Elections 2010 KIravu ulikuwa unafahamu ulichokuwa unaongea

quimby_joey

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
390
164
jana nilipata wasaa wa kumsikiliza huyu kibaraka wa CCM na serikali yake, Rajabu Kiravu wakati akijibu swali la mwandishi mmoja. Jamaa kwa kujiamini kabisa akasema jamii ya watanzania inafuga wezi na kuwakumbatia, mwizi ambaye anjulikana mtaani kama mtoto wa mzee fulani hata siku moja hawezi kukamatwa, kunyooshewa kidole wala kuitwa mwizi, mwizi ni yule anayetoka mbali ambaye hafahamiki pale. Kiravu alikuwa hajui kuwa kutokana na wao kumfaham Kikwete, na ndiye aliyewaweka pale basi hata kama ameiba kura yeye si mwizi, ila slaa anayelalamika kwasababu ni mgeni hafahamiki ananyooshewa kidole kuwa ni mchochezi anayechochea vijana wafanye vurugu kisa maslahi yake binafsi. jamani tunaburuzwa, haya ni matusi.
 
Tatizo la watu kama wewe "NEGATIVE MINDED PEOPLE" ni kuwa "unapoliendea jambo fulani unatafuta makosa tu mazuri hutafuti"

We ni miongoni mwa watanzania wengi "waliofurahishwa na ubeti uliongezwa wa 'TUNATAKA MABADILIKO' ". Mbona mabadiliko haya yanatetewa wanapokosa CHADEMA? au huu ubeti ulitakiwa uwe "TUNATAKA CHADEMA ITAWALE" watanzania mfano wako mko wengi na mabadiliko mnayoleta ni kutuchomea shule na ofisi za serikali, Hamna maana yoyote

Kiravu alikuwa anajibu maswali kwa usahihi kulingana na uelewa wake
 
Ni kweli alijibu kulingana na uelewa wake kwa sababu kwa mtu wa level yake siamini kama anaweza kuwa kibaraka ,labda kama shule alienda kusoma si kuelimika .Lakini majibu yake yamedhihirisha kuwa aidha ni kilaza au ni kibaraka asiyena haya usoni
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom