Kipima Joto ITV!! Mambo Bado Mazito Mtaani

Kipima Joto ITV!! Mambo Bado Mazito Mtaani

babalao 2

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
5,425
Reaction score
3,300
Kipimajoto kama ada kimetoa majibu tata kwa upande wa Rasimu ya Sitta.
Swali
Je katiba pendekezwa imekidhi mahitaji ya kukivusha kizazi hiki na kijacho salama?
Matokeo ni
79%------ HAPANA
18%------ NDIYO
03%------ SIJUI
Wataalamu huku kwa wananchi ni kimbembe zaidi.
Ikumbukwe kuwa ili iwe Katiba Rasmi inatakiwa
50% ya wananchi wa Tanganyika watakaopiga kura waseme ndiyo.
Na
50% ya wananchi wa Zanzibar watakaopiga kura wapigie ndiyo.
Kazi ipo
 
Hahahaha
Wachekeshaji wa mfalme kazini
 
Mchekeshaji ni wewe usiejitambua hizo ni takwimu za kipima joto kama wananchi walivyopiga kura pale ITV kwa hiyo wewe unapingana na uhalisia kwa kuwa tu umejivisha ujinga wa mapenzi kwa maCCM.

Nakumbuka Warioba kama vile aliwaambia Waje mtaani kwenyewe.
Sijui fungu la hongo litatosha kweli.
 
Kipimajoto kama ada kimetoa majibu tata kwa upande wa Rasimu ya Sitta.
Swali
Je katiba pendekezwa imekidhi mahitaji ya kukivusha kizazi hiki na kijacho salama?
Matokeo ni
79%------ HAPANA
18%------ NDIYO
03%------ SIJUI
Wataalamu huku kwa wananchi ni kimbembe zaidi.
Ikumbukwe kuwa ili iwe Katiba Rasmi inatakiwa
50% ya wananchi wa Tanganyika watakaopiga kura waseme ndiyo.
Na
50% ya wananchi wa Zanzibar watakaopiga kura wapigie ndiyo.
Kazi ipo

hata kule bmk kura zilikua hivi hivi ila ccm ni wataalam wa kupiga nyoka funika funua, tutarajie funika funua hata kwenye kura za maoni.
 
kweli UKAWA mnajifariji, hivi hizo takwimu ni za watu wangapi walio piga kura? ngoja hiyo katiba ije kwa wananchi wanaone itapita kwa asilimia ngapi?
 
hawa jamaa uwa siwahamini kabisa kama waliweza kutupiga changala la macho bungeni hata uku tu wataturaghai Mkuu usiweke asilimia kubwa kama hawa jamaa watashindwa uku
 
Ukiona unaelekea kushindwa,unaweza kumtafuta shetani akusaidie kushinda kama ccm walivyoshindaBMK lakini ushindi wa Mungu daima utadumu na si shetani.
 
Mchekeshaji ni wewe usiejitambua hizo ni takwimu za kipima joto kama wananchi walivyopiga kura pale ITV kwa hiyo wewe unapingana na uhalisia kwa kuwa tu umejivisha ujinga wa mapenzi kwa maCCM.

Na wew unakiamin kipima joto cha ITV kinacho hoji watu watatu wa hapo kinondon halafu ndo unataka ireflect Tanzania nzima mkuu huwezi kuwa serious ..
 
kweli UKAWA mnajifariji, hivi hizo takwimu ni za watu wangapi walio piga kura? ngoja hiyo katiba ije kwa wananchi wanaone itapita kwa asilimia ngapi?

Mkuu nawe siku hizi uko mitaa hii ya Lumumba nini kilikupata
 
Hakuna linaloshindikana ndani ya ccm wanajitekenya wenyewe na wanacheka wenyewe nini 50% wakitaka hadi 99% tanganyika na znz inapatikana,dawa yao 2015 tusifanye makosa tuongeze wabunge wa upinzani wakifika 300 tu ndani ya bunge ni silaha tosha,mambo mengi mazuri yatapita!!
 
Hakuna linaloshindikana ndani ya ccm wanajitekenya wenyewe na wanacheka wenyewe nini 50% wakitaka hadi 99% tanganyika na znz inapatikana,dawa yao 2015 tusifanye makosa tuongeze wabunge wa upinzani wakifika 300 tu ndani ya bunge ni silaha tosha,mambo mengi mazuri yatapita!!

Kweli mkuu
 
Swali la msingi kwa ccm ni Je,wanapita kwa halali kabisa ktk vitu vinavyotendeka?
Jiulizeni,sio kujiamini hapa kumbe si kihalali bali ni njia ovu zinatumika halafu mnajidai.Ipo siku watasema ss basi,haya matokeo si ya kwel.
 
Hivi hicho kipimajoto nacho ni kipindi cha kuleta kwa GT wakitumie kama sampling ya maoni ya watanzania?

Kipindi kinahoji watu 10 pale mikochoni viwandani ndo useme ni maoni ya watz??? Ama kweli mna matatizo vichwani. Na ndio maana mmeshupalia kusema maoni ya watu 17000 kuwa ni ya matanzania mln45. Mkiambiwa hamna akili mnakasirika lakini ndio ukweli wenyewe kwan hakuna kipindi cha kipumbavu kwenye tv za bongo kama kipimajoto itv na bango tbc.
 
Hapo hapana yangu haikuwepo nadhani ni asilimia 90 HAPANA

BACK TANGANYIKA
 
kweli UKAWA mnajifariji, hivi hizo takwimu ni za watu wangapi walio piga kura? ngoja hiyo katiba ije kwa wananchi wanaone itapita kwa asilimia ngapi?

Katiba ipite mara ngapi?wananchi watapiga kura ya ndio nyinyi nendeni mkaandamane na Mbowe
 
Mkuu nawe siku hizi uko mitaa hii ya Lumumba nini kilikupata

Chinkutentema, lazima tuseme ukweli, maani sidhani kama kuna mtu atatuma sms ya 120 halafu akajibu eti hajui, hivyo naona majibu yao sijui huwa yanajuisha watu wangapi kama sio wale wanahojiwa mabarabarani na wafanyakazi wenyewe!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom