Kisiasa, mwaka 2017 CCM imeimarika sana!

Kisiasa, mwaka 2017 CCM imeimarika sana!

Ni imeimarika sana ila ili tujiridhishe zaidi hebu fanyeni kuondoa vikwazo mikutano ya kisiasa kama enzi za JK
mikutano ya siasa yenye tija na maendeleo kwa jimbo haikatazwi.
 
Inaimarika kwa kudhoofisha wenzake?

Jambo la msingi kwa watawala ambalo wanapaswa kujiuliza kabla hawajatumia nguvu zaidi kutaka kuua upinzani ni hili:

Kwanini Mwl. Nyerere aliwakubalia wale wachache 20% na kuwanyima walio wengi 80% ambao ndio waliyakataa mageuzi?

Inapaswa watawala wafahamu kwamba Upinzani upo MOYONI na sio MACHONI

Hila na dhuluma hizi wanazowafanyia watanzania ni kuwalimbikizia HASIRA ndani ya mioyo yao na siku zitakapolipuka ndio tutajua kwamba MAGEUZI ndio mfumo wa kidunia HAYAEPUKIKI

Watawala fanyeni wajibu kwa haki msitumie hila.
 
Namtakia salamu za heri ya krismasi na mwaka mpya 2018 mwenyekiti wa CCM Taifa.

Sio siri mwaka huu CCM imefanikiwa sana kisiasa na kiutendaji pia.

CCM imefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kutekeleza ilani yake na ahadi kwa wananchi.

Yapo mengi ya kujivunia na kutembea kifua mbele kama chama dola.

Vita dhidi ya ufisadi na mafisadi ilipamba moto mwaka huu.

Utetezi wa rasilimali za nchi ni jambo kubwa sana kwa serikali chini ya CCM Kujivunia.

Vita dhidi ya rushwa ndogo na kubwa imeimarika na hatua zimechukuliwa na kuonekana kuchukuliwa.

Maendeleo kwa wananchi wa hali ya chini yameanza kuonekana vilivyo.

Tija katika masoko na bei za mazao ya kilimo hasa hasa kwenye korosho imeonekana.

Viwanda vimeanza kujengwa hasa hasa katika mkoa wa pwani.

Tumeshuhudia uzinduzi wa miradi mikubwa ya maji hasa katika maeneo korofi kama Sengerema na longido.

Fedha za kutosha katika afya hasa eneo la dawa na vifaa tiba imesaidia kubiresha huduma za afya nchini.

Ujenzi wa miuondo mbinu kama ya barabara na madaraja ni eneo lililodhihirisha umadhubuti wa serikali ya JPM.

Kufufuka kwa shirika letu la anga na ndege sio jambo la kubezwa.

Mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu imeongezwa na kutolewa kwa wakati na kwa wanaostahili.

Kurejeshwa kwa ardhi zilizopokwa na mafisadi na wabinafsi imewapatia faraja wananchi waliozulumiwa.

Kuondolewa kwa vihiyo na vilaza katika sekta ya huduma za umma sio jambo dogo lakini limefanyika kwa ustadi na werevu wa hali ya juu.

Mikopo kwa vijana na wanawake imewafikia walengwa kwa mara ya kwanza.

Uwajibishwaji wa papo kwa papo kwa viongozi wazembe wa umma umeonesha nia na dhamiri safi ya Serikali ya JPM.

Ukusanyaji wa kodi halali za serikali umeumeonesha uimara wa Serikali ya JPM.

Utalii umeboreka huku ujangili dhidi ya Tembo na wanyama wengine muhimu umepungua kwa kasi.

Usimamizi wa rasilimali zetu kama nchi umeimarishwa kiusimamizi na kisheria.

CCM imeweza kuwavutia wanachama muhimu na wengi wa vyama vya upinzani hadi wakajiuzulu na kujiunga na CCM ili kuwa huru na kumsupport Magufuli katika kuleta maendeleo ya mama Tanzania.

Chini ya uwenyekiti wa Rais Magufuli CCM imeweza kuunganishwa upya na kutoa fursa kwa kila mwanaccm.

WanaCCM wote wanapaswa kuyatambua mazuri mengi yaliyotekelezwa na kikosi kazi chini ya Rais Magufuli...na hivyo wanatakiwa kuyasema na kuwaelimisha wananchi.

Yapo mengi ya kuyaelezea lakini kwa kifupi naweza kuyataja haya.

Tuingeze mengine ili tujitathmini kama nchi.

Mungu amponye na kumlinda Rais wa Jamhuri huru ya Tanzania ambaye pia ni mwenyekiti wa chama dola CCM ndugu John Pombe Magufuli.

Magufuli as expected has shown the world that he is more than a politician...he is a performance oriented leader!!


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!
Ila katika statement yako mwishon usisahau KWA MTUTU WA BUNDUKI usiliache hilo neno ni muhimu sana kwa mustakabali wa uimarikaji wa CCM mwaka 2017usiliache hilo kuliweka kwenye hoja yako.
 
Inatia faraja sana!inaleta ari ya kumshabikia na kumpambania Magufuli
Ujinga wenu huwa hauwaishi mnampambania magufuli?mnampambaniaje magufuli?kwa nini mnatumia nguvu nyingi sana kumpamba ? Maana nijuavyo mimi chema chajiuza chenyewe bila hata promotion! Mbona nawaona promotion zina zidi ? Au ndio sio chema ? Halafu tikiwaambia UVCCM wengi hamna akili mnanuna , mnaimarika kivipi wakati hampo kwenye ushindani?
 
Imeimarika ndio. Lakini kwa kuingia ulingoni na kumwelekeza refa kumfunga mikono bondia waliyenaye ulingoni. Hongereni sana
 
Hakuna demokrasia nzuri kama kuteua wapinzani katika nafasi za kiserikali.Hilo limefanyika mwaka huu
Hao wapinzan kina nani? Wapinzani makada watiifu?? Matawi yenu nayo ni wapinzani? Weken bunduki chini kwanza zipigane hoja hapo ndio tutaujua uwezo wenu na huko kuimarika mnako imba mmezuia watu kufanya siasa kwenye majimbo ya wengine halafu kina tulia wanashinda kugawa misaada kwenye majimbo ya wenzao wakati walio tenda kama wao walikamatwa!? Kweli CCM inaimarika kwa mtutu wa bunduki na utekaji nyaraa
 
mikutano ya siasa yenye tija na maendeleo kwa jimbo haikatazwi.
Kwahiyo katiba inaelekezaje mkuu au mnaikanyaga tu mjuavyo ninyi,

Je chama ca siasa kikifanya mikutano kwa ajili ya kujiimarisha ni kosa kubwa kwenu sio

Yaani mnapenda kusikia mnachokitaka tu sio
 
Hakuna aliyetarajia ikani ya ccm kutekelezwa vilivyo ndani ya muda mfupi hivi!

Huku kushuka kwa uchumi ni sehemu ya hiyo ilani? kwanini vitisho na hata matumizi mabaya ya madaraka dhidi ya wanaosema ukweli dhidi ya awamu hi yameshamiri zaidi?
 
Namtakia salamu za heri ya krismasi na mwaka mpya 2018 mwenyekiti wa CCM Taifa.

Sio siri mwaka huu CCM imefanikiwa sana kisiasa na kiutendaji pia.

CCM imefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kutekeleza ilani yake na ahadi kwa wananchi.

Yapo mengi ya kujivunia na kutembea kifua mbele kama chama dola.

Vita dhidi ya ufisadi na mafisadi ilipamba moto mwaka huu.

Utetezi wa rasilimali za nchi ni jambo kubwa sana kwa serikali chini ya CCM Kujivunia.

Vita dhidi ya rushwa ndogo na kubwa imeimarika na hatua zimechukuliwa na kuonekana kuchukuliwa.

Maendeleo kwa wananchi wa hali ya chini yameanza kuonekana vilivyo.

Tija katika masoko na bei za mazao ya kilimo hasa hasa kwenye korosho imeonekana.

Viwanda vimeanza kujengwa hasa hasa katika mkoa wa pwani.

Tumeshuhudia uzinduzi wa miradi mikubwa ya maji hasa katika maeneo korofi kama Sengerema na longido.

Fedha za kutosha katika afya hasa eneo la dawa na vifaa tiba imesaidia kubiresha huduma za afya nchini.

Ujenzi wa miuondo mbinu kama ya barabara na madaraja ni eneo lililodhihirisha umadhubuti wa serikali ya JPM.

Kufufuka kwa shirika letu la anga na ndege sio jambo la kubezwa.

Mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu imeongezwa na kutolewa kwa wakati na kwa wanaostahili.

Kurejeshwa kwa ardhi zilizopokwa na mafisadi na wabinafsi imewapatia faraja wananchi waliozulumiwa.

Kuondolewa kwa vihiyo na vilaza katika sekta ya huduma za umma sio jambo dogo lakini limefanyika kwa ustadi na werevu wa hali ya juu.

Mikopo kwa vijana na wanawake imewafikia walengwa kwa mara ya kwanza.

Uwajibishwaji wa papo kwa papo kwa viongozi wazembe wa umma umeonesha nia na dhamiri safi ya Serikali ya JPM.

Ukusanyaji wa kodi halali za serikali umeumeonesha uimara wa Serikali ya JPM.

Utalii umeboreka huku ujangili dhidi ya Tembo na wanyama wengine muhimu umepungua kwa kasi.

Usimamizi wa rasilimali zetu kama nchi umeimarishwa kiusimamizi na kisheria.

CCM imeweza kuwavutia wanachama muhimu na wengi wa vyama vya upinzani hadi wakajiuzulu na kujiunga na CCM ili kuwa huru na kumsupport Magufuli katika kuleta maendeleo ya mama Tanzania.

Chini ya uwenyekiti wa Rais Magufuli CCM imeweza kuunganishwa upya na kutoa fursa kwa kila mwanaccm.

WanaCCM wote wanapaswa kuyatambua mazuri mengi yaliyotekelezwa na kikosi kazi chini ya Rais Magufuli...na hivyo wanatakiwa kuyasema na kuwaelimisha wananchi.

Yapo mengi ya kuyaelezea lakini kwa kifupi naweza kuyataja haya.

Tuingeze mengine ili tujitathmini kama nchi.

Mungu amponye na kumlinda Rais wa Jamhuri huru ya Tanzania ambaye pia ni mwenyekiti wa chama dola CCM ndugu John Pombe Magufuli.

Magufuli as expected has shown the world that he is more than a politician...he is a performance oriented leader!!


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!

imefanikiwa na kuuwa nakuteka watu
 
Tumeimarika mnoo lakini kwa gharama kubwa sana..think and digest..Lakini tusijisahau upinzani huwa mioyoni mwa watu na sio kwa viongozi wao "wanaohamia" kwetu. Natamani 2018 tuwafungulie minyororo tuone wamakufa kiasi gani na kupima uimara wetu CCM.
 
Back
Top Bottom