Kosa mnalolifanya CHADEMA!!

Kosa mnalolifanya CHADEMA!!

Tuko kwenye hatua ya kupigia kura Katiba Pendekezwa. Katiba ya wananchi ilizikwa Dodoma. UKAWA ipo pale pale ilihali UKUTA ni operation ya CHADEMA.
Ni sawa lakini mbona kuna ubaguzi kwenye UKUTA, Kwa nini tusiungane kam tulivyo ungana kwenye katibaaaaa
 
Acheni Wandamane, nahitaji wateja kwenye Pharmacy yangu hapa Mwananyamala Hospital
Polisi wanajiandaa na Mabomu, Chadema wanajiandaa na Mabango na viroba nami najiandaa na Plaster, Bandeji, pain killers n.k najua sikosi wateja kuanzia tarehe 1 September
 
Acheni Wandamane, nahitaji wateja kwenye Pharmacy yangu hapa Mwananyamala Hospital
Polisi wanajiandaa na Mabomu, Chadema wanajiandaa na Mabango na viroba nami najiandaa na Plaster, Bandeji, pain killers n.k najua sikosi wateja kuanzia tarehe 1 September
kufa kufaana.
 
Lakini kwanini tuvitenge Vyama vingine??
Hatujavitenga, nafikiri kama ulimsikia mwenyekiti Mbowe alisema kwenye hili la Ukuta tunawakaribisha vyama vyote, asasi za kiraia, taasisi na wale wasiokuwa na vyama
 
Mkuu nimekukubali sana viongozi wa chadema hebu warudieni washirika wenu kuwaomba radhi Na kuwaomba wawaunge mkono kwani kidole kimoja hakivunji chawa
 
Chadema tokaikubari mafisadI imebakia kutapata tuuu maraukuta hukuwanainchi HaWana mdaaa na maukuta Yao. Haaaahaaa wanainchii wqmesharidhika na kasi ya jpm wala hawanampangoo na maaandamanoo. Na rare he moja itakuwa nI aibuuu kuuu kwa chademaa wataandamana mafisaid tuuu haaaahaaaaa
 
Tuko kwenye hatua ya kupigia kura Katiba Pendekezwa. Katiba ya wananchi ilizikwa Dodoma. UKAWA ipo pale pale ilihali UKUTA ni operation ya CHADEMA.
Chadema haina ajenda nzuri na vyama vinavyounda ukawa, nakumbuka barua ya siri iliyovuja ikisainiwa na Mwalimu, na hamkuwahi kuikanusha, mnachofanya sasa kina maudhui ya ile barua, mnataka mmoja wa vyama vya vya upinzani lakini umoja huo uwe wa kuwajenga nyinyi chadema huku ukiviangamiza vyama vingine, wakati wa uchaguzi mliwasumbua sana CUF kwenye majimbo yalioonekana wana nguvu mkatumbukiza wagombea wenu kinyume na makubaliano mkiwa na lengo moja tu wenzenu washindwe mbaki kuwa wapinzani wakuu, na ata leo mnaendesha operations hizi kivyenu mkiwa na ajenda ya kujiimarisha nyinyi zaidi kuliko wenzenu, Mbatia mmefanikiwa kumfanya mbuzi wa kafara lakini CUF sijui itakuwaje.
 
Acheni Wandamane, nahitaji wateja kwenye Pharmacy yangu hapa Mwananyamala Hospital
Polisi wanajiandaa na Mabomu, Chadema wanajiandaa na Mabango na viroba nami najiandaa na Plaster, Bandeji, pain killers n.k najua sikosi wateja kuanzia tarehe 1 September
Fikra za kijinga hizi, huoni kuwa vurugu zikitokea huwa wanajeruhiwa hata walio majumbani ambao hawakuwepo kwenye maandamano?
Subiri uje umpe mkeo hizo bandeji baada ya kuangukiwa na kitu chenye ncha kali wakati anaosha vyombo nyumbani
 
Chadema haina ajenda nzuri na vyama vinavyounda ukawa, nakumbuka barua ya siri iliyovuja ikisainiwa na Mwalimu, na hamkuwahi kuikanusha, mnachofanya sasa kina maudhui ya ile barua, mnataka mmoja wa vyama vya vya upinzani lakini umoja huo uwe wa kuwajenga nyinyi chadema huku ukiviangamiza vyama vingine, wakati wa uchaguzi mliwasumbua sana CUF kwenye majimbo yalioonekana wana nguvu mkatumbukiza wagombea wenu kinyume na makubaliano mkiwa na lengo moja tu wenzenu washindwe mbaki kuwa wapinzani wakuu, na ata leo mnaendesha operations hizi kivyenu mkiwa na ajenda ya kujiimarisha nyinyi zaidi kuliko wenzenu, Mbatia mmefanikiwa kumfanya mbuzi wa kafara lakini CUF sijui itakuwaje.
Sina uhakika na hoja yako. Ila ushirikiano kwenye masuala ya kitaifa hayana chama.
 
Watanzania walishaikataa hii katiba kwa kusema haitufai na ni mbovu sasa mtu akiivunja tunamlaumu kwa nini?
tusimlaumu anayeivunja katiba tumulaumu aliyetupa katiba mbovu
Na tuanze sasa kupigania katiba mpya !!

Kazi yangu ni kushauri na kuongea ukweli milele ?
Ingawa naunga mkono operations Ukuta lakini kuna makosa ya kimkakati ya Kutowashirikisha wana ukawa wote katika maandamano yenu !!
Haya maandamano yalitakiwa kuwashirikisha NCCR,CUF na NLD
Kitendo cha kuvitenga hivi vyama mnafanya makosa hapo !!

Mlipotuletea manifesto ya chama uchaguzi uliopita hatukuona mkileta manifesto zaidi ya moja hivyo Sera yenu ingeendelea kuwa moja tu ya kuviunganisha hivi vyama viwe na ajenda za kudumu kama
Kupigania Ufisadi
Kutafuta katiba mpya
Kutafuta tume huru ya uchaguzi
Kupambana na wavunja katiba mpya itakayopatika.

Tulishawai kuongea lugha moja kuwa katiba tuliyonayo ni mbovu na hatuiitaji tunachokitaka ni katiba mpya !!
Sasa kama tunataka katiba mpaya iweje twendelee kuipigania ya zamani tena tunayojua ni mbovu??

Mwacheni Rais avunje katiba hii aimalizie ili tutafute vizuri katiba mpya
Waiteni CUF ,NCCR na NLD tudai katiba mpya!!!
Ukawa ya kudai katiba ishakufa siku nyingi.
Hata hiyo katiba mpya (ya wananchi) hawaitaki...wanaitaka hiii hii iliyopo.
Huo umoja wa ukawa unaouongelea ulikuwa na umoja wa "genge la kampeni" ili kuiwezesha Chadema kupata kura na viti vingi zaidi.
Ukweli wa genge hilo na dhana yake umeiona mara tu baada ya uchaguzi.
Baadhi yetu tuliwashtukia siku nyingi sana.
 
Hatujavitenga, nafikiri kama ulimsikia mwenyekiti Mbowe alisema kwenye hili la Ukuta tunawakaribisha vyama vyote, asasi za kiraia, taasisi na wale wasiokuwa na vyama
Wanawakaribisha vyama vyote kwenye "move" ya chadema.
Hawakuvishirikisha, kufanya maamuzi pamoja au kupanga mikakati pamoja.
Hiyo ndiyo ilikuwa dhana ya "umoja wa katiba..." na sasa wanapigania "haki za kikatiba", wenzao wako wapi?
Hii janja ya nyani tushaing'amua.
 
Kweli katiba yetu ina shida kubwa! Lakini kufanikiwa kwa UKUTA pia kutaleta haja ya kutazamwa upya kwa katiba iliyopo!

UKUTA uko pale pale! 01.09.2016, Bado hakijazaliwa kiumbe chenye uwezo wa kuzuia UKUTA!
Vp na kutokufanikiwa kama dalili zinavyoanza jionyesha?
 
Back
Top Bottom