Kiwanda chafungwa kwa kusindika nyama ya Punda

kibogo

JF-Expert Member
Apr 1, 2012
9,739
4,732
Punda.jpg


Baraza la taifa la usimamizi wa mazingira {NEMC} limekifungia kiwanda cha Huwa Cheng Company Limited kilichopo mjini Dodoma na kukitoza faini ya shilingi milioni 200 baada ya kubaini kiwanda hicho kinajihusisha na usindikaji wa nyama ya Punda kinyume na utamaduni wa watanzania huku mazingira yake yakiwa hatarishi kutokana na uchafu unaozalishwa kuzagaa kwenye makazi ya watu.

Ni mabishano makali baina ya wamiliki wa kiwanda hiki raia wa uchina na maofisa wa NEMC yaliyochukua muda mrefu kabla ya maofisa hao kutoa tamko la kufungwa kwa kiwanda hicho ambacho mbali na kuzalisha nyama ya Punda ambayo ni kinyume na utamaduni wa watanzania lakini pia mazingira ya uzalishaji wake ni hatarishi kwa afya za wafanyakazi na majirani wa eneo hilo.

Kiwanda hiki ambacho kwa siku kinadaiwa kuchinja Punda wasiopungua 200 inaelezwa kuwa mbali na kukiuka utamaduni lakini pia kinaharibu kizazi cha wanyama hao ambao uzao wake unatajwa kuwa ni mdogo hali inayotishia wanyama hao ambao kwa kanda ya kati hutumiwa katika kazi mbalimbali kupungua ama kutoweka kabisa.

Mohamed Hamis ni meneja msaidizi wa kiwanda hiki ambaye anazungumza kwa niaba ya raia hao wa uchina anasema nyama hizo za Punda zinasafirishwa kwenda kuuzwa nchini China.

Wakazi wa mji wa Dodoma ambao wanatupa lawama kwa mamlaka za mkoa kutobaini kiwanda hicho na kukichukulia hatua huku kukiwa na taarifa ya nyama hizo kuzagaa na kuuzwa katika maeneo mbalimbali ya mji huo hasa kwenye mabaa na migahawa ya chakula.


Chanzo: ITV


1. Wauaji wa Tembo = Wachina
2. Wasafirishaji wa Pembe za Ndovu = Wachina
3. Wawekezaji wa Gesi nchini = Wachina
4. Madawa ya kulevya mengi kutoka Tanzania yanayosafirishwa na wasanii na washabiki wa CCM yanakamatiwa China

Ebu tutafakari kwa kina hawa wachina wanadhamira ya dhati kwa nchi hii? leo hii wanachinja Punda na kujifanya wanasafirisha nje ya nchi.


Kuna post mbili tayari kuhusiana na hiki kiwanda , lakini nimekuja na post hii makusudi kwakuwa ina mengi ambayo hayakusemwa.

Binafsi nilifika pale kiwandani na kukaa karibia wiki tatu hivi, kiwanda kiko eneo la four ways Ikungi njia ya kwenda Singida nyuma ya magodown ya Bhanji, ni eneo la viwanda tupu.

Hiki kiwanda kina eneo kubwa sana, na ni uwekezaji usiopungua USD 1,000,000/= Kiwanda kinajishughulisha na kuchinja punda na pia ukusanyaji wa ngozi za ng'ombe, kuziprocess mpaka hatua ya mwisho na kuzisafirisha kwenda China.

Hapo kiwandani pana facilities zote za kufanyia hiyo shughuli ya ngozi, (nitaweka picha) na pia baadhi ya facilities kwa ajili ya uchinjaji punda kama cold room kubwa sana, containers za friji machinjio nk
Hiki kiwanda kilikamilika mwaka jana na kuanza shughuli zake za ngozi na uchinjaji, lakini sina uhakika kama leseni yake ni kwa ajili ya biashara gani.

Baada ya kuchinja punda wanaofikia container 3 za 40ft, walistukiwa na mamlaka husika kuwa hawana kibali cha kuchinja na kusafirisha nyama ya punda, kwahiyo pale kulikuwa na rumbesa wa nyama za punda za tangu October mwaka jana, zikiwa cold room( nimezila sana karibia siku zote 21 nilipokea pale)
Wachina wakaanza kusaka kibali kwa nguvu zote huku biashara ya ngozi ambayo haikuwa na tatizo ikiendelea.

Katika kuhangaika kwao wakakutana na bwana mmoja aliyekuwa karibu na Waziri husika. Huyu waziri bila kutafakari na kufanya fitina (kibongobongo), akalazimisha mpaka kibali kikapatikana kwa njia za mkato/panya (hapa shekeli ilitumika sana).

Huyu Waziri alivyokuwa juha au mpuuzi (naomba radhi kwa kutumia maneno haya) kwenye bunge la bajeti la mwaka huu alisimama bungeni na kukifagilia sana hiki kiwanda. Kumbukumbu za video zipo na kwenye Hansard rasmi za bunge pia pamoja na taarifa za habari.

Aliihusisha serikali moja kwa moja na kiwanda hiki na kuita ni uwekezaji uliotukuka(siku hiyo nilishangaa mpaka watu wakanishangaa.

Hiki kiwanda pamoja na uwekezaji mkubwa ni kiwanda cha ujanjaujanja kinachofanya mambo yake mengi bila kufuata kanuni na tararibu za uwekezaji nchini, kuna mapungufu mengi sana pale, kuanzia kwa wafanyakazi management mpaka utendaji kazi.

Najiuliza hivi Waziri mzima anayaiwakilisha serikali aliweza vipi kusimamia mpaka kibali kikapatikana bila kwanza kujiridhisha na huo uwekezaji?

Hakika hii ni kasha kubwa kwa chama na serikali na Taifa pia.
 
kwa hawa wachina watawalisha watanzania hadi nyoka, paka, panya, mbwa na kadhalika. hawa niwakuwa nao makini.
 
sasa tujiulize izo nyama zinapitia wapi kwenda china kama airport miaka yote hiyo kwa nini hawakugundua na kama bandarini nako hawakujua nini kinasafirishwa kinatoka wapi kama hao wote hawakujua ina mana tra hawajapata chochote na je kiwanda kinajengwa wachina wanafanya kazi punda wanaletwa na watanzania na kuna watanzania wameajiriwa hapo majirani wanaishi kuzunguka kiwanda wote hao hawajui kilichokua kinaendelea TANZANIA HOYEEE
 
Hivi jamani serikali ya CCM iko wapi,inashindwa kusimamia hata hili na tuna wizara ya chakula kabisa,yaani imefikia mahali kweli watanzania tunalishwa nyama ya Punda,tena na wageni? Hakuna shida october sio mbali.
 
Kwa wale waliofuatilia habari ya ITV leo wameona jinsi kiwanda cha Wachina kinavyochinja punda karibia 40 kila siku, kusindika na kuexport nyama hiyo kwenda China bila kibali chochote kimsingi wamepewa kibali cha kufanya kazi nyingine lakini wao wamegeukia kumaliza punda wetu.

Halafu cha kukera zaidi ni mchina anahojiwa na maafisa wa serikali halafu anajifanya kuwatunishia misuli mpaka askari. ama kweli serikali ya CCM imeoza na kusababisha nchi yetu kuwa shamba la bibi.

Tumeona juzi jinsi wachina walivyosafirisha pembe za ndovu kutoka hapa, na sio hao tu wako wengi Dar na huko mikoani wanaosababisha ujangiri ushamiri kwa kuendekeza hii biashara ya pembe za ndovu.

Hivi watanzania tutakaa kimya mpaka lini wakati nchi yetu inasafishwa na kila mtu? yaani ni kama hakuna kiongozi au mwananchi mwenye uchungu na mali zetu .
 
Nimeona hiyo ishu ni aibu sana kama wachina wanachinja punda na watz wanauziwa japo sio utamaduni wetu na inchi inajinasibu kuwa na idara ya TISS, hawa TISS kazi yao nini? Aibu sana
 
Wamehamia, kwenye fuso zetu tea aaah kwani punda wananunua sh ngapi mi ninao arobain na siku hiz majan /malisho hakuna nataka nipunguze aisee
 
kuna mambo ya kufuatilia, hao wachina wana kibali cha kuanzisha kiwanda cha vyakula? hiyo inasairishwa kwa njia gani mamlaka zinajua? tuanze na serikali ya mtaa, kata, wilaya na mkoa zilkua wapi? tuje bandari na airport wanajua nini? tuende mitaani hao wanaouza punda na wanaonunua nyamam ya punda na kutulisha, tukifuatilia kote huko tutaweka misingi ya kuzuia hay yasijirudia, lakini tukiishia kufunga na kutoza faini, kesho tutasikia lingine.
 
Mikataba 17 ya kichina iliyosainiwa ndo utekelezaji wake huo,wachina africa magharibi wanafukuzwa,sisi tunawakumbatia.
 
Kwa wale waliofuatilia habari ya ITV leo wameona jinsi kiwanda cha Wachina kinavyochinja punda karibia 40 kila siku, kusindika na kuexport nyama hiyo kwenda China bila kibali chochote kimsingi wamepewa kibali cha kufanya kazi nyingine lakini wao wamegeukia kumaliza punda wetu.

Halafu cha kukera zaidi ni mchina anahojiwa na maafisa wa serikali halafu anajifanya kuwatunishia misuli mpaka askari. ama kweli serikali ya CCM imeoza na kusababisha nchi yetu kuwa shamba la bibi.

Tumeona juzi jinsi wachina walivyosafirisha pembe za ndovu kutoka hapa, na sio hao tu wako wengi Dar na huko mikoani wanaosababisha ujangiri ushamiri kwa kuendekeza hii biashara ya pembe za ndovu.

Hivi watanzania tutakaa kimya mpaka lini wakati nchi yetu inasafishwa na kila mtu? yaani ni kama hakuna kiongozi au mwananchi mwenye uchungu na mali zetu .

Kwani Punda nazo ni Nyara?
 
punda wakipelekwa machinjioni Dodoma wanapigwa na umeme kabla ya kuchinjwa
 

Attachments

  • punda.doc
    5.8 MB · Views: 845
tatizo sio wachina ,hivi wametoka china na kuanza kuchinja na kusafilisha nje ya nchi ,hivi walinzi wa nchi hii wapo wapi,hivi vibali wamepata wapi ,ukiangalia kiwanda kipo katikati ya nchi ,

CCM ondokeni madarakani kabla hamujahondolewa ,mliuza ,tembo,mkahuza twiga,mkahusa makenge kwa mkuwaiti sasa minahuza vilongwe ,CCM mwisho mtauza watu.
 
Back
Top Bottom