Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 54,015
- 43,157
Wanakumbi.
Kiongozi mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, ametoa ujumbe wake wa kwanza wa njia ya video tangu Marekani iliposhambulia nchi yake na Iran kusitisha mapigano na Israel.
Habari za kutolewa kwa ujumbe huo zilianza kumiminika kupitia mitandao ya kijamii na vyombo vya habari vya serikali ya Iran, kabla ya ujumbe wake kutangazwa kwa ukamilifu saa nane na dakika 35 swa na saa saa za ndani (7:35 kwa saa za Afrika ya Mahsariki).
Haya ndio yamejiri kuhusu hotuba yake:
Katika hotuba iliyotangazwa na runinga ya serikali Khamenei anasema "hakuna jambo la maana" lililotokea kwenye maeneo ya nyuklia yaliyopigwa na Marekani mapema wiki hii, matamshi ambayo yanapinga moja kwa moja matamshi ya Rais wa Marekani Donald Trump kwamba mpango wa nyuklia wa Iran "umefutwa"
Kiongozi wa Iran anasema nchi yake ilionyesha umoja wake, na kutuma ujumbe kwamba "watu wetu ni sauti moja"
Khamenei anasema Trump aliitaka nchi yake "kujisalimisha" lakini maoni yake yalikuwa "makubwa sana kutolewa kwa mdomo" wa rais wa Marekani
"Kwa nchi kubwa na taifa kama Iran, kusema ijisalimishe ni tusi," anaongeza
Kiongozi wa Iran pia alitishia kufanya mashambulizi zaidi katika kambi za Marekani katika eneo na kuongeza: "Iwapo shambulio litatokea, gharama kwa adui na mchokozi itakuwa kubwa."
Hapo awali, katika machapisho yaliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, Khamenei alisema Iran "iliipiga kofi zito usoni mwa Marekani" katika shambulio lake katika kambi ya Marekani nchini Qatar. Hakukuwa na majeruhi kutokana na shambulio hili
Pia alitoa pongezi mara kwa mara kwa kile alichokitaja kuwa ni "ushindi" wa nchi yake dhidi ya Israel
Maoni yake yanakuja siku mbili baada ya usitishaji mapigano uliomaliza vita vya siku 12 kati ya Iran na Israel. Mashambulizi ya Israel dhidi ya Iran yamewauwa takriban raia 627, kulingana na wizara ya afya ya Tehran. Mashambulizi ya Iran dhidi ya Israel yaliwaua watu 28, kama ilivyoripotiwa.
SOURCE 👇🏽
Iran would respond to any future U.S. attack by striking American military bases in the Middle East, Supreme Leader Ayatollah Ali Khamenei said on Thursday Source: The Citizen Supreme leader, in first appearance since ceasefire, says Iran would strike back if attacked
Kiongozi mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, ametoa ujumbe wake wa kwanza wa njia ya video tangu Marekani iliposhambulia nchi yake na Iran kusitisha mapigano na Israel.
Habari za kutolewa kwa ujumbe huo zilianza kumiminika kupitia mitandao ya kijamii na vyombo vya habari vya serikali ya Iran, kabla ya ujumbe wake kutangazwa kwa ukamilifu saa nane na dakika 35 swa na saa saa za ndani (7:35 kwa saa za Afrika ya Mahsariki).
Haya ndio yamejiri kuhusu hotuba yake:
Katika hotuba iliyotangazwa na runinga ya serikali Khamenei anasema "hakuna jambo la maana" lililotokea kwenye maeneo ya nyuklia yaliyopigwa na Marekani mapema wiki hii, matamshi ambayo yanapinga moja kwa moja matamshi ya Rais wa Marekani Donald Trump kwamba mpango wa nyuklia wa Iran "umefutwa"
Kiongozi wa Iran anasema nchi yake ilionyesha umoja wake, na kutuma ujumbe kwamba "watu wetu ni sauti moja"
Khamenei anasema Trump aliitaka nchi yake "kujisalimisha" lakini maoni yake yalikuwa "makubwa sana kutolewa kwa mdomo" wa rais wa Marekani
"Kwa nchi kubwa na taifa kama Iran, kusema ijisalimishe ni tusi," anaongeza
Kiongozi wa Iran pia alitishia kufanya mashambulizi zaidi katika kambi za Marekani katika eneo na kuongeza: "Iwapo shambulio litatokea, gharama kwa adui na mchokozi itakuwa kubwa."
Hapo awali, katika machapisho yaliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, Khamenei alisema Iran "iliipiga kofi zito usoni mwa Marekani" katika shambulio lake katika kambi ya Marekani nchini Qatar. Hakukuwa na majeruhi kutokana na shambulio hili
Pia alitoa pongezi mara kwa mara kwa kile alichokitaja kuwa ni "ushindi" wa nchi yake dhidi ya Israel
Maoni yake yanakuja siku mbili baada ya usitishaji mapigano uliomaliza vita vya siku 12 kati ya Iran na Israel. Mashambulizi ya Israel dhidi ya Iran yamewauwa takriban raia 627, kulingana na wizara ya afya ya Tehran. Mashambulizi ya Iran dhidi ya Israel yaliwaua watu 28, kama ilivyoripotiwa.
SOURCE 👇🏽
Iran would respond to any future U.S. attack by striking American military bases in the Middle East, Supreme Leader Ayatollah Ali Khamenei said on Thursday Source: The Citizen Supreme leader, in first appearance since ceasefire, says Iran would strike back if attacked