Kova na Mwema mnalifahamu hili?

GAGL

JF-Expert Member
Aug 5, 2010
390
392
Napenda kulishukuru Jeshi la polisi kwa huduma za afya mnazotoa hapa baracks kurasini. Lakini kuna mambo ya ajabu hapa. Raia wa kawaida wanapoenda kutibiwa hapa kwa huduma ambayo wanailipia, wanatozwa gharama kubwa kinyume na gharama halisi kwa kuambiwa wakanunue dawa kwenye famasia iliyokaribu na kilwa pub. Mfano, shangazi yangu alienda kutibiwa malaria na presha pale, akaambiwa atoe sh 3000 kwa ajili ya dawa mseto ya malaria ambayo kihalisia inauzwa sh 600. Na kwa maelezo ya wizara ya afya, dawa hii inatakiwa kuuzwa vituo vya afya vya serikali tu au na vile vilivyothibitishwa. Kwa hapa dawa hii utaambiwa imeisha ila inapatikana famasia iliyopo hapa kilwa pub ambayo naamini ni mradi wa baadhi ya madaktari. This is against the law and it is pure corruption.
 
Hii ni typical case of Conflict of Interest at play!! Conflict of interest, njia mojawapo inaweza ikaonekana pale ambapo tuseme Mzee Bakhressa kamajiri kijana akamuuzie mikate yake pale kariakoo na mwisho wa siku hupewa ujira faida ya utumishi wake huo.

Sasa pale inpotokea kwamba kijana huyu naye kajichagulia kujifungulia banda la kuuza mikate labda tuseme pale mtaa wa swahili kwa lengo kama lile lile la muajiri wake (kujipatia faida zaidi kihalali na kuweza kujikimu kimaisha), kwake huyu kijana uhalali wa biashara yake unatowekea kwenye ule mlango wa kudiriki kumnyima tajiri wake biashara kwa kuelekeza wateja wanaotembelea duka la tajiri wake waende mtaa wa pili kuna ka-kibanda vijana fulani mle wanauza mikate freshi na mizuri kweli kweli!!! Huu ni hujuma hatari sana ambao haukubaliki kwenye bishara hata kidogo.

Watumishi wengi wasio waaminifu huwaangusha mabosi wao kwa mtindo huo huo na kukifika mwisho wa mwezi tena bila hata aibu ndio huyo tena katia timu na madai ya 'nipe mshahara wangu' yakiwa yamenin'inizwa mbeeeele kama tai - jambo kama laiti ingalikua imenaswa na timu ya Masanja Mwanawane lazima mtu ungesikia kemeo kali sana pamoja na hitimisho la 'wizi mtupu!!!'

Miongoni mwa mbinu chafu zinazofanya biashara nyingi zisiweze kupaa hata umbali wa kimo cha ndama kuelekea kwenye malengo waliyojiwekea ni pamoja na mbinu mbali mbali chafu za mgongano kimaslahi kama vile mwajiriwa anapochagua am kwa kudai kwamba mkate hamna, au kafanya mkate wa tajiri uwe wa ghali zaidi kwa kujiongeze yake kitenesi pale juu, au hata kuhujumu mikata ya tajiri kwa kuiingizia dosari kama vile kuweka memnde mle - japo haya kwa Bakhresa naamini hayajawahi kutokea hata siku moja na ninampongeza kwa kutupa ajira.

Lakini kwa kuwa mbele ya sheria hamna kesi dogo, hebu kakimbilie mara moja pale Upanga nyuma kidogo ya kituo cha daladala cha Palm Beach kushoto unavyoelekea Mwenge; kula kona pale kwenye kale kakichochoro kisha ukaandike herufi 'Z' kali pale baada ya kupita geti la jeshi na kushoto mwako tu utaona geti la kijani lenye sura ya kama ka chukizo fulani hivi - mle ndani kuna Mtanzania mmoja hivi ambaye ni a Down-to-earth soft-spoken but highly critical minded gentleman aitwaye Hosea na ninaamini salamu nzito zitatua pale zahanati ya polisi Kurasini ili iwe fundisho kwa wafanyakazi wengine ambao huendeleza usemi wa Ali Choki (Chako chako na changu pia ni chako) kwenye kazi za watu.

Mzee Kova japo ni polisi mkubwa na ni mtumishi hodari sana ambaye kamwe hatosahauliwa na majambazi wa Mbeya na Tunduma, vile vile kiutendaji ndiye mwenye zahanati ya Kurasini, lakini mgawanyiko wa kazi unamzuia kukamata hao madaktari na minesi Makanjanja wa huko Kurasini kwa madai kama haya.

Kumbukumbu zinaonyesha kwamba Ndugu Dr Hosea, sawa sawa na kaka yake Ndugu Dr Magufuli naye kashindwa kabisa kuonyesha umakini na makali yake katika kazi hiyo ya kuzuiya rushwa nchini kutokana na sababu zile zile zilizomzuia John Magufuli majuzi kubomoa majengo yanayotusababishia foleni kwenye hifadhi ya barabara. Ndani ya CCM ni kwamba kama maslahi ya FISADI fulani imeguswa basi watendaji huombwa kuzingatia zaidi UBINADAMU kuliko SHERIA mstari kwa mstari.

Mpe pole sana shangazi.
 
Back
Top Bottom