Kipo wapi Kiwanda cha saruji Shinyanga?

Kipo wapi Kiwanda cha saruji Shinyanga?

monaco

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2012
Posts
2,184
Reaction score
1,779
Huu tunaambiwa ni Uchumi wa Viwanda,Serikali ya Viwanda,ziliwahi Kuwa Tetesi kuanzishwa kwa Kiwanda Cha cement Shinyanga maeneo ya Kizumbi.Kiwanda ambacho kingeweza Kusambaza cement mikoa ya Shinyanga,Mwanza,Musoma,Simuyu Kagera na Hata Geita-Chatto.
Sijui ndoto hizo zilifia wapi?

Ila Vijiweni napo maneno hayaishi Kuwa Mkoa huu baadhi ya "Matajiri"

Hawapendi mkoa uendelee kwa Kuwa Wanapopeleka Marobota ya Pamba Dar as salaam na malori na kurudi na Cement
Lakini sasa tumeambiwa Kuna Kiwanda cha Nyuzi na Nguo,Bariadi

Na Ni wakati Muafaka sasa wa Kuendeleza Uchumi wa Viwanda kwa kuanzisha Kiwanda cha Cement Shinyanga kwa Kuwa malighafi muhimu zipo kama:
1.Limestone reserve,
2.Redsoil

Labda Power supply ndo ikosekane....yaani Umeme, na Fuel for firing,kuchomea clinker,
Sababu sasahivi hakuna Kununua Coal kutoka south Africa,inatakiwa itoke songea au Mbeya.

Mwisho wa yote Mkoa huu Msiusahau sana sana,ndio umekuwa ukilisha Dar na Tanzania kwa kipindi kirefu sana sana,Kwa Kuwa na Migodi kama Mwadui,Kahama mining,buzwagi na Mifugo inayotoka kwa wingi Mkoa huu!

Shinyanga Imekosa tuu Msemaji....yaani wa kuisemea wengine waliopo wapo Strategic tuu kwa maslahi yao binafsi tens wala Sio maslahi ya Chama Dola hapana!

Nawasilisha!
 
Huu ukanda ukipata kiwanda cha saruji na bei ikawa kama Mtwara enzi za Dangote au Dar naamini sekta ya ujenzi itakua sana hata nyumba za makazi tu.
 
Mbunge wetu Masele amepata kazi Katika Bunge LA Africa ndiyo maana !
 
Nadhani upatikanaji wa raw material kwa gharama ya chini ndo tatizo...maana mtu anaweza akawwka kiwanda akajikuta anauza bei sawa na ya dar au zaidi

Kuna kiwanda cha mabati ukiwa unaelekea viwandani barabara ya mwanza sina hakika kama kinaendelea vizuri
 
Back
Top Bottom