Kingunge Ngombale Mwiru

WanaJF, kuna huyu mzee Kingunge Ngombale Mwiru ambaye amekuwa mtu muhimu sana katika siasa na sera mbali mbali za Tanzanai tangu enzi za Mwalimu Nyerere mpaka sasa. Huyu mtu alijulikana kama kichwa kilichokuwa nyuma ya Nyerere kuhusu uanzishaji na uendelezaji wa siasa na sera za Ujamaa hapa nchini.

Hakuwa mjamaa tu bali alikuwa Mkomunisti. Alikuwa na bado ni mtaalam wa Propaganda wa CCM. Hakuwa anamwamini Mungu. Katika ulaji wa viapo vya ofisi yeye alikuwa hatumii Biblia wala Quran.

Kwa hiyo mambo mengi yaliyoleta hadha kubwa enzi za Nyerere kama vijiji vya ujamaa inawezekana yalitokana na ushawishi wa Kingunge. Leo hii inashangaza yeye bado ni mshauri mkuu wa Kikwete kisiasa katika enzi hizi za Ubepari kubuhu na ufisadi.

Familia yake (mke na watoto) wanahusishwa na mikataba tata kama ule wa Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo. Tunapoangalia nyuma na kuangalia kwa macho mapaya huko tulikotoka naomba tumjadili huyu mzee, hasa wale wanaomfahamu kwa karibu.

Na kwa kuwa yeye bado yuko hai basi atapata nafasi ya kuelezea au kukosoa yale yanayosemwa. Tusingoje afe halafu ndiyo tuanze kumsifia au kumkosoa. Nawakilisha.

Binafsi namwona Kingunge kama mnafiki wa wanafiki. Mzee huyu alifaulu vyema kumzuga Nyerere kama vile alikuwa mtetezi shupavu wa ujamaa kumbe alikuwa kinyume chake! Mzee huyu hana msimamo na ni kielelezo cha wanafiki wanaowazunguuka viongozi wetu wakijifanya wanasimamia yale yanayosimamiwa na viongozi kumbe ni wasaliti wakubwa. Binafsi mwanasiasa huyu alinivutia sana miaka ya sabini kama mtetezi wa kweli wa ujamaa na wanyonge wa Tanzania. Vijana wengi wasomi wa miaka hiyo tulimwona mmojawapo kati ya vijana shupavu wa Nyerere. Lakini yaliyojitokeza baada ya kifo cha Mwalimu yamedhihirisha wazi unafiki wake! Aliyekuwa mtetezi shupavu wa Ujamaa sasa kageuka kuwa si mtetezi shupavu wa ubepari na unyonyaji tu bali pia fisadi mkubwa! katika jarida moja lililotoka miaka ya mwanzo ya sabini la "Towards Socialism" ambalo ndani yake kulikuwa na wachangiaji kadhaa Mzee huyu aliwasilisha mada iliyotuhamasisha wengi kama mimi. Nitanukuu kipengele kimoja tu muuone unafiki wa Mzee huyu leo hii, akijadili juu ya maslahi ya wabunge alisema " Katiba yetu inasema waziwazi kwamba mbunge atatokana na au mkulima au mfanyakazi, lakini hali ilivyo sasa mtu akishachaguliwa katika nafasi hii (ya ubunge) anakoma kuwa mkulima au mfanyakazi. Maana kipato chake cha mwezi kinakuwa sawa na kipato cha mkulima au mfanyakazi cha zaidi ya mwaka mzima!" Swali ni kwamba bado anasimamia alichokitetea miaka ya 70 hadi kuonekana mtetezi shupavu wa ujamaa au amebadilika? Na swali jingine ni Nyerere aliufahamu unafiki wake huo?
 
Kingunge ngombale mwilu au kwa jina lake la kikatoliki Joseph. Huyu mtu baba yake pale kilwa kipatimu aanaheshimika sana kwa kueneza dini ya kikatoliki. Baba yake mzazi alikuwa anatembea maili 45 na sacrament kichwani huku mvua inanyesha kwenda vigangoni kufanya ibada. Anaweza akaondoka saa mbili asubuhi nyumbani na akarudi saa tatu usiku kwa miguu au wakati mwingine akiwa na baiskeri. alikuwa hajali mvua au jua kali. Alijenga makanisa mengi sana vijijini . Yaani mzee ngombale kwake ukatoliki ulikuwa kama kazaliwa nao.

Sasa wewe hebu fikiria, mzee kama huyo leo asikie mwanae kamkana mungu kwa sababu ya kupenda siasa, kweli atampa baraka? Si atasononeka jamani. Ndio maana ukiangalia career yake katika uongozi ipo na mikosi mikosi tuu. mara nyerere kamtosa! Mara wananchi wanamchukia, mara mwane kaua. Yaani kwa ushauri wa bure, kingunge asione haya kurudia kanisa katoliki lililomlea utotoni kwa heshima ya baba yake.

Kingunge, please, you need to change your thinking before you change your living! Watu bilion sita duniani waseme kuna mungu, yeye aseme hakuna mungu! Is that fair the devil to guide his steps instead of God of Abraham?
 
Mengine tunamsingizia Mungu. Yaani hata kufanya wizi pale ubungo bus terminal ni kwa sababu ya kumuasi baba yake?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom