?
 
Naulizia anayefahamu utaratibu wa kuagiza mbwa kutoka South Africa?

Mkuu Buza, unaagiza mbwa kwa ajili ya shughuli gani? Ulinzi au kama pet?

Ni breed gani ya mbwa unatafuta? Awe na umri gani na jinsia gani?

Malengo yako ya baadaye na huyo mbwa ni nini kuzalisha au kutokuzalisha?
 
Nahitaji boerboel puppy kwa ajili ya ulinzi home akikua. Lakini Nahitaji kuzalisha ili niuze puppies kufidia gharama za matunzo.
 
agiza rhodesia ridgeback ndio wazuri kwa ulinzi. matunzo ni muhimu lakini... sio kuwapa mabaki ya kiti moto au mifupa ya makongoro.. be prepared. nenda mali asili & mifugo wizarani watakupa info zote. all the best.
 
Nahitaji boerboel puppy kwa ajili ya ulinzi home akikua. Lakini Nahitaji kuzalisha ili niuze puppies kufidia gharama za matunzo.
.

Wanauzwaje mkuu hao boerboel? Unahitaji kwenda wizara ya Mifugo ili upate Import Permit ya kuingiza mbwa toka nje ya nchi. Katika hicho kibali utahitajika uwe na (1): Details za mbwa e.g Jina la mbwa, Breed ya mbwa, Gender ya mbwa, tarehe ya kuzaliwa ya mbwa.

(2): Chanjo zilizo kamilika za mbwa DHLP, D=Distemper, H=Hepatitis, L=Leptospirosis na Rabies vaccination(ambapo chnjo ya kwanza ya Rabies inatolewa mbwa akiwa na umri wa miezi 3).

(3): Internal and external parasites.

Hizi documents zinatakiwa zitolewa na Veterinary wa serikali tokea huko South Africa.

Mbwa anaposafirishwa toka SA anatakiwa awe accompanied na hizo original documents.

Fuatilia zaidi toka Wizara ya Mifugo hapo Dar es salaam.
 
Asante tundapori, lakini nataka kijua breeders wa ukweli.
 
Asante tundapori, lakini nataka kijua breeders wa ukweli.

Hapo ndiyo mtihani mkubwa ulipo, vinginevyo ujiandae kuingizwa mitaani. Labda uwe na jamaa SA anayejuamambo ya mbwa.

Import permit inayotolewa na wizara ya mifugo nafikiri inagharimu TSh 40,000/= valid for 30 days only from the date of issue of Import Permit, kwa hiyo inahitaji maandalizi mazuri na ya kuaminika.

Unategemea kumleta Tanzania kwa usafiri gani? Kama ni kwa ndege watu wa ndege wanaweza kuwa na masharti yao e.g asiwe na umri chini ya miezi mitatu na kreti maalum ya kusafirishia mbwa.

Mimi nategemea kuagiza Rottweiler toka Ulaya kuna jamaa yangu anabeba mabox huko, atakuwa mjamzito na atajifungulia bongo!
 
Hapo ndiyo mtihani mkubwa ulipo, vinginevyo ujiandae kuingizwa mitaani. Labda uwe na jamaa SA anayejuamambo ya mbwa.

Import permit inayotolewa na wizara ya mifugo nafikiri inagharimu TSh 40,000/= valid for 30 days only from the date of issue of Import Permit, kwa hiyo inahitaji maandalizi mazuri na ya kuaminika.

Unategemea kumleta Tanzania kwa usafiri gani? Kama ni kwa ndege watu wa ndege wanaweza kuwa na masharti yao e.g asiwe na umri chini ya miezi mitatu na kreti maalum ya kusafirishia mbwa.

Mimi nategemea kuagiza Rottweiler toka Ulaya kuna jamaa yangu anabeba mabox huko, atakuwa mjamzito na atajifungulia bongo!
DUU Mbwa wamekuwa adimu namna hiyo jamani kiasi cha kutolewa mpaka Ulaya. Mbona naona breeds nyingi tu zinapatika Tanzania?
 
Ukifanikiwa tundapori tujuzane. Rott ni wazuri pia kwa ulinzi ila nasikia si wazuri sana Kama nyumba Ina watoto wadogo.
 
Ukifanikiwa tundapori tujuzane. Rott ni wazuri pia kwa ulinzi ila nasikia si wazuri sana Kama nyumba Ina watoto wadogo.
Si Kweli Mkuu. Rot is one of the Best breed i have ever met. Ni msikivu sana. Nililia sana pale alipogongwa na gari akiwa na miezi minne unusu. Alikuwa nirafiki wangu wa ukweli na rafiki kwa wanangu
 
Si Kweli Mkuu. Rot is one of the Best breed i have ever met. Ni msikivu sana. Nililia sana pale alipogongwa na gari akiwa na miezi minne unusu. Alikuwa nirafiki wangu wa ukweli na rafiki kwa wanangu
Itakuwa amechanganya kati ya Rot na Pitbulls. Mimi nina well trained 4 German Shepherds...wawili wana miaka 4 na wawili wana miaka 2. Kuna jamaa waliingia nyumba ya jirani kuiba usiku, katika purukushani za kukimbizwa mmoja akakosea akaruka ukuta na kuingia nyumbani kwangu. Mbwa walimkalisha kimya kimya...kila akitaka kuinuka akimbie anapigwa meno anarudi chini kimya. Mpaka mlinzi anakuja kumkuta jamaa yuko hoi hatamaniki. Uzuri wa GS huwa hawapigi kelele wakifanya yao..utakuta tu mtu yuko hoi.
 
Back
Top Bottom