Kisarawe kupata maji safi leo, Pugu, Ukonga, aprili mwakani

elivina shambuni

JF-Expert Member
May 31, 2018
461
295
1572935693937.png


WAKATI wakazi wa mji wa Kisarawe mkoani Pwani, wakitarajia kuanzia leo kupata majisafi ya Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (Dawasa), wakazi wa Ukonga, Ukonga Magereza, Gongo la Mboto, Pugu na Banana wilayani Ilala, watapata majisafi ifi kapo Aprili mwakani.

Hayo yamebainishwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa, Cyprian Luhemeja wakati akieleza maendeleo ya mradi mkubwa wa maji wa Kisarawe kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Dawasa, Jenerali Davis Mwamunyange, jana.

Mwamunyange aliipongeza Dawasa kwa kutekeleza mradi huo mkubwa kwa kutumia fedha zao za ndani, wakati kwenye miradi mingine mingi wamekuwa wakipewa fedha za serikali. Alisema mradi huo ni wa kihistoria na wa mfano kwa mamlaka zingine za maji nchini. “Kazi kubwa imefanyika Kisarawe. Mradi umekamilika kwa asilimia 99, zimebaki kazi ndogo ndogo, leo ilikuwa niwashe pampu ya maji kwenye tangi kubwa la Kisarawe, lakini bado kazi ndogo sana za kukamilisha” alisema Mwamunyange.

Aliwaeleza wakazi wa Kisarawe kuwa Dawasa imetekeleza kikamilifu na kwa haraka agizo lililotolewa na Rais John Magufuli la kuondoa kero ya maji katika mji huo. Luhemeja alifafanua kuwa Dawasa imetekeleza mradi huo wa Kisarawe, kwa kutumia fedha za ndani na umegharimu zaidi ya Sh bilioni 10. Alisema mradi huo utahudumia wananchi zaidi ya 25,000.

Luhemeja alisema tangi kubwa lililojengwa Kisarawe, litahifadhi maji mengi kuliko mahitaji ya mji wa Kisarawe, hivyo Dawasa imeamua kuongeza mtandao wa maji katika maeneo mengine ya jirani, yatakayohudumiwa na tangi hilo kubwa. Alisema wameanza kujenga tangi dogo eneo la Pugu, litakalorahisisha usambazaji maji ya Dawasa maeneo ya Pugu, Ukonga, Ukonga Magereza, Gongo la Mboto na Banana wilayani Ilala.
 
Apo ndio maji huwa yananichanganya ,yameruka maeneo ya karibu yamefika maeneo ya mbali

Maji ya TZ hayatofauti na umeme ,nakumbuka kipindi fulani nilitembelea kijiji kahama umeme umekiruka kijiji unaenda mbele kuna kimgodi kidogo
 
Apo ndio maji huwa yananichanganya ,yameruka maeneo ya karibu yamefika maeneo ya mbali

Maji ya TZ hayatofauti na umeme ,nakumbuka kipindi fulani nilitembelea kijiji kahama umeme umekiruka kijiji unaenda mbele kuna kimgodi kidogo
yaani sehem kubwa ya KIBADA hakuna maji ya bomba, lakini maji yamekwenda pugu na gongo la mboto, labda 'kasungura' kanyewe ni kadogo!
 
58 years after independence tunaongelea maji. Maji. Yaani maji. I rest my case
 
58 years after independence tunaongelea maji. Maji. Yaani maji. I rest my case
Sijui mtatumia hoja gani ufipa kuwaaminisha wananchi waje kubanana ufipa nanyi.
Najua imekuuma sana hoja ya maji nayo imefutwa a serikali hii.
 
Kisarawe na mto ruvu ni karibu zaidi kuliko hayo maeneo ya pugu, g/mboto na banana ndio maana imekuwa rahisi kisarawe kufikiwa na mradi kwa urahisi.
 
Back
Top Bottom