Malenga ninawajia, kisima nakisifiaMachoni kinavutia, nakipa mia kwa miaumbo lake asilia, bado halijafuliaKisima hiki kisima, raha kinanipatiaNdani ninavyo ingia, akili zangu zarukaNabaki kushangilia, machozi yabubujikaSi kama eti nalia, mwenzenu nafurahikakisima hiki kisima, raha kinanipatiaKasoro sijaiona, ya kisima nawambiaNinapotazama kina, walahi nimeridhiaUkija kwenye upana, wala haujazidiakisima hiki kisima, raha kinanipatiaKingo ninapozishika, taratibu natelezasifanyi kupaparika, bingwa wa kucheza chezakiu inapo ondoka, pembeni najisogezakisima hiki kisima, raha kinanipatiaNa leo ninatangaza, miliki najipatiasitaki kuja kuwaza, mbona nilikiachiayeyote nitacharaza, atakae karibiakisima hiki kisima, raha kinanipatiaNa Sindano Mwana wa Ganzi (SMG)