Kituo kikuu cha mabasi ya mikoani ubungo.

Kituo kikuu cha mabasi ya mikoani ubungo.

Magita

JF-Expert Member
Joined
Aug 23, 2013
Posts
319
Reaction score
144
Nasikitika sana watanzania tumelogwa hata tunashindwa kuchukua hatua, kituo hiki tunashikwa 200/= lakini ndani hakuna vyoo wala sehemu ya kusubiria mvua au jua mfano leo asbh mvua yote ile ilimalizika ktk miili ya abiria, kumbe kama plan zilikuwa dhaifu kwanini mliwahi kubomoa? Na kwanini tuendelee kushikwa 200/= wakati hakuna huduma yeyote ya kijamii?
 
Wamesema wazi kwa wasindikizaji abiria kama vipi ishia nje ya geti sio lazima uingie ndani
 
Vyoo vipo ndani kama hujui uliza.
Huduma ya bure hata kwa mkeo upati labda kwa mama yako tu.
 
Sasa wewe unalipa 200 ili uingie ndani kufanya nini?wakati tiketi unakatia nje
 
wamesema wazi kwa wasindikizaji abiria kama vipi ishia nje ya geti sio lazima uingie ndani

kama anamizigo na anawatoto na hela ya kumpa mbebaji haipo unafanyaje? Halafu utamaduni wetu wa kitanzania wa kumsindikiza mgeni nikuhakikisha mgeni kapanda bus na limeondoka,,je ukiishia nje halafu gari likaahirisha safari na wewe umeishia nje na kurudi usalama wa mgeni wako ukoje na ukizingatia siyo mwenyeji na anamizigo mingi na anawatoto? Try to think big.
 
Mimi huwa silipi zile 200/= 200/= pale, hata sijui za nini. Nikienda kumsindikiza abiria naenda na ticket niliyosafiria zamani mkoani so naingia nayo na kutoka nayo for free, na kwa bahati nzuri wale mburula wa mlangoni hawasomi
 
Mimi huwa silipi zile 200/= 200/= pale, hata sijui za nini. Nikienda kumsindikiza abiria naenda na ticket niliyosafiria zamani mkoani so naingia nayo na kutoka nayo for free, na kwa bahati nzuri wale mburula wa mlangoni hawasomi

Duh... yaani nchi hii kila mtu anaona namna rahisi ya kutatua matatizo ni kuwa mwizi! Huyo anaenda na ticket ya zamani ni wiziii. Iko siku utakuta mtu makini aithet utapigwa au uishie kupata aibu!
Point ya msingi hapa ni kuwa "je ni halali kulipia wakati hakuna huduma ndani?"
Serikali = ccm =janga
 
Vyoo vipo ndani kama hujui uliza.
Huduma ya bure hata kwa mkeo upati labda kwa mama yako tu.

wewe, ubungo ni stand pekee duniani inayowaibia wasafiri, tiketi ya basi unakatia ndani mlangoni unalipishwa sh 200 kwa huduma gani inapatikana mule ndani? mvua ikinyesha tope na maji kila mahali, ukienda chooni unalipishwa sh 300 nyingine, au hii ndio miaka 50 ya uhuru na maisha bora ya mtanzania?
 
Kituo kilikusudiwa kuhamishwa kwa muda mrefu lakini hadi leo sijaona juhudi za kukihamisha.
 
Mtalaumu CCM hadi siku zenu za kuishi zinaisha mabadiliko yanaanza na wewe

Labda shoka tuliite shoka na koleo liitwe koleo. Serikali iliyopo madarakani ikifanya vizuri sifa ziende kwa ccm, hali kadhalika ikiboronga basi lawama ccm wazikubali. Tuambiwe kama ni kweli kituo cha mabasi ya kwenda mikoani kilitakiwa kijengwe mbezi ya kimara na kama kuendelea kuwepo pale pa zamani kunatokana na serikali kuogopa kuhojiwa sababu ya kujenga infrastructure ya daraja lililopo kwa kukosa coordination nzuri kwa wizara husika.
 
kama anamizigo na anawatoto na hela ya kumpa mbebaji haipo unafanyaje? Halafu utamaduni wetu wa kitanzania wa kumsindikiza mgeni nikuhakikisha mgeni kapanda bus na limeondoka,,je ukiishia nje halafu gari likaahirisha safari na wewe umeishia nje na kurudi usalama wa mgeni wako ukoje na ukizingatia siyo mwenyeji na anamizigo mingi na anawatoto? Try to think big.

Unaahirisha safari. Wewe utasafiri vipi kama huna pesa?
 
Back
Top Bottom