Balantanda
JF-Expert Member
- Jul 13, 2008
- 12,476
- 4,757
Kwani mkuu wewe hili hauliangalii kwa mboni za kisiasa?...Hauoni kama uliyoaandika kwenye bandiko hili ni siasa tupu....Bandiko la kisiasa lazima lijadiliwe kwa mtazamo wa kisiasa Chifu...Sijui ni kwanini watu wanaangalia kila jambo kwa mboni za kisiasa badala ya masilahi mapana ya nchi.
Jambo zuri rekodi zipo hivyo wengine tunapozungumza tuna uhakika
Hatuhitaji kufanya makosa yale yale kwasababu tu wapo wanaofanya makosa hayo hayo
Hii ni dhana mbovu sana
Huyu bwana alisimama kupinga ukuu wa Wilaya, leo anarudi kuwaambia watu wale wale, taswira yake kama kiongozi inakuwa wapi?
Lakini pia lazima tujifunze kwa viongozi wetu waliotangulia. Wapo walioacha masialhi yao binafsi kutetea nchi. Hata kama ni wachache, hatupaswi kuishi kwa historia yao tu, ni wakati tujenge historia ya kizazi hiki. Je, haya ndiyo tunatarajia kwa vijana kama hawa?
Lakini pia mteule alienda mbali, si kwa ukuu wa Wilaya, alifikia mahali anapotosha umma, anazungumza uongo usiohitaji certificate.
Leo kazawadiwa kwasababu hiyo tu! Tunajenga nchi kweli?
Tukianza kutetea haya, ipo siku watu watateua wajomba zao, nao watasema wanaweza kufanya nao kazi vizuri, kuna shida gani!!
Hebu tuangalie nchi kwa upana wake. Nipo katika rekodi nikipinga nafasi za ukuu wa wilaya. Ninapoona ukuu huo unatolewa kwasababu tu fulani anapepeta sana , inatia shaka
Kiongozi anateuliwa kwasababu alimtwanga mzee fulani katika kongamano!
Ndio tunahitaji hayao?
Halafu tukisema lipo tatizo, wapo wanaosema mbona Mrema naye alitwangwa kule Tanga? ina make sense kweli
Amepatikana mwenye chongo katika jamii ya vipofu hivyo nyie vipofu lazima mshangilie ili hali nae ana chongo!Unamsema mr liabilty alipohamia chadema akalazimisha watu wake wawepo kwenye nafasi za ubunge na viti maalum
CC: Barafu ya motoAmepatikana mwenye chongo katika jamii ya vipofu hivyo nyie vipofu lazima mshangilie ili hali nae ana chongo!
Weka akiba ya maneno kamandaAmepatikana mwenye chongo katika jamii ya vipofu hivyo nyie vipofu lazima mshangilie ili hali nae ana chongo!
Ukiona kiongozi yeyote chini ya jua anachagua viongozi au watendaji kwa kulipa fadhila bila Kuangalia utendaji wa mtu jua kuna kasoro hapo na usitegemee jipya! Huwezi jaza watu wa propaganda kwenye uongozi utegemee UTENDAJI!
Mkuu,yanaendelea kutimia!Polepole Mkuu wa wilaya.
Sasa picha hili limekuwa rasimi!Picha ndio kwanza limeanza
Kuna aliyekuwa mgombea aliahidi hadi vyeo katika idara nyeti za serikali kwa watakaomfanikisha kuingia magogoni.Je,ikitokea anapatikana kiongozi wa aina hii katika jamii yako,utaaridhika nae na kumwamini?
Mtu wa aina hii ana mapenzi na watu wake au ana mapenzi tu na baadhi ya watu?
Kipimo kizuri cha kiongozi huwa ni muda hivyo ni busara kuweka akiba ya maneno pale unapopata kiongozi mpya katika jamii yako.
Ni ushauri tu.