Kipindi cha "Huyu ndiye Lowassa na Uchaguzi Mkuu wa 2015" kurushwa ITV usiku wa leo

Salary Slip

Platinum Member
Apr 3, 2012
49,323
152,126
Kitarushwa kuanzia saa 3:05 usiku wa Ijumaa ya leo.

Chanzo:ITV

Wenye "chuki" mjinyonge!

Update:
Kipindi kimeanza,ni tathimini ya yaliyojiri katika uchaguzi mkuu uliopita kutoka kuomba ridha ya CCM na baadae kuhamia CHADEMA na zoezi zima la kampeni.

Nikiangali picha kwakweli nakumbuka mbali na ninapata masikitiko fulani.All in all,kwa hizi picha zinazoonyesha maelfu ya watu,mh.Lowassa ameandika historia kubwa katika siasa za nchi hii.

Kuhama CCM na kujiunga CHADEMA na kisha kugombea uraisi kupitia CHADEMA /UKAWA, mh.Lowassa ameandika historia kubwa katika maisha yake ya kisiasa kulikoni kama angebaki ndani ya Chama cha Mapinduzi(CCM).

Ukweli lazima usemwe hata kama wengine hampendi.
 
Last edited:
Kipindi kina msaada mkubwa kwa sasa na baadae.Tujaribu kufikiria nje ya box na tuipende nchi yetu.
 
sasa kitasaidia nini hiki kipindi?
afu hapa ni kama kuna vinyongo fulan kwenye mioyo ya watu. unapokubali kuolewa usiulize nitalalaje na huyu mwanaume
Mh! Haya mama kila la kheri!
 
Mtoa Mada hii itakuwa kweli?

kama ndivyo naona kuna hatari ya ITV kufungiwa ikiwa mikutano ya kisiasa imepigwa marufuku
Je kipindi kama hicho kitakuwa salama?
 
Mh, mbona utata hapa!
Au kwa vile Mzee Lubuva alitwambia 'anasoma matokeo kadri anavyoletewa', ndio wanataka kutwambia ni nani alikuwa namletea!? Ngoja tusubiri
 
Treni imekwisha ondoka abiria wote walio chelewa watoke nje ya stesheni milango na mageti yanafungwa, rudini makwenu!!!!! Hapa haruhusiwi mtu kulala wala kupiga kambi. Mmesikia nyie. Eeehhhh!!!!!
 
Binadamu wabaya sana!! Yani watu kila kukicha wanakuja na mbinu za kutafuna pesa za huyu mzee...hukumu haiko mbali
 
sasa kitasaidia nini hiki kipindi?
afu hapa ni kama kuna vinyongo fulan kwenye mioyo ya watu. unapokubali kuolewa usiulize nitalalaje na huyu mwanaume
Mkuu Kwani mpaka unaolewa ulikua hujui dhumuni la hiyo ndoa ??
 
Mbona tunamfahamu kitambo kama fisadi nadhani hicho kipindi hakina tofauti na Diary ya Lady jay dee ama Wema in my shoes hongera kwake kwa kufuata nyayo za akina wema
 
Nawashangaa ITV kwanini hawakubali matokeo jamano na uzuri aliyeingia kwa kazi aliyoifanya tu kama mtu hujalewa maji ya ushabiki,huwezi ukawaza lowassa ambaye hata yeye anajua huu muziki unaoendelea asingeuweza,shame on you itv,na team nzima angalieni upepo sometimes
 
Back
Top Bottom