Kipindi cha Njiapanda cha Clouds fm, lengo kuu ni nini?

Kipindi cha Njiapanda cha Clouds fm, lengo kuu ni nini?

watanzania ni watu wavivu sijapata ona. unakuta eti kijana mzima wa afya na hana ulemavu wowote anadai eti yeye yatima asaidiwe!!! Kwani uyatima ndio ubaki kulia lia?
 
Hilo hitimisho lako ndilo sahihi kupita maelezo ila mengine yote ni kupingana na masilahi ya hicho chombo kumbuka kuwa ile ni sehemu ya biashara

Kama ni sehemu ya biashara unataka kusema hata hao jamaa wenye shida wanalipia ndio wanarushwa hewani?
 
Nipo tofauti kidgo nawe.
Katika story ya mtu,.kuna maonyo na mafunzo.mengi ambayo jamiii huweza kuipata,.pia kwa mtoa story huweza jikuta amesogea katika mikono itayoweza kumsaidia.
Kuna ambao huchangaiwa pale n.k

Nikweli kabisa kuna wenye matatizo mbali mbali wameshasaidiwa sana kupitia hicho kipindi.
 
Siamini kama wewe ni msikilzaji wa dhati wa kipindi hiki kama kweli wewe ni msikilizaji wa dhati basi jitahidi kuwa mkweli. Hiki kipindi kimesaidia sana watu wengi sana waliokuwa na matatizo makubwa lakini hilo hutaki kuliona ,watanzania tunatabia mbaya sana ya kupenda kukatisha tamaa watu wachache waojitahidi kuleta mchango fulani katika jamii,wewe at your level umefanya nini kusaidia jamii hii ya kitanzania ,njia panda kimekua voted ndio kipindi bora kabisa cha kijamii hapa TZ,tujivunze kuapriciate yale yanayofanywa na wengine.

Hao wengine wanakuwa na sababu zao nyingine za kuichukia hiyo radio na siyo sababu ya kipindi
 
kuna redio inaitwa PRAISE POWER 99.3FM nao kila asubuhi kuna kipindi cha majonzi, hivi unaanzaje siku na vipindi vya majonzi/matatizo? mara mwingine alibakwa na mjomba, mwingine aliambukizwa UKIMWI yaani vurugu tupu. USHAURI vipindi vya kusikitisha namna hiyo peleka saa 8-9 huko mchana. Asubuhi viwe vipindi vya kuchangamsha watu wakafanye kazi/kusaka noti
 
Binafsi sioni kama ni kibaya sana japo hakiwasaidii waathirika au wenye majanga of such
my take;
iwe cente ya kusaidia watu wenye uhitaji maarumu let us say anaye ingia hapo asaidiwe na watu wanao donate
bado tunahtaji kujua matatizo kwani kuna watu wnapata matumaini mapya ecourages nk
umma utambue matatizo si0wote wanajua kuwa kuna watu hawana hata mlo mmoja
sorry for typos

Kimewasaidia sana mkuu.watu wamechangiwa kwa,ajili ya elimu,afya na kibiashara.mim ni mmoja wa wachangiaji.
 
Hiki kipindi hurushwa kila Jumapili kuanzia saa 8 mchana. Nimekuwa nikikisikiliza kwa muda sasa, lakini sijatambua lengo kuu hasa la hiki kipindi ni nini. Maana nionavyo ni kama mtangazaji " anawachora" wale wageni wanaoeleza matatizo mule, na "wageni" wanavyojiachia na matatizo yao utafikiri kuna la maana atakalopata humo zaidi ya kupewa pole na watuma sms/ wasikilizaji.

Wajameni, Watanzania tupunguze malalamiko redioni, huu umaskini tulionao haumalizwi kwa kuhojiwa redioni. Tunapaswa kufanya kazi kwa bidii na pia kuwa na nidhamu na matumizi.

Ni hayo tu kwa leo.

Kimekuacha njia panda ! ? ....pole!
 
watanzania ni watu wavivu sijapata ona. unakuta eti kijana mzima wa afya na hana ulemavu wowote anadai eti yeye yatima asaidiwe!!! Kwani uyatima ndio ubaki kulia lia?


siku yakikukuta ndo utakugundua Dhiki haina Ujinga.

inshaallah days are numbered
 
Hawa watu walishawahi kumuhoji yule mtoto aliyeishi porini na nyani (Baraka) wakasema watamsaidia. Tangu wamemaliza kipindi mpaka sasa yapata miezi 6 hawajamsaidia chochote ambacho walikuwa wamehaidi kumsaidia mtoto baraka na mama yake mlezi. moja ya vitu walivyoahaidi cloude ni kumpatia shughuli ya kufanya yule mama na aliambiwa achague shughuli gani ya kufanya akasema ataweza kuuza kuku wa kienyeji na clouse walimpa ahadi ya kumpatia mtaji. mpaka sasa imekuwa ahadi hewa ili hali clouse wameingiza ela kwa kile kipindi.
 
Back
Top Bottom