Kodi ya vibanda vya stendi ya Buzuruga

Kodi ya vibanda vya stendi ya Buzuruga

koryo

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2010
Posts
639
Reaction score
278
Jana katika hali ya kushangaza watumishi wa Halmashauri wa Ilemela wakiongozwa na Mkurugenzi wao Ndugu Wanga waliwafungia wafanyabiashara wa Vibanda vya Stendi ya Buzuruga kisa kwa kutolipa Tshs.200,000 kwa mwezi.

Kwa mtu mwenye akili timamu kodi ya Tshs.200,000 kwa mwezi haiwezekani hata kidogo. Pale Stendi ya Buzuruga wengi wa wafanyabiashara wanaganga tuu njaa hawana mapato ya kulipa Tshs.200,000 kwa mwezi. Waliwaomba walipe Tshs.40,000 kwa mwezi Halmashauri ikagoma. Wafanyabiashara wanalipa kodi nyingi sana kama Leseni Tshs.150,000 kwa mwaka, Tshs.400,000 kodi ya mapato kwa mwaka, usafi,mabango etc.

Halmashauri isilete chuki baina yake na wananchi na hii itapelekea Serikali ya CCM kuchukiwa na wananchi na kuja kukosa kura 2020. Nashauri walipe angalau Tshs.40,000 kwa mwezi. Mhe. Mbunge hao ni wapiga kura wako nakushauri ufuatilie hili jambo usije ukakosa kura bado tunakuhitaji.
 
Mkuu jana milango mitatu ya mzee imepigwa kufuli hapo buzuruga
 
Jana katika hali ya kushangaza watumishi wa Halmashauri wa Ilemela wakiongozwa na Mkurugenzi wao Ndugu Wanga waliwafungia wafanyabiashara wa Vibanda vya Stendi ya Buzuruga kisa kwa kutolipa Tshs.200,000 kwa mwezi. Kwa mtu mwenye akili timamu kodi ya Tshs.200,000 kwa mwezi haiwezekani hata kidogo. Pale Stendi ya Buzuruga wengi wa wafanyabiashara wanaganga tuu njaa hawana mapato ya kulipa Tshs.200,000 kwa mwezi. Waliwaomba walipe Tshs.40,000 kwa mwezi Halmashauri ikagoma. Wafanyabiashara wanalipa kodi nyingi sana kama Leseni Tshs.150,000 kwa mwaka, Tshs.400,000 kodi ya mapato kwa mwaka, usafi,mabango etc. Halmashauri isilete chuki baina yake na wananchi na hii itapelekea Serikali ya CCM kuchukiwa na wananchi na kuja kukosa kura 2020. Nashauri walipe angalau Tshs.40,000 kwa mwezi. Mhe. Mbunge hao ni wapiga kura wako nakushauri ufuatilie hili jambo usije ukakosa kura bado tunakuhitaji.
Toka lini ccm wakawa watetezi wa wafanyabiashara ndogo ndogo? mbona manspaa za dar-es-salaam tunalipa kwa mwezi sh. 15,000/ kwa mwaka 180,000 sasa hiyo 200,000 kwa mwezi c hatari jamani ..daah alafu mtu bado unaishabikia chichiem?
 
Jana katika hali ya kushangaza watumishi wa Halmashauri wa Ilemela wakiongozwa na Mkurugenzi wao Ndugu Wanga waliwafungia wafanyabiashara wa Vibanda vya Stendi ya Buzuruga kisa kwa kutolipa Tshs.200,000 kwa mwezi. Kwa mtu mwenye akili timamu kodi ya Tshs.200,000 kwa mwezi haiwezekani hata kidogo. Pale Stendi ya Buzuruga wengi wa wafanyabiashara wanaganga tuu njaa hawana mapato ya kulipa Tshs.200,000 kwa mwezi. Waliwaomba walipe Tshs.40,000 kwa mwezi Halmashauri ikagoma. Wafanyabiashara wanalipa kodi nyingi sana kama Leseni Tshs.150,000 kwa mwaka, Tshs.400,000 kodi ya mapato kwa mwaka, usafi,mabango etc. Halmashauri isilete chuki baina yake na wananchi na hii itapelekea Serikali ya CCM kuchukiwa na wananchi na kuja kukosa kura 2020. Nashauri walipe angalau Tshs.40,000 kwa mwezi. Mhe. Mbunge hao ni wapiga kura wako nakushauri ufuatilie hili jambo usije ukakosa kura bado tunakuhitaji.



Kwa akili zako unaona walipe kodi ya 40000/= eneo kama hilo,wewe kweli.......... Kisesa kwenyewe kodini zaidi ya 50000/= kwa mwezi,kama wameshindwa kulipa wahamishie biashara zao Kishiri
 
Shs 200.000/= ni kwa miezi mitatu siyo mwezi mmoja, hamna mfanyibiashara wa vyumba kuzunguka stand anayeweza kulipa 200.000 kwa mwezi Tanzania nzima.
 
mkuu koryo,pengine mimi nilielewa vibaya.mkurugenzi wa ilemela anasema halmashauri iliwapangisha wafanyabiashara kwa kodi ya sh elfu 20 kwa mwezi.wafanyabiashara hao wakawapangisha watu wengine na kuwatoza kodi ya mpaka shilingi laki 3 kwa mwezi huku wakilipa elfu 20 pekee kwa halmashauri na zinazobaki wanaweka mifukoni mwao.baada ya kushtuka halmashauri imewapa notisi ya saa 48 waondoe bidhaa zao ili ipangishe kwa watu wengine na kodi imepanda toka elfu 20 hadi laki 2 kwa mwezi.niko tayari kusahihishwa wadau.
 
Pale hamna biashara hapajachangamka kama ile stand ya zamani ya Tanganyika bus.

Hata ile stand ya nyegezi bado maduka yanapigwa doro
 
Kazi tu,Kua mzalendo Lipa kodi kwa manufaa ya nchi yako.
 
Tatizo ni watu kuwa na habari.zisizowahusu na kukosa habari zinazowahusu(R.C DSM 2016)
 
Back
Top Bottom