Kipi bora kununua Hiace mpya kwa 30M ama kuchukua Tata Marcopolo kwa mkopo

Kwa kuwa unataka ushauri wa magari ngoja tukushauri kwenye magari ambao tumeshatoka huko.

1. Kwa lengo la mzunguko wa pesa ya chap chap na pressure juu, chukua TATA kwa sababu zifuatazo.
a. Vipuri vyake ni bei juu, na ufundi wake ni gharama, pindi kile cha upya kimeisha.
b. Ngoma ikichoka huwezi iuza mapema ukilinganisha na hiace utakayonunua.
C. Ukikomaa mlangoni ni vyema, ila kwa sababu wewe ni mgeni kwenye game, watakupgisha mswaki mwanzo mwisho, na jioni dereva anajua posho yake ipo, hivyo huna la kubisha maana hela ulikuwa unachukua wewe.
Mfano, kama wangekuwa wenyewe wangepanga foleni na kujaza level seat na wanaenda mdogo mdogo ila ukiwa nao wanakwambia foleni ndefu tuanze mbele huko wanakimbizana mwisho wa route unaenda mswaki na kurudi mswaki.. ( bora uwaache wenyewe wakuletee hesabu usiweke mpambe).
Hapa kama unaweza omba hata deiwaka kwanza kwenye magari kwa miezi kadhaa then ndo uwe na chombo yako uzuge nimepewa na uncle. Faida yake utajua konda/derva yupi chenga na yupi mzuri.

D. Mabao kwa costa na hiace hayatofautiana sana, ila costa/tata inaongoza,
E. Riba ya mkopo against na running expenses unatakiwa uliangalie haswa baada ya miezi 6-8 kuisha.

2. Chukua hiace/costa.( agiza japani)
Kwani hela yake ni 50 hadi 100k ni yako na ukiipata huwazi marejesho.
Wewe ni service na benk.
2. Ikichooka ni rahisi kufanyiwa matengenezo ikarudi karibia na upya kwa bei nafuu ukilinganisha tata.
3. Unaweza ukapata tenda ya kubeba wanafunzi wa shule na ikakulipa kwa rahisi kwa ruti za asubuhi na mchana.
Kingine u cane manage seven kuendesha mwenyewe.

Ushauri mwingine mbadala wa hayo magari/ iron businesses.
1. Cjui upo wapi ila fuga mbuzi wa nyama, fuga mbuzi tafuta eneo hiko singida kodi( hata heka 10.) Kashinde huko ununie mbuzi uwe na mbuzi 50 kwa kuanzia nakuapia baada ya mwaka na nusu. Hutaki tena hiace au tata.
2.ushauri mwingine usifanye haraka kwenye jambo lolote anza mdogo mdogo na usiwekeze mzigo wote kwenye 1 running business.

Nakutakia mafanikio mema, ukafanikiwe mwana jf
Salute kwako ndugu
 
Chukua hiyo ya kulaza 200k kwa siku ukipiga mwezi una milioni 6,
Ndani ya miezi sita ukitoa service ndogo ndogo unamaliza deni na kuanza kula faida,

Nb.
Kuwekeza kwenye biashara ya Usafiri kunahitaji Uvumilivu na kujitoa maana muda wowote kitu kikibuma/mnemba unapata lose.
Usimdanganye kuwa akimaliza deni anaanza kula faida kumbuka kuna pesa ambayo aliitanguliza kwa Mhindi zaidi ya M 25, so baada ya kumaliza deni, anatakiwa aanze kukusanya pesa aliyojikopesha ambayo ni M 25, ambayo ataikusanya zaidi ya miezi 6. so faida ataanza kuipata baada ya miezi 15.
 
Mkuu hao wa hindi wanahitaji ulipe angalau 50% ya bei ambayo ni kama 60m kwa hire purchase tena hizo Tata zinalaza 120,000 hadi 150,000 kwa route za Dar manaake utaendesha miaka miwili kumaliza deni Tata hiyo intakua imedepreciate sana, lakini kikubwa zaidi vipuri vya hizo gari nivipya na bei iko juu sana hamna used, utaendesha kwa pressure yeye muhidi hana hasara atakuambia ukate Bima kubwa incase yeye gari lake linarudi......tena mtu mwenye mali ya 120m hawezi kukaa kwenye mlango au usukani stress ninyingi utagonga na pia ma konda na madereva watakupiga vita paka uwachie gari.....unaweza ukafa kabla hujamaliza mkopo huo, jua kila sehemu/kazi inawenyewe acha wazarama waendesha dala dala zao utaumia zaidi tafuta biashara nyingine salama zaidi
Umeongea ukweli mtupu bila kupepesa macho. Ukweli Ndio huo uwezi kuwa na 30M ukae kwy ukonda utakufa na stress
 
Hiyo ni kila kitu usajili na TRA ile gharama zao umeshalipa mana kuna muda ushuru Wa serikali unazidi gharama ya Gari japan
Mkuu naona watu wanaongea wasiyoyajua kila mtu ni Mjuaji tuu lakini ukweli wa mambo hawayajui

Mie naomba nikupe experience yangu, nilichukua mwezi wa tatu Tata 105M. Unalipa 30% ambayo ni kama 30.15M. Bima kubwa 10.6M. Wanakukopesa 73.5 interest in 23% Jumla inakuja 92M kwa mwezi unarejesha 3.8M. Sasa mie niliipeleka mkoani inapiga route mkoa to mkoa baada ya kutoa matumizi yotee mafuta na posho inalaza 150k mpaka 250k siku hazilingani. inatembea masaa 8 mpaka tisa kwa siku gari haichoki tofauti na Dar inatembea zaidi ya masaa 15. Kwa mwezi unauhakika wa kulaza 4.5M mpaka 6M

Gari ikiwa bado mpya service ni oil tuu kila baada ya wiki inategemeana na urefu wa safari yako Max service Km ni 7000, Tairi na break baada ya muda kwa sababu inatembea kila siku.

Kila biashara ina changamoto watu wasikutishee kwani wanaoifanya wanawezaje. Tafuta dereva Mzuri konda weka ndugu yako unaemwamini utatembea kifua mbele. Baada ya miezi 24 unamaliza mkopo wako unaendelea kula maisha au uanweza kuuza hata 40M unarudisha hela yako. Gari ukiitunza vizuri inaweza kufanya kazi hata miaka zaidi ya 10.

Angalizo hii biashara hela ya hesabu usiende kulia bata inatakiwe uiwekee kwenye account na hyo account usiizoee fanya kama hauijuii kabisa maana gari muda wowote inaweza taka hela afu we hela ushalia bata ndo hapo unaposikia mtu amepaki gari. Siku zote hela za biashara usiziingize kwenye matumizi yako binafsi au ya nyumbani acha biashara ijiiendeshe yenyewe huku matumizi yako unayatoa sehemu nyinyinge

Ukihitaji Contact za Tata karibu. All the Best
 
Hiyo ni kila kitu usajili na TRA ile gharama zao umeshalipa mana kuna muda ushuru Wa serikali unazidi gharama ya Gari japan
Milioni 40 unapata Coaster na ushalipia kila kitu. Kama unataka kufanya hii business hata kwa ubishi anza na Coaster lako bila mkopo.
Screenshot_20191210-120428.jpeg
Screenshot_20191210-120219.jpeg
 
Habarini wanajamvi.

Ninaombeni msaada Wa kimawazo na ushauri kwa wenye uzoefu na hii biashara. IPI bora Nina 40M ninafikiria kuiwekeza kwa biashara ya huduma za usafirishahi Wa abiria.

Hapa nilipo nipo njia panda kati kununua hiace mpya inayo range 25-30M ama niende pale kwa wahindi niwape 30+M wanipe marcopolo tata mpya yenye zero mileage afu nawalipa kidogokidogo wanabaki na kadi original.

Hii inaweza ikaleta hesabu ya 200k kwa siku wakati hiace itanilazia 50k kwa siku. Hii tata mpya ninawazia mana ni mpya hivyo zile heavy services and spear replacement rate inakuwa ni ndogo kuliko hii used hiace.

Karibuni kwa wenye mawazo positives tushauriane katika kuusukuma umasikini mbali.
keisangora Chukua TATA , tafuta route nzuri na management nzuri , usimamizi wa maintenance,fuel na drivers ni muhimu na ndo changamoto kubwa otherwise hamna biashara yenye 0 challenges, ukishindwa kabisa fanya outsourcing zipo kampuni ninafanya usimamizi wa mabasi kwa makubaliano maalumu wewe yako ni hesabu ya siku tu , the rest wanadeal nayo wenyewe,mfano routes,drivers, maintenance, insurance, nk
 
Nimesoma coment zote mwanzo mwisho
wadau wametoa ushauri mzuri tena wakitaalamu na kiuzoefut

kulingana na mawazo yaliyotolewa humu, ni vema ukaufuatilia na kutekeleza ushauri wa kufungua hardware

Habarini wanajamvi.

Ninaombeni msaada Wa kimawazo na ushauri kwa wenye uzoefu na hii biashara. IPI bora Nina 40M ninafikiria kuiwekeza kwa biashara ya huduma za usafirishahi Wa abiria.

Hapa nilipo nipo njia panda kati kununua hiace mpya inayo range 25-30M ama niende pale kwa wahindi niwape 30+M wanipe marcopolo tata mpya yenye zero mileage afu nawalipa kidogokidogo wanabaki na kadi original.

Hii inaweza ikaleta hesabu ya 200k kwa siku wakati hiace itanilazia 50k kwa siku. Hii tata mpya ninawazia mana ni mpya hivyo zile heavy services and spear replacement rate inakuwa ni ndogo kuliko hii used hiace.

Karibuni kwa wenye mawazo positives tushauriane katika kuusukuma umasikini mbali.
 
Nenda Tata saivi wanauza kama 120M ivi ila unalipa 30% na Bima comprehessive 10M. gharama zingine ni TRA , Sumatra kama laki tano ivii. Gari ikiwa Mpya na ukipata dereva mzuri service ni oil tuu mpaka miezi sita
Achana na kitu ya kiindi au kichina, kama una uwezo nunua coster used au hata tipa la mkononi kuliko izo vitu za bara asia. Unaweza jikuta kabla ya kurudisha nusu ya mkopo unaanza tafuta engine na giabox za canter bure
 
Harware minimum mtaji shingap
Minimun nashauri iwe 10million japokua pungufu yahapo pía unaweza kufanya, 10-15m unaweza kuchukua mzigo kwa supplier mmoja a ukapewa mzigo wa 20-30m, sio vitu vyote kwenye hardware vinalipiwa cash, mfano baadhi ya mabati rangi nabaadhi yavitu vingine unaweza kuvipata bila kulipia kwajumla inategemea namakubaliano yako nasupplier. Kitu ambacho huwezi kukopeshwa ni gypsum, cement nabaadhi yavitu vingine
 
Minimun nashauri iwe 10million japokua pungufu yahapo pía unaweza kufanya, 10-15m unaweza kuchukua mzigo kwa supplier mmoja a ukapewa mzigo wa 20-30m, sio vitu vyote kwenye hardware vinalipiwa cash, mfano baadhi ya mabati rangi nabaadhi yavitu vingine unaweza kuvipata bila kulipia kwajumla inategemea namakubaliano yako nasupplier. Kitu ambacho huwezi kukopeshwa ni gypsum, cement nabaadhi yavitu vingine
Una uzoefu mkuu..hongera
 
Back
Top Bottom