Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,775
- 218,396
Awamu ya Pili ya mpango kabambe wa kuwaamsha wananchi wa Tanzania kudai Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi, ambao sasa umeongezewa kipengele cha "Okoa Bandari Zetu," unaanza rasmi 28/07/2023 Mkoani Kagera.
Taarifa iliyosambazwa na Chadema kote duniani inaonyesha kwamba mkutano mkubwa wa hadhara wa kuzindua kampeni hiyo utafanyika kwenye Uwanja wa Mashujaa, Manispaa ya Bukoba na utaongozwa na Mwamba Mwenyewe Freeman Mbowe akiwa pamoja na Tundu Lissu.
Nimebahatika kuwemo kwenye Timu ya Wataalam Wasomi, waliokagua Chopa itakayotumika kwa mashambulizi ya angani. Kiukweli, chama kimejipanga na sasa kimekomaa hasa, mipango yake ni ya kisasa mno hadi inashangaza! Watu wa Kagera wana bahati sana kwa kampeni hii, kuanzia kwao, maana kila kitu ni kipya kabisa, hadi mic ni mpya!
Kama kawaida, mimi mtumishi wenu Erythrocyte nitawaletea kila kitakachojili.
Mungu ibariki Chadema.
Taarifa iliyosambazwa na Chadema kote duniani inaonyesha kwamba mkutano mkubwa wa hadhara wa kuzindua kampeni hiyo utafanyika kwenye Uwanja wa Mashujaa, Manispaa ya Bukoba na utaongozwa na Mwamba Mwenyewe Freeman Mbowe akiwa pamoja na Tundu Lissu.
Nimebahatika kuwemo kwenye Timu ya Wataalam Wasomi, waliokagua Chopa itakayotumika kwa mashambulizi ya angani. Kiukweli, chama kimejipanga na sasa kimekomaa hasa, mipango yake ni ya kisasa mno hadi inashangaza! Watu wa Kagera wana bahati sana kwa kampeni hii, kuanzia kwao, maana kila kitu ni kipya kabisa, hadi mic ni mpya!
Kama kawaida, mimi mtumishi wenu Erythrocyte nitawaletea kila kitakachojili.
Mungu ibariki Chadema.