Rajabu Msechu
Member
- Apr 13, 2016
- 35
- 18
Habari za asubuhi great thinkers wenzangu, natumaini kwa uwezo alitupatia mwenyezi Mungu hatujambo.
Nimeona ni jambo la mbolea kuleta uzi huu kwenye jukwaa hili hasa baada ya uchunguzi yakinifu nilioufanya kwenye kituo cha mabasi Makumbusho.
Wazungu wanakwambia, "No Research, No Right To Speak".
Ningependa kwenda kwenye kiini moja kwa moja, wakati kituo cha mabasi Mwenge kilipoamishwa kupisha upanuzi wa barabara na hatimaye kuhamishiwa Makumbusho, niliamini kwamba maboresho ya kituo kipya yangekuwa bora zaidi.
Hapo awali wakati kituo hiki cha Makumbusho kinaanza, uliwekwa utaratibu mzuri sana kama vile usafi, ulinzi, halikadhalika wapiga debe walipigwa marufuku. Lakini kadri muda ulipokuwa ukizidi kwenda ndipo mambo yakaanza kubadilika taratibu.
Nikianza na kero ya kwanza ya uwepo wa wapiga debe mateja, hawa watu kama wanavyojulikana kwenye jamii huwa hawana dhamana.
Hawa ndio chanzo cha uhalifu pale kituoni hasa kwa wasafiri kuibiwa mali zao kama vile, simu, mikoba na fedha.
Kama hiyo haitoshi hawa wapiga debe huwaleta wenzao ambao wao kazi yao ni kuchora ramani za kuwaibia watu ndani ya stand.
Ndio maana sasa hivi hali ya kiusalama kwa ujumla pale ndani sio ya kuridhisha ukilinganisha na hapo awali.
Kero nyingine ni ujenzi wa miundominu ya stand, tukianzia kwenye zile paving blocks walizoweka na barabara za vumbi za kuingia kituoni, ambapo ikinyesha mvua hugeuka kuwa dhahama pale hasa kwa matope kujaa.
Mwisho kabisa ningependa kutoa rai kwa wasafiri wanaotumia kituo cha Makumbusho kuwa makini sambamba na wahusika waliopewa jukumu kuhakikisha wanarekebisha dosari hizi.
Nimeona ni jambo la mbolea kuleta uzi huu kwenye jukwaa hili hasa baada ya uchunguzi yakinifu nilioufanya kwenye kituo cha mabasi Makumbusho.
Wazungu wanakwambia, "No Research, No Right To Speak".
Ningependa kwenda kwenye kiini moja kwa moja, wakati kituo cha mabasi Mwenge kilipoamishwa kupisha upanuzi wa barabara na hatimaye kuhamishiwa Makumbusho, niliamini kwamba maboresho ya kituo kipya yangekuwa bora zaidi.
Hapo awali wakati kituo hiki cha Makumbusho kinaanza, uliwekwa utaratibu mzuri sana kama vile usafi, ulinzi, halikadhalika wapiga debe walipigwa marufuku. Lakini kadri muda ulipokuwa ukizidi kwenda ndipo mambo yakaanza kubadilika taratibu.
Nikianza na kero ya kwanza ya uwepo wa wapiga debe mateja, hawa watu kama wanavyojulikana kwenye jamii huwa hawana dhamana.
Hawa ndio chanzo cha uhalifu pale kituoni hasa kwa wasafiri kuibiwa mali zao kama vile, simu, mikoba na fedha.
Kama hiyo haitoshi hawa wapiga debe huwaleta wenzao ambao wao kazi yao ni kuchora ramani za kuwaibia watu ndani ya stand.
Ndio maana sasa hivi hali ya kiusalama kwa ujumla pale ndani sio ya kuridhisha ukilinganisha na hapo awali.
Kero nyingine ni ujenzi wa miundominu ya stand, tukianzia kwenye zile paving blocks walizoweka na barabara za vumbi za kuingia kituoni, ambapo ikinyesha mvua hugeuka kuwa dhahama pale hasa kwa matope kujaa.
Mwisho kabisa ningependa kutoa rai kwa wasafiri wanaotumia kituo cha Makumbusho kuwa makini sambamba na wahusika waliopewa jukumu kuhakikisha wanarekebisha dosari hizi.