Kingunge

Kingunge

Nimeangalia taarifa ya habari ITV mzee Kingunge anatoa ya moyoni. Kama kweli huyu mzee anaongea kama mwana ccm, basi hakuna tofauti kati ya CCM na UKAWA kwa sasa

Mzee amefunguka sasa wafanye maamuzi bila kuchelewa,mtu akikuaibisha amekuaibisha tu usipochukua maamuzi inakula kwako jumla.
 
Ile stendi ya ubungo bado iko chini ya familia yake? Yeye hakuona kanuni kukiukwa alipokuwa anajipatia zaidi ya Sh milioni tatu faida ya chee kwa siku kwenye taasisi ya serikali, wakati wengine wanakosa huduma hata ya madawa muhimu.

Bila ya shaka alikuwa hata kodi halipi.

Na hiyo tenda ya parking jee bado anayo? Inakuwaje yeye anapata tenda mbili wenzake zero?
 
Anachokitafuta anakijua lakini? maana umaarufu anao toka zamani sasa ajiangalie.........

Kunyang'anywa ulaji UBT basi imekuwa nongwa! Yaani endapo mgombea unayemuunga mkono hakupita basi mchakato ni batili? Ana maslahi gani katika ugombea wa ENL?

Jana kuna mwanaJF mmoja alitupa msemo "A good decision is made on knowledge, not numbers" (by Plato). Alitaka CCM wafanye maamuzi kwa kufuata namba au kwa mfumo wa wengi wape wachache wanyime? Haya anayofanya KNM ni ishara ya ubinafsi uliokithiri na falsafa ya ufashisti ya "My way or no way"
 
Huyu mzee kibogoyo ni mnafiki sana hivi wakati wa issue ya Richmond huyu mzee alikuwa wapi? mbona hakumtetea Lowassa wakati huo ? Kama yeye anjiona ni kada mwanzilishi wa CCM mbona hayo mengine mengi anayafungia macho? Mfano sijasikia hata siku moja akikemea issue za Richmond, EPA, Kgoda na mengine mengi.Yaani ameona issue ni Lowassa tu why??? Nafikiri hapa ana personal iterests kutolewa Ubungo bus terminal nafikiri ndo sababu kubwa namshauri akelee vijukuu vyake. Shame on you mzee Kingunge.
 
Back
Top Bottom