Kitengule Hospital wamemhudumia mgonjwa, kisha wakakataa kumuandikia dawa kisa hana pesa

Kingsmann

JF-Expert Member
Oct 4, 2018
4,448
16,313
Malalamiko kwa Wizara ya Afya kwenda Hospitali ya Kitengule iliyoko Tegeta jijini Dar es Salaam.

Leo ndugu yangu alizidiwa ghafla, ikabidi wakimbize Kitengule kwani wanaishi karibu na hapo.

Alikuwa na tatizo la mguu kupata ganzi, na kupata maumivu ya mgonjo, tatizo ambalo limekuwepo kwa muda sasa. Hivyo leo maumizi yalizidi ndipo wakaamua wamuwahishe hapo Kitengule.

Baada ya vipimo ikiwemo xray, ameonekana ana tatizo kwenye misuli ya mgongo, ndiyo inayompelekea mpaka anapata ganzi za mguu.

Hivyo walianza na kumpa "Physiotherapy" kwanza ndipo wakafuatia suala la kumpa dawa.

Kimbembe kimekuja hapa kwenye dawa, daktari alowahudumia akawaambia dawa zinacost elfu 30 (30,000/=). Ndugu kwa wakati huo wakawa wameishiwa pesa, wakamuomba daktari japo awaandikie hiyo dawa kisha watanunua baadaye wakishajipigapiga angalau wanunue hata za kuanzia.

Cha kushangaza daktari amegoma katakata kuwandikia dawa kama hawana hiyi elfu 30. Na akaondoka kabisa ofisini kwake maana ilishakuwa jioni..

Hili jambo ni jipya kwa utaratibu wa matibabu ulivyo. Mgonjwa akishalipia gharama ya matibabu ina maana ni pamoja na kuandikiwa dawa la tatizo lake lililogundulika baada ya vipimo.

Wajibu wa daktari ni kumuandikia dawa mgonjwa, suala la atanunulia wapi halimuhusu, kama ipo hapo hospitali husika basi ni jambo jema, kama haipo basi ni haki ya mgonjwa kuandikiwa "Prescription" ili akanunue mahali inapopatikana.

Ni kosa kisheria na kimaadili kwa daktari kukataa kumuandikia mgonjwa dawa kwa sababu yoyote ile. Huyu mgonjwa akipatwa na lolote huko aliko huyo daktari na Hospitali kwa ujumla watakuwa wamehusika 100% kufa kwake.

Bado sijapata jina la huyo daktari, lakini nikilipata nitaliweka wazi hapa ili wahusike wasaidie kukomesha hawa wahuni walioingilia fani nyeti kama hii inayohusika na uhai wa wanadamu wenzetu.

Wizara ya Afya Tanzania

Wizara Maendeleo ya Jamii

IMG_20231004_181414.jpg


IMG_20231004_181521.jpg
 
Hili Nahisi litaonekana, sikuhizi JF imekua ikisaidia sana uovu, mara nyingi malalamishi naoa yakifika juu.
 
Poleni sana. lakini wakati mwingine tuwe wakweli, hizo dawa haziokotwi, zinauzwa, hivi ungekuwa wewe ungefanyaje? na ukimhudumia mtu akasema hana hela na umempa dawa boss wako anakuja kukudai hiyo hela ya dawa utakuwa mgeni wa nani?
Shida sio kumpa dawa, yani hata kuwaandikia dawa inayatakiwa kutibu tatizo lake wamegoma mpaka wahakikishe ana hiyo elfu 30 ndipo wamuandikie...

Yani target yao ni wauze dawa, ambalo ni jambo lisilomhusu mgonjwa.

Mgonjwa kalipia kila kitu ikiwemo kumuona daktari na vipimo, majibu yameonesha tatizo lilipo, kwa nini usimuandikie dawa akamunue mbele ya safari kama hana pesa kwa muda huo?
 
Malalamiko kwa Wizara ya Afya kwenda Hospitali ya Kitengule iliyoko Tegeta jijini Dar es Salaam.

Leo ndugu yangu alizidiwa ghafla, ikabidi wakimbize Kitengule kwani wanaishi karibu na hapo.

Alikuwa na tatizo la mguu kupata ganzi, na kupata maumivu ya mgonjo, tatizo ambalo limekuwepo kwa muda sasa. Hivyo leo maumizi yalizidi ndipo wakaamua wamuwahishe hapo Kitengule.

Baada ya vipimo ikiwemo xray, ameonekana ana tatizo kwenye misuli ya mgongo, ndiyo inayompelekea mpaka anapata ganzi za mguu.

Hivyo walianza na kumpa "Physiotherapy" kwanza ndipo wakafuatia suala la kumpa dawa.

Kimbembe kimekuja hapa kwenye dawa, daktari alowahudumia akawaambia dawa zinacost elfu 30 (30,000/=). Ndugu kwa wakati huo wakawa wameishiwa pesa, wakamuomba daktari japo awaandikie hiyo dawa kisha watanunua baadaye wakishajipigapiga angalau wanunue hata za kuanzia.

Cha kushangaza daktari amegoma katakata kuwandikia dawa kama hawana hiyi elfu 30. Na akaondoka kabisa ofisini kwake maana ilishakuwa jioni..

Hili jambo ni jipya kwa utaratibu wa matibabu ulivyo. Mgonjwa akishalipia gharama ya matibabu ina maana ni pamoja na kuandikiwa dawa la tatizo lake lililogundulika baada ya vipimo.

Wajibu wa daktari ni kumuandikia dawa mgonjwa, suala la atanunulia wapi halimuhusu, kama ipo hapo hospitali husika basi ni jambo jema, kama haipo basi ni haki ya mgonjwa kuandikiwa "Prescription" ili akanunue mahali inapopatikana.

Ni kosa kisheria na kimaadili kwa daktari kukataa kumuandikia mgonjwa dawa kwa sababu yoyote ile. Huyu mgonjwa akipatwa na lolote huko aliko huyo daktari na Hospitali kwa ujumla watakuwa wamehusika 100% kufa kwake.

Bado sijapata jina la huyo daktari, lakini nikilipata nitaliweka wazi hapa ili wahusike wasaidie kukomesha hawa wahuni walioingilia fani nyeti kama hii inayohusika na uhai wa wanadamu wenzetu.

Wizara ya Afya Tanzania

Wizara Maendeleo ya Jamii

View attachment 2771797

View attachment 2771798
Mtindo huu unafanywa na hospitali nyingi za binafsi, watakupima na kukupa jibu ila usiponunua dawa yao hawakuandikii dawa ya kununua kwingine.
 
Poleni sana. lakini wakati mwingine tuwe wakweli, hizo dawa haziokotwi, zinauzwa, hivi ungekuwa wewe ungefanyaje? na ukimhudumia mtu akasema hana hela na umempa dawa boss wako anakuja kukudai hiyo hela ya dawa utakuwa mgeni wa nani?
Mkuu au mimi sijaelewa? Sidhani kama alitaka apewe bure,
Naahisi alitaka apewe jina la dawa ili akanunue mwenyewe anapoamini pana unafuu labda..

Hapo hoja ya Dr. Ilikua ni kwamba siruhusu mtoke bila kuona dawa, yaani katika picha ya kua na uhakika mgonjwa amepata dawa, akiamini ya kua mnaweza msinunue, hivyo kanunueni mnakonunua mje mnioneshe au mnunue hapa, angeeleweka kua ana nia nzuri.

Kibongo bongo hii inaweza kua na hoja, kuna watu wanaandikiwa dawa haendi kununua, yeye anaenda kujua tatizo, kuhusu dawa atatumia azijuazo, ambazo pengine zikamleta shida, Tatizo linazidi, au usumbufu zaidi kwa Dr. Ambao haukua na lazima..

Ila kwa Picha hii, inaleta mswali.
 
Shida sio kumpa dawa, yani hata kuwaandikia dawa inayatakiwa kutibu tatizo lake wamegoma mpaka wahakikishe ana hiyo elfu 30 ndipo wamuandikie...

Yani target yao ni wauze dawa, ambalo ni jambo lisilomhusu mgonjwa.

Mgonjwa kalipia kila kitu ikiwemo kumuona daktari na vipimo, majibu yameonesha tatizo lilipo, kwa nini usimuandikie dawa akamunue mbele ya safari kama hana pesa kwa muda huo?
ungeenda kwa MKuu wa Kituo, toa malalamiko yako, ukiona hajakusaidia, nenda viongozi wa wilaya.
 
Poleni sana. lakini wakati mwingine tuwe wakweli, hizo dawa haziokotwi, zinauzwa, hivi ungekuwa wewe ungefanyaje? na ukimhudumia mtu akasema hana hela na umempa dawa boss wako anakuja kukudai hiyo hela ya dawa utakuwa mgeni wa nani?
Hujaelewa, hajasema apewe bure bali aandikiwe wakanunue kwa wakati wao, inamaanisha vipimo walishalipia
 
Malalamiko kwa Wizara ya Afya kwenda Hospitali ya Kitengule iliyoko Tegeta jijini Dar es Salaam.

Leo ndugu yangu alizidiwa ghafla, ikabidi wakimbize Kitengule kwani wanaishi karibu na hapo.

Alikuwa na tatizo la mguu kupata ganzi, na kupata maumivu ya mgonjo, tatizo ambalo limekuwepo kwa muda sasa. Hivyo leo maumizi yalizidi ndipo wakaamua wamuwahishe hapo Kitengule.

Baada ya vipimo ikiwemo xray, ameonekana ana tatizo kwenye misuli ya mgongo, ndiyo inayompelekea mpaka anapata ganzi za mguu.

Hivyo walianza na kumpa "Physiotherapy" kwanza ndipo wakafuatia suala la kumpa dawa.

Kimbembe kimekuja hapa kwenye dawa, daktari alowahudumia akawaambia dawa zinacost elfu 30 (30,000/=). Ndugu kwa wakati huo wakawa wameishiwa pesa, wakamuomba daktari japo awaandikie hiyo dawa kisha watanunua baadaye wakishajipigapiga angalau wanunue hata za kuanzia.

Cha kushangaza daktari amegoma katakata kuwandikia dawa kama hawana hiyi elfu 30. Na akaondoka kabisa ofisini kwake maana ilishakuwa jioni..

Hili jambo ni jipya kwa utaratibu wa matibabu ulivyo. Mgonjwa akishalipia gharama ya matibabu ina maana ni pamoja na kuandikiwa dawa la tatizo lake lililogundulika baada ya vipimo.

Wajibu wa daktari ni kumuandikia dawa mgonjwa, suala la atanunulia wapi halimuhusu, kama ipo hapo hospitali husika basi ni jambo jema, kama haipo basi ni haki ya mgonjwa kuandikiwa "Prescription" ili akanunue mahali inapopatikana.

Ni kosa kisheria na kimaadili kwa daktari kukataa kumuandikia mgonjwa dawa kwa sababu yoyote ile. Huyu mgonjwa akipatwa na lolote huko aliko huyo daktari na Hospitali kwa ujumla watakuwa wamehusika 100% kufa kwake.

Bado sijapata jina la huyo daktari, lakini nikilipata nitaliweka wazi hapa ili wahusike wasaidie kukomesha hawa wahuni walioingilia fani nyeti kama hii inayohusika na uhai wa wanadamu wenzetu.

Wizara ya Afya Tanzania

Wizara Maendeleo ya Jamii

View attachment 2771797

View attachment 2771798
Sasa ile private hospital ......kama huna bima wala pesa ulitakaje ? Atalipaje mishahara na kununua dawa umeme gharama uendeshaji ? Kila mtu atakuja na free ataweza ? Tuheshimu hospital za wawekezaji ile sio ya serikalii
 
Mkuu au mimi sijaelewa? Sidhani kama alitaka apewe bure,
Naahisi alitaka apewe jina la dawa ili akanunue mwenyewe anapoamini pana unafuu labda..
Hapo hoja ya Dr. Ilikua ni kwamba siruhusu mtoke bila kuona dawa, yaani katika picha ya Maendeleo ya mgonjwa, akiamini ya kua mnaweza msinunue.
Uko sahihi
 
Sijaelewa Kama mgonjwa alinyimwa dawa au daktari aligoma kumuandikia mgonjwa jina la Dawa.

Kama hiyo hospitali ni private, daktari Yupo sahihi unless inapokea angalau 50% ya ruzuku kutoka wizarani.

Kwa kuongezea, ukiwa na rundo la ndugu ambao ukihitaji elfu 30 ya haraka unakosa, basi ni bora uwapunguze
 
Poleni sana. lakini wakati mwingine tuwe wakweli, hizo dawa haziokotwi, zinauzwa, hivi ungekuwa wewe ungefanyaje? na ukimhudumia mtu akasema hana hela na umempa dawa boss wako anakuja kukudai hiyo hela ya dawa utakuwa mgeni wa nani?
Kama nimemuelewa mleta mada nikamba....
Analalamika kuhusu Dr kuto kumuandikia dawa mgonjwa na sio kumpatia dawa mgonjwa.
 
Poleni sana. lakini wakati mwingine tuwe wakweli, hizo dawa haziokotwi, zinauzwa, hivi ungekuwa wewe ungefanyaje? na ukimhudumia mtu akasema hana hela na umempa dawa boss wako anakuja kukudai hiyo hela ya dawa utakuwa mgeni wa nani?
Hawakutaka wapewe dawa bure, walitaka waandikiwe ili wakifika nyumbani wanunue.
 
Mtindo huu unafanywa na hospitali nyingi za binafsi, watakupima na kukupa jibu ila usiponunua dawa yao hawakuandikii dawa ya kununua kwingine.
Maadili hayawaruhusu wahudumu wa afya ikiwemo madaktari kufanya kitu cha namna hii, huu ni uuaji.

Mgonjwa ana haki ya kuandikiwa dawa inayotakiwa kulingana na tatizo lake na ana haki ya kwenda kununua dawa popote anapoona panamfaa, halazimishwi kununua hospitali ileile..

Mgonjwa kama ameshindwa kumudu gharama za dawa husika, huwa kuna "Alternative Drugs" za bei ya chini ili angalau zikamsaidie hata kama haziko sawa na zile alizokusudia..
 
Sasa ile private hospital ......kama huna bima wala pesa ulitakaje ? Atalipaje mishahara na kununua dawa umeme gharama uendeshaji ? Kila mtu atakuja na free ataweza ? Tuheshimu hospital za wawekezaji ile sio ya serikalii
Soma uzi mzima acha kukurupuka kwa kusoma heading tuu..

Hakuna sheria wala taratibu za kitabibu zinazomtaka mgonjwa anunue dawa mahali alipotibiwa tuu...

Taratibu zinamtaka mgonjwa aandikiwe dawa kulingana na tatizo lake.

Kitendo cha kukataa kumuandikia dawa kisa hana pesa ni sawa sawa na kuua.
 
Malalamiko kwa Wizara ya Afya kwenda Hospitali ya Kitengule iliyoko Tegeta jijini Dar es Salaam.

Leo ndugu yangu alizidiwa ghafla, ikabidi wakimbize Kitengule kwani wanaishi karibu na hapo.

Alikuwa na tatizo la mguu kupata ganzi, na kupata maumivu ya mgonjo, tatizo ambalo limekuwepo kwa muda sasa. Hivyo leo maumizi yalizidi ndipo wakaamua wamuwahishe hapo Kitengule.

Baada ya vipimo ikiwemo xray, ameonekana ana tatizo kwenye misuli ya mgongo, ndiyo inayompelekea mpaka anapata ganzi za mguu.

Hivyo walianza na kumpa "Physiotherapy" kwanza ndipo wakafuatia suala la kumpa dawa.

Kimbembe kimekuja hapa kwenye dawa, daktari alowahudumia akawaambia dawa zinacost elfu 30 (30,000/=). Ndugu kwa wakati huo wakawa wameishiwa pesa, wakamuomba daktari japo awaandikie hiyo dawa kisha watanunua baadaye wakishajipigapiga angalau wanunue hata za kuanzia.

Cha kushangaza daktari amegoma katakata kuwandikia dawa kama hawana hiyi elfu 30. Na akaondoka kabisa ofisini kwake maana ilishakuwa jioni..

Hili jambo ni jipya kwa utaratibu wa matibabu ulivyo. Mgonjwa akishalipia gharama ya matibabu ina maana ni pamoja na kuandikiwa dawa la tatizo lake lililogundulika baada ya vipimo.

Wajibu wa daktari ni kumuandikia dawa mgonjwa, suala la atanunulia wapi halimuhusu, kama ipo hapo hospitali husika basi ni jambo jema, kama haipo basi ni haki ya mgonjwa kuandikiwa "Prescription" ili akanunue mahali inapopatikana.

Ni kosa kisheria na kimaadili kwa daktari kukataa kumuandikia mgonjwa dawa kwa sababu yoyote ile. Huyu mgonjwa akipatwa na lolote huko aliko huyo daktari na Hospitali kwa ujumla watakuwa wamehusika 100% kufa kwake.

Bado sijapata jina la huyo daktari, lakini nikilipata nitaliweka wazi hapa ili wahusike wasaidie kukomesha hawa wahuni walioingilia fani nyeti kama hii inayohusika na uhai wa wanadamu wenzetu.

Wizara ya Afya Tanzania

Wizara Maendeleo ya Jamii

View attachment 2771797

View attachment 2771798
Vipi na hospital za serikali ambazo kama hauna hela ya dawa hawakupi cheti kabisa?

Mimi naona ni Yale Yale maana private wanakupima, wanakwambia ugonjwa ulionao, kama hauna hela ya dawa unaondoka na Chet bila ya kuandikiwa dawa wakati serikalini unapimwa, unaambiwa ugonjwa ulionao, wanakuandikia dawa kama hauna hela ya dawa wanakizuia cheti (Kadi) kwahyo huwezi kununua popote dawa Hadi urudi kwao

Kwahyo kama unaishotaki hospital ya private kwa kufanya hivyo, nakukumbusha kuwa hata serikalini wanafanya ivoivo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom