Kipanya: Kulikoni tena!

Kibonzo hicho kinaweza kuwa na maana nyingi, lakini kwa ujumla kinachora picha ya hali ya kisiasa nchini Tanzania, hasa kati ya vyama vya CCM na Chadema.

Mtu aliyechimba kaburi na kuingia humo akichota maji anaweza kuashiria juhudi za kuondoa matatizo au changamoto zilizopo, lakini pia kuna uwezekano wa kuwa anajitafutia matatizo zaidi kwa kujiingiza katika hatari.

Hali hii inaweza kutafsiriwa kama juhudi za kuleta mabadiliko katika mazingira magumu.

Kwa upande mwingine, mwanachama wa CCM anayelala pembeni anaweza kuashiria utepetevu au kutokujali hali iliyopo, ambayo inaweza kuwa ni kielelezo cha watu walio katika madaraka kutokuwa na hamu ya kushughulikia matatizo ya wananchi.

Katika muktadha wa kauli za "no reform, no elections" kutoka kwa Chadema na wengine wanaosema kuna uchaguzi, kibonzo hicho kinaweza kuwakilisha mgawanyiko wa mawazo kwenye chama.

Wengine wanataka mabadiliko ya kweli kabla ya uchaguzi, huku wengine wakiona uchaguzi kama njia ya kuleta mabadiliko, bila kujali mfumo wa kisasa.

Hivyo, kibonzo hiki kinaweza kuwa kielelezo cha mgawanyiko wa mawazo na hisia kuhusu mwelekeo wa kisiasa na hali ya demokrasia nchini Tanzania.
 
Nyumbu wamejiingiza kwenye shida kweli kweli ya kiakili.......hawana jingine wanalowaza zaidi ya unyumbu wao. Poleni.
 
Kila mtu anatafsi yake!
KIjani baada ya kupandikiza G55 wanajaribu tena kusafisha kaburi kuona kama wanaweza kuizika Khak!
 
Ingependeza hayo maji angekuwa anayachota na kikombe.
 
Itapendeza ukitoa tafsiri yako
Tafsiri yangu ni, wenye nguo za kijani mbinu yao si maiti iisubiri kaburi, ni kaburi lisubiri maiti. Meaning makaburi yao wanayachimba mapema halafu yanakaa wazi yakisubiri maiti.

Sasa mhusika yu mahututi, kaburi linapaswa kuwa wazi tayari kwa kupokea maiti, mchimbaji anayaondoa maji na anafurahia hiyo hali sababu alijiandaa mapema kwa kichimba kaburi, kuchimba ni kugumu kuliko kuondoa maji.

Mhusika asipofariki, kaburi litabaki wazi likiendelea kusubiri.
 
Shukrani bwana Kipanya, ila michoro yako inakuwaga migumu sn kuitafsiri, kwnn?
 
Hii ni series Ndefu sana Faana
Yaani inabidi Ucheze na Matukio yote..

Ilianza Hivi..


Ikaja Hivi..


Ikaja Kuwa Hivi..


Ikafikia Huku

Sasa Imefika Huku



Maana Yake walichokiandaa Mwanzoni Kilielekea Kusua sua ila kwa Sasa Kinaelekea Kukamilika na Ndo maana Anatoa Maji kujiandaa
 
Hii Ni Tafsiri Yangu Kwa leo imeenda Na Matukio Yote
 
Unganisha dots uchaguzi ndani ya CDM na hili kundi jipya la waasi wa G55 ndani ya CDM. Hilo shati ni jezi ya CCM maana yake anayesuka mipango yote ya kuidhoofisha CDM ni CCM japokuwa ule uliosukwa kipindi cha uchaguzi ulifeli. Je, safari hii huu mkakati CCM waliokuja nao wa kuanzisha waasi wa G55 ndani ya CDM utafaulu? Ndio maana jamaa anatoa hayo maji huko shimoni akitegemea chochote kitaikumba CDM.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…