Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
YAH: SALAAM ZA POLE.
Kwa niaba yangu binafsi, na kwa niaba ya Dayosisi ninayoiongoza kwa neema, pokea salaam za pole kama Baraza, Kanisa na binafsi kwa Fr. Charles Kitima kwa tukio ovu lililofanyika na kumdhuru mtumishi wa Baraza.
Shambulio hilo si la Fr. Kitima, si la TEC, wala la Imani ya Kikristo TU.
Ni shambulio kwa wapenda HAKI na AMANI wote. Zaidi ni shambulio kwa Mama Tanzania, kilichokuwa kitovu cha amani yetu.
Soma Pia: Padri Kitima ashambuliwa na watu wasiojulikana. Inadaiwa hali yake ni mbaya
Tunasimama nanyi kumuombea apone. Tunasimama nanyi kuwaombea waliomjeruhi wabadilishwe bila kutaka, kuwa watu wema.
Tunaioombea Serikali yetu, isitishwe na ubaya bali iseme,
HAITATOKEA TENA.
Tumsifu Yesu Kristo.
Bwana Yesu Asifiwe.