Kinana, Nape mmekubali kushindwa Arusha Mjini

Kinana, Nape mmekubali kushindwa Arusha Mjini

DALLAI LAMA

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2012
Posts
8,652
Reaction score
2,642
Wanabodi.

Tarehe 13 jumapili kura zinachukua nafasi hapa Arusha huku mgombea wa ccm Philemon Mollel akiachwa pekee hata kampeni hajafanya kisawasawa.

Arusha Mjini hatujamuona katibu mkuu wa chama Kinana wala Magufuli wala kikwete hata Nape.

Hesabu za haraka haraka hazisomi kwa mgombea wa ccm kwani wapiga kura wengi hawakuona juhudi zake.

Kinana na Nape mbona mmemtelekeza mgombea wenu kwa kutokuonekana wala kutuma rasilimali fedha?
 
Wanajua matokeo ndio maana hawakujishughulisha
 
wamefanya kitu cha busara sana sana maana hakuna namna ccm inaweza kushinda Arusha
 
Hivi jana Kinana aliingia mitini?? Maana magari yalikuwa yana sema Kinana angekuwa Arusha kuhitimisha kampeni za Ccm.
 
Kwn hizo fedha za kumsaidia mgombea wao wameshindwa kuzifanyia kazi nyingine hats wenyewe wanajua km arusha ni ngome ya ukawa,ndio maana hawataki kujishughulisha waswahili wanasema silence means yes
 
Sasa uko yupo lowassa unazani kinana au viongozi ccm wasinge tia miguu wao niwaelawa wameona ngoma ngumu awezi kung'oa
 
Wewe kinana yupo arusha na magufuli na kikwete wapo wote wamejichimbia mahotelini ila Kwa Lema mwaka huu watatoka damu manake Lema ni machame moja hakatwi mtu
 
Kwa Arusha hata kama wangempeleka Magufuli isingesaidia.
 
wanabodi.

Tarehe 13 jumapili kura zinachukua nafasi hapa arusha huku mgombea wa ccm philemon mollel akiachwa pekee hata kampeni hajafanya kisawasawa.

Arusha mjini hatujamuona katibu mkuu wa chama kinana wala magufuli wala kikwete hata nape.

Hesabu za haraka haraka hazisomi kwa mgombea wa ccm kwani wapiga kura wengi hawakuona juhudi zake.

Kinana na nape mbona mmemtelekeza mgombea wenu kwa kutokuonekana wala kutuma rasilimali fedha?

ccm hatutaki hata kuisikia huku
 
Lkn mwigulu si alikuwepo???????

Hata ule uchaguzi mdogo wa madiwani Mwigulu alikuwepo, huyu huwa hana aibu kwani amezoea kushindwa kwani kiuhalisia hasingekuja huko kwani kipindi kile aligongwa 4-0
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom