plan z
JF-Expert Member
- Jun 10, 2019
- 1,395
- 1,439
SIMU/WHATSAPP: 0768571786
Nilimuhurumia sana Lucyra jinsi alivyokua akiteseka kwa sababu yangu. Kiukweli sikumfanyia makusudi, utotoni sikumkubalia kwa sababu ya masomo na malezi yangu ya kiseminari lakini safari hii sikumpenda kabisa kwa sababu ya Leyra. Sikuogopa ujirani wa familia zetu wala ukaribu wa wazazi wetu nilimueleza Lucyra kila kitu wazi lakini kutokana na kuzidiwa na nguvu ya mapenzi alishindwa kabisa kunielewa tena kumuogopa kwangu Leyra ndio kulimpa moyo na kufanya azidi kusubiri jibu la ndio kutoka kwangu, jambo ambalo kiukweli lilikua haliwezekani.
Ukisema cha nini wenzako wanasema watakipata lini.
Kama ilivyokua kwangu kumuogopa Leyra kulivyompa moyo Lucyra ndivyo kumkataa kwangu Lucyra kulivyompa moyo Daniel, Cr wa darasa letu ambaye alitokea kumpenda sana Lucyra. Daniel na Lucyra walifahamiana tokea sekondari, walisoma darasa moja kidato cha tano na cha sita katika shule ya Mt. Mathias iliyopo jijini Dar es salaam.
Tokea huko Daniel alikua akimtaka Lucyra, alimueleza jinsi anavyompenda lakini mimi nilikua kikwazo, Lucyra alimkataa kwa sababu yangu lakini cha ajabu Daniel hakuacha wala hakuchoka kumpenda.
Mwanzo nilikua mbali na Lucyra nchini Kenya masomoni lakini Daniel alinifahamu sababu Lucyra alimwambia habari zangu. Safari hii nilikua karibu nae chuo kimoja darasa moja, Daniel aliogopa sana alijua wazi kama ningemkubali Lucyra basi huo ndio ungekua mwisho wake. Mimi kumkataa Lucyra aliona haitoshi aliamini asipofanya kitu ipo siku ningeweza kubadilisha mawazo yangu.
Mimi kumpenda Leyra kwa Daniel zilikua ni habari njema lakini kitendo cha kumuogopa ilikua habari mbaya kwake.
Njia sahihi ya kufanya hio izidi kua habari njema kwake ilikua ni mimi na Leyra kua karibu. Daniel alidhamiria kufanya kitu lakini hakujua afanye kitu gani, jambo hilo lilimuumiza kichwa kwa muda wa wiki mbili mpak Dr. Grosse alipokuja Darasani na kutaka Cr atengeneze makundi mbali mbali kwa ajili ya asaimenti alizokua ameziandaa.
Daniel hakutaka kuzubaa aliona hio ndio ilikua fursa pekee ya kuitumia kutengeneza ukaribu wangu na Leyra. Daniel alicheza kama Ronaldo, alinipanga kundi moja na Leyra bila kuogopa naye alijipanga kundi moja na Lucyra.
Lilikua jambo muhimu sana kwetu sote ingawa mwanzo lilinitesa sana kwa sababu ya aibu, kujizuia kubehua na kukohoa mbele ya Leyra. Japo niliteseka mwanzoni lakini mpango wa Daniel ulizaa matunda, polepole kama mwendo wa kobe nilianza kumzoea Leyra na ukaribu wetu mkubwa ukaanzia hapo.
“Hi naitwa Leyra Lacena” Leyra aliniambia baada tu ya kukutana kwenye kundi tulilipongiwa.
“Naitwa Alfred Kamba” kwa mara ya kwanza niliongea nae kama haitoshi tukasalimiana kwa kushikana mikono.
Labda kwa sababu wote tulikua tunapendana, ndani ya muda mfupi ukaribu wangu na Leyra ulikua mkubwa sana, kama mwendo wa saa mbovu lile jina la domogundi lilianza kupotea taratibu.Leyra alikua na kitu fulani cha pekee ndani yake achana na uzuri, tabasamu na uchangamfu aliokua nao. Ndani yake ni kulikua na nguvu fulani ya kutenda miujiza sababu kila sekunde niliyoongea nae nilisikia furaha ya ajabu, tabasamu lake lilitosha kunisahaulisha matatizo yangu yote, nilijiona mwepesi mwili mzima kana kwamba nilikua nimesamehewa dhambi zangu zote.
Wakati Tanzania ikipata uhuru wake mwaka 1961 mimi uhuru wangu niliupata hapo, polepole hali ya kujiamini ilikuja, nilianza kumtania Leyra, nikaanza kumshika kiuno, kumkumbatia na kumuangalia kwa uhuru zaidi bila kuibia kama hapo awali.
“Leyra wewe ni mzuri sana” nilimwambia kila mara tulipokutana, ushuzi ulipata mjambani kama utani na mimi domo zege nikawa nimeula.
Kila nilichofanya na kumwambia Leyra alikua akitabasamu hata siku moja sikuwahi kumuona akiwa amekasirika.
Pamoja na mambo yote hayo kumwambia Leyra kua nampenda nilishindwa, nilitamani kumwambia Leyra kua nampenda sana na naomba awe mpenzi wangu lakini nilishindwa kabisa. Kila nilipotaka kumwambia maradhi yangu ya aibu yalinishika na kufanya niwe mpole kama mkulima aliyepotea shamba.
Leyra alitambua udhaifu wangu kua nilikua mahututi na maradhi ya aibu, aliamua kunipa ushirikiano, kila nilipomsifia kuhusu uzuri wake yeye pia alinisifia, kila nilipokua nikimuangalia nae aliniangalia, nilipotabasamu nae alitabasamu, alishika na kuzichezea ndevu zangu huku akiitekenya pua yangu.
Jamani ndugu zangu naombeni msinicheke kiukweli nakubali kua nilikua fala wa mwisho kabisa duniani kwani licha ya ushirikiano wote huo alionipa Leyra bado nilishindwa kumtamkia Leyra neno nakupenda.
Kwa sababu na yeye pia alikua ananipenda Leyra aliamua kunivumilia aliamini hatua tuliyofikia ilikua ahueni kuliko hapo awali.
Leyra alizidi kuwakataa wanaume wanaojua kueleza hisia zao ambao kutwa nzima walikua wakimsumbua na kumfuata kama kumbikumbi, aliwakataa kwa sababu yangu bila shaka alitamani kuniambia kua ananipenda lakini aliogopa kunianza, aliogopa angeonekana malaya ndio maana akachagua kuvumilia mateso yote kwa sababu yangu mimi.
Jambo hili lilituumiza sote wawili, ukaribu wetu haukua na maana yoyote sababu tulikua tunapendana lakini tulishindwa kuelezana hisia zetu.
‘When a woman love she love for real’ maneno ya wimbo wa msanii maarufu R-Kelly yalithibitika hapa kwani licha madhaifu yangu yote bado Leyra aliendelea kunivumilia, muda wote alikua upande wangu kila tulipokua free darasani au weekend tulishinda wote, tulitoka out kutembea sehemu tofauti tofauti pamoja.
Mambo yote haya yalikua mwiba mkali kwenye moyo wa Lucyra msichana mrembo aliyetokea kunipenda sana pengine kuliko wanawake wote waliowahi kunipenda. Ukaribu wangu na Leyra ulimtesa sana kuliko kitu chochote, muonekano wake dhaifu kila nilipoonana nae uliyathibitisha maumivu yake wazi, nilimuhurumia sana lakini sikuzikubalia hisia zake.
Mpaka wakati huo mpango wa Daniel haukusaidia kitu chochote kwa upande wao sababu ulimuumiza sana Lucyra. Badala ya kupendwa kama alivyodhani hapo awali safari hii Daniel alichukiwa zaidi kwa sababu ya kunipanga kundi moja na Leyra na kufanya tuwe na ukaribu mkubwa ambao ulimuumiza sana Lucyra msichana aliyenipenda toka utoto wetu ambaye maskini ya Mungu alianza kukuonda sababu ya stress na mawazo.
Kila nilipomuona Lucyra nilikumbuka utoto wetu, wema na upendo mkubwa alionionyesha toka utotoni ulinihukumu, maradhi yake ya mapenzi yalinitoa machozi, kudhoofu kwake kulinighutusha sana nilitamani niwe nae hata kwa kumdanganya lakini kutoka seminarini nilifundishwa kutokua muongo hata kidogo. Kwanini niwe na mtu ambaye simpendi ili kumsaidia na kumfurahisha yeye, moyo wangu ulikataa kabisa kulikubali hili jambo.
Kila muomba mboga huombea chungu chake maneno haya ya wahenga yalinipa moyo kuendelea kushikilia msimamo wangu, sikujihesabia haki lakini naamini sikua na kosa lolote mateso yote aliyoyapata Lucyra ilikua ni juu yake mwenyewe.
Pengine labda nilikua na makosa bila kujua ndio maana Mungu aliamua kuniadhibu kwa kunipa maradhi ya aibu na kufanya nishindwe kumuambia Leyra hisia zangu kwani hadi muda huo sikua nimemuambia neno lolote kuhusu mahusiano licha ya jitihada zote alizokua amezifanya.
......... Itaendelea......
Nilimuhurumia sana Lucyra jinsi alivyokua akiteseka kwa sababu yangu. Kiukweli sikumfanyia makusudi, utotoni sikumkubalia kwa sababu ya masomo na malezi yangu ya kiseminari lakini safari hii sikumpenda kabisa kwa sababu ya Leyra. Sikuogopa ujirani wa familia zetu wala ukaribu wa wazazi wetu nilimueleza Lucyra kila kitu wazi lakini kutokana na kuzidiwa na nguvu ya mapenzi alishindwa kabisa kunielewa tena kumuogopa kwangu Leyra ndio kulimpa moyo na kufanya azidi kusubiri jibu la ndio kutoka kwangu, jambo ambalo kiukweli lilikua haliwezekani.
Ukisema cha nini wenzako wanasema watakipata lini.
Kama ilivyokua kwangu kumuogopa Leyra kulivyompa moyo Lucyra ndivyo kumkataa kwangu Lucyra kulivyompa moyo Daniel, Cr wa darasa letu ambaye alitokea kumpenda sana Lucyra. Daniel na Lucyra walifahamiana tokea sekondari, walisoma darasa moja kidato cha tano na cha sita katika shule ya Mt. Mathias iliyopo jijini Dar es salaam.
Tokea huko Daniel alikua akimtaka Lucyra, alimueleza jinsi anavyompenda lakini mimi nilikua kikwazo, Lucyra alimkataa kwa sababu yangu lakini cha ajabu Daniel hakuacha wala hakuchoka kumpenda.
Mwanzo nilikua mbali na Lucyra nchini Kenya masomoni lakini Daniel alinifahamu sababu Lucyra alimwambia habari zangu. Safari hii nilikua karibu nae chuo kimoja darasa moja, Daniel aliogopa sana alijua wazi kama ningemkubali Lucyra basi huo ndio ungekua mwisho wake. Mimi kumkataa Lucyra aliona haitoshi aliamini asipofanya kitu ipo siku ningeweza kubadilisha mawazo yangu.
Mimi kumpenda Leyra kwa Daniel zilikua ni habari njema lakini kitendo cha kumuogopa ilikua habari mbaya kwake.
Njia sahihi ya kufanya hio izidi kua habari njema kwake ilikua ni mimi na Leyra kua karibu. Daniel alidhamiria kufanya kitu lakini hakujua afanye kitu gani, jambo hilo lilimuumiza kichwa kwa muda wa wiki mbili mpak Dr. Grosse alipokuja Darasani na kutaka Cr atengeneze makundi mbali mbali kwa ajili ya asaimenti alizokua ameziandaa.
Daniel hakutaka kuzubaa aliona hio ndio ilikua fursa pekee ya kuitumia kutengeneza ukaribu wangu na Leyra. Daniel alicheza kama Ronaldo, alinipanga kundi moja na Leyra bila kuogopa naye alijipanga kundi moja na Lucyra.
Lilikua jambo muhimu sana kwetu sote ingawa mwanzo lilinitesa sana kwa sababu ya aibu, kujizuia kubehua na kukohoa mbele ya Leyra. Japo niliteseka mwanzoni lakini mpango wa Daniel ulizaa matunda, polepole kama mwendo wa kobe nilianza kumzoea Leyra na ukaribu wetu mkubwa ukaanzia hapo.
“Hi naitwa Leyra Lacena” Leyra aliniambia baada tu ya kukutana kwenye kundi tulilipongiwa.
“Naitwa Alfred Kamba” kwa mara ya kwanza niliongea nae kama haitoshi tukasalimiana kwa kushikana mikono.
Labda kwa sababu wote tulikua tunapendana, ndani ya muda mfupi ukaribu wangu na Leyra ulikua mkubwa sana, kama mwendo wa saa mbovu lile jina la domogundi lilianza kupotea taratibu.Leyra alikua na kitu fulani cha pekee ndani yake achana na uzuri, tabasamu na uchangamfu aliokua nao. Ndani yake ni kulikua na nguvu fulani ya kutenda miujiza sababu kila sekunde niliyoongea nae nilisikia furaha ya ajabu, tabasamu lake lilitosha kunisahaulisha matatizo yangu yote, nilijiona mwepesi mwili mzima kana kwamba nilikua nimesamehewa dhambi zangu zote.
Wakati Tanzania ikipata uhuru wake mwaka 1961 mimi uhuru wangu niliupata hapo, polepole hali ya kujiamini ilikuja, nilianza kumtania Leyra, nikaanza kumshika kiuno, kumkumbatia na kumuangalia kwa uhuru zaidi bila kuibia kama hapo awali.
“Leyra wewe ni mzuri sana” nilimwambia kila mara tulipokutana, ushuzi ulipata mjambani kama utani na mimi domo zege nikawa nimeula.
Kila nilichofanya na kumwambia Leyra alikua akitabasamu hata siku moja sikuwahi kumuona akiwa amekasirika.
Pamoja na mambo yote hayo kumwambia Leyra kua nampenda nilishindwa, nilitamani kumwambia Leyra kua nampenda sana na naomba awe mpenzi wangu lakini nilishindwa kabisa. Kila nilipotaka kumwambia maradhi yangu ya aibu yalinishika na kufanya niwe mpole kama mkulima aliyepotea shamba.
Leyra alitambua udhaifu wangu kua nilikua mahututi na maradhi ya aibu, aliamua kunipa ushirikiano, kila nilipomsifia kuhusu uzuri wake yeye pia alinisifia, kila nilipokua nikimuangalia nae aliniangalia, nilipotabasamu nae alitabasamu, alishika na kuzichezea ndevu zangu huku akiitekenya pua yangu.
Jamani ndugu zangu naombeni msinicheke kiukweli nakubali kua nilikua fala wa mwisho kabisa duniani kwani licha ya ushirikiano wote huo alionipa Leyra bado nilishindwa kumtamkia Leyra neno nakupenda.
Kwa sababu na yeye pia alikua ananipenda Leyra aliamua kunivumilia aliamini hatua tuliyofikia ilikua ahueni kuliko hapo awali.
Leyra alizidi kuwakataa wanaume wanaojua kueleza hisia zao ambao kutwa nzima walikua wakimsumbua na kumfuata kama kumbikumbi, aliwakataa kwa sababu yangu bila shaka alitamani kuniambia kua ananipenda lakini aliogopa kunianza, aliogopa angeonekana malaya ndio maana akachagua kuvumilia mateso yote kwa sababu yangu mimi.
Jambo hili lilituumiza sote wawili, ukaribu wetu haukua na maana yoyote sababu tulikua tunapendana lakini tulishindwa kuelezana hisia zetu.
‘When a woman love she love for real’ maneno ya wimbo wa msanii maarufu R-Kelly yalithibitika hapa kwani licha madhaifu yangu yote bado Leyra aliendelea kunivumilia, muda wote alikua upande wangu kila tulipokua free darasani au weekend tulishinda wote, tulitoka out kutembea sehemu tofauti tofauti pamoja.
Mambo yote haya yalikua mwiba mkali kwenye moyo wa Lucyra msichana mrembo aliyetokea kunipenda sana pengine kuliko wanawake wote waliowahi kunipenda. Ukaribu wangu na Leyra ulimtesa sana kuliko kitu chochote, muonekano wake dhaifu kila nilipoonana nae uliyathibitisha maumivu yake wazi, nilimuhurumia sana lakini sikuzikubalia hisia zake.
Mpaka wakati huo mpango wa Daniel haukusaidia kitu chochote kwa upande wao sababu ulimuumiza sana Lucyra. Badala ya kupendwa kama alivyodhani hapo awali safari hii Daniel alichukiwa zaidi kwa sababu ya kunipanga kundi moja na Leyra na kufanya tuwe na ukaribu mkubwa ambao ulimuumiza sana Lucyra msichana aliyenipenda toka utoto wetu ambaye maskini ya Mungu alianza kukuonda sababu ya stress na mawazo.
Kila nilipomuona Lucyra nilikumbuka utoto wetu, wema na upendo mkubwa alionionyesha toka utotoni ulinihukumu, maradhi yake ya mapenzi yalinitoa machozi, kudhoofu kwake kulinighutusha sana nilitamani niwe nae hata kwa kumdanganya lakini kutoka seminarini nilifundishwa kutokua muongo hata kidogo. Kwanini niwe na mtu ambaye simpendi ili kumsaidia na kumfurahisha yeye, moyo wangu ulikataa kabisa kulikubali hili jambo.
Kila muomba mboga huombea chungu chake maneno haya ya wahenga yalinipa moyo kuendelea kushikilia msimamo wangu, sikujihesabia haki lakini naamini sikua na kosa lolote mateso yote aliyoyapata Lucyra ilikua ni juu yake mwenyewe.
Pengine labda nilikua na makosa bila kujua ndio maana Mungu aliamua kuniadhibu kwa kunipa maradhi ya aibu na kufanya nishindwe kumuambia Leyra hisia zangu kwani hadi muda huo sikua nimemuambia neno lolote kuhusu mahusiano licha ya jitihada zote alizokua amezifanya.
......... Itaendelea......