Kodi ya Viwanja, je itapunguza bei za Mashamba?

MPadmire

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
3,928
3,225
Waziri Wa Ardhi Nyumba na Makazi, Mh. Lukuvi ametangaza kampeni ya Ulipaji kodi kwa kila mwenye shamba au kiwanja

Je..Kama wewe umenunua kiwanja na unadunduliza pesa ili ujenge..huoni bei ya Kiwanja itakuja kuwa mara 2?

Je Wale wenye viwanja kama 2 mpaka 8...utalipia kodi viwanja vyote au utaamua kuuza upunguze mzigo wa kodi?

Je hii kodi ya viwanja..itaaffect bei za viwanja?

Kwa nini Serikali isichukue kodi ya miaka 5 kwa mashamba yake na kukabidhi watu wanaotaka kwa makazi au Kilimo (Hii itaondoa ulanguzi wa viwanja) Example Kigamboni...Burka, ....Arumeru/NSSF, Mbeya Forest, Njiro Kiserian
 
Kulipa kodi ni uzalendo.

Ila Lukuvi akivuna kodi kwa wananchi halafu baadae aje kuwaambia hawakustahili kumiliki atakuwa si muungwana!
 
Kulipa Kodi ni Uzalendo, kuleta maendeleo na kutoa huduma za jamii

Kuajiri Madokta wa kutosha, kulipa waalimu vizuri

Hii ya Kutoza Ardhi kodi ni nzuri sanaaa

naipongeza hii
 
Nampongeza kwa hilo. Kuna mijitu inamiliki maeka mengi itauza kwa hasara maana wengine hawana ardhi kabisa.
Mh. Ingia mpaka vijijini watu wapate ardhi.
Uko mbali tu ningekupa mkono wa heko.
 
Mtu unamiliki mpaka viwanja 8.? Why???? We call that greedy!

Ndio, kabisa Mtu ana Viwanja kama 8 au zaidi ya kumi kwa lengo la kuja kuuza bei juu
Walipia kodi sasa...Fisi hawa na Tamaa zao

Kuna wengine wamehodi mashamba makubwa na hawalipi kodi..

Komesha hao

Pongezi Lukuvi..

Naomba lifanyike kwa nia njema tu kusaidia wananchi....

Walipe Kodiiiiii
 
Tafute pesa, idadi ya viwanja inahusu nini unadhani vinapatikana bure, people worked on it. Hata hivyo direct tax kwenye kila kitu ni kuua uchumi go back read, then comment. They killing our economy tunashagilia, uchumi unadumaa. We consume that we don't produce and we produce what don't consume.
 
Tafute pesa, idadi ya viwanja inahusu nini unadhani vinapatikana bure, people worked on it. Hata hivyo direct tax kwenye kila kitu ni kuua uchumi go back read, then comment. They killing our economy tunashagilia, uchumi unadumaa. We consume that we don't produce and we produce what don't consume.

Wacha maneno........wengi viwanja wanavipata kwa figisu. Especially maafisa ardhi. Baada ya kuvigawa Kama wanavyoelekezwa na sheria....wanajiuzia wenyewe kwa bei ndogo then wanakuja kuviuza kwa bei za magendo. Hii michezo inafahamika. Iam sure hata wewe unajua. Wengine wana nunua viwanja Kama njia ya kutakatisha pesa chafu!

Hivi kweli unakuwa na viwanja 10 au 20.......vya nini? That's greedy. Kama no farm hata Kama ni ekari 1000 as long as unazitumia na unalipa kodi....then it's fine. But hizi plots za ujanja ujanja......no way
 
Back
Top Bottom