Kinana awasili Nyakanazi - Kagera, apata mapokezi makubwa na afanya kikao na Wafugaji

security guard

JF-Expert Member
Sep 27, 2011
799
603

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Katibu wa CCM mkoa wa Kagera Ndugu Idd Ame wakati wa mapokezi katika mkoa wa Kagera.



Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kagera Costansia Buhiye mara baada ya kuwasili Nyakanazi mkoani Kagera ikiwa siku ya kwanza ya ziara yake ya siku 10 katika mkoa wa Kagera.



Katibu Mkuu wa CCM akisalimiana na wakazi wa Nyakanazi mkoani Kagera.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akiwa amembeba mtoto Aloyce Atukuzwe wakati wa kusalimia wananchi wa Nyakanazi mkoani Kagera.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Nyakanazi waliojitokeza kumpokea ambapo anategemewa kuwa na ziara ya siku 10 mkoani Kagera.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Abdulrahaman Kinana amewasili katika Kijiji cha Nyakanazi wilayani Biharamulo Mkoani Kagera ambapo amepata mapokezi makubwa kijijini hapo ambapo mamia ya Wananchi walijitokeza katika uwanja wa shule ya msingi Nyakanazi.

Katibu Mkuu aliwahutubia wananchi na kuwaeleza lengo la ziara yake kuwa ni kuhimiza hatua za utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya 2010 - 2015, kukagua uimara wa Chama pamoja na kuhimiza wananchi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapigakura na kuwaandaa wanachama wa CCM na watendaji katika kuelekea uchaguzi mkuu wa oktoba mwaka huu.

Pia, Katibu Mkuu amefanya mazungumzo na uongozi na wanachama wa chama cha wafugaji Mkoa wa Kagera, ambapo wamemueleza changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo katika shughuli zao za ufugaji ambapo wamedai kuwa hifadhi ya pori na askari wa wanyamapori wanawatesa na kuwanyanyasa. Katibu Mkuu anaendelea na Kikao hicho aitaka Serikali kurudisha mifugo iliyokamatwa kwa wananchi na kisha yafanyike mazungumzo baina ya Serikali na Wafugaji hao ili kupata suluhu ya kudumu ya tatizo la malisho na maji kwa wanyama na wafugaji na baada ya hapo ataelekea Biharamulo na kisha wilayani Bukoba tayari kuanza ziara yake ya siku 28 Mkoani Kagera, Geita na Mwanza.


 
Pia, Katibu Mkuu amefanya mazungumzo na uongozi na wanachama wa chama cha wafugaji Mkoa wa Kagera, ambapo wamemueleza changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo katika shughuli zao za ufugaji ambapo wamedai kuwa hifadhi ya pori na askari wa wanyamapori wanawatesa na kuwanyanyasa. Katibu Mkuu anaendelea na Kikao hicho aitaka Serikali kurudisha mifugo iliyokamatwa kwa wananchi na kisha yafanyike mazungumzo baina ya Serikali na Wafugaji hao ili kupata suluhu ya kudumu ya tatizo la malisho na maji kwa wanyama na wafugaji na baada ya hapo ataelekea Biharamulo na kisha wilayani Bukoba tayari kuanza ziara yake ya siku 28 Mkoani Kagera, Geita na Mwanza.

Wape tu Kimisi, Burigi na Kasindaga kama wanavyotaka, halafu tuone walima kahawa wa Karagwe utawaambia nini maana mapori hayo yakishaharibiwa, mvua karagwe kwaheri
 
Wengi wao huko ni Warundi, maana hawa ndg zetu wa kwa nkulunzinza hata mke na mume wakipishana lugha mbio Tanzania.
 
Wape tu Kimisi, Burigi na Kasindaga kama wanavyotaka, halafu tuone walima kahawa wa Karagwe utawaambia nini maana mapori hayo yakishaharibiwa, mvua karagwe kwaheri

Mimi ningemshauri Mh.Kinana kupuuzia wafugaji wanao hamisha mifugo yao ovyo ovyo na kwenda kuvamia mapori ya Wananchi wanao jali kutunza mazingira yao, kwanini Serikali haiwakemei wafugaji wanao haribu mazingira kwenye mikoa wanayo toka wanakata miti eti kufukuza mbung'o mikoa yao ikiwa jangwa hawakumbuki kupanda miti badala yake wanakimbilia kuvamia mikoa mingine na kuendeleza uharibifu wao - kwa nini hawafugi kitaalamu zaidi kuliko kuwa na lundo la ng'ombe - mbona wakati wa enzi za Kambarage walikuwa hawana ubavu wa kufanya wapendalo kutokana na jeuri ya PESA sasa hivi wanajiona wapo juu ya sheria na viongozi wa chini wanawavumilia tu!!!!

Wanasema wao ni matajiri lakini wanashindwa kujenga majosho ya ngombe wao wanategemea Serikali iwachimbie - wanaleta vurugu tu Taifa zima na wanafanya wapendalo na malalamiko yasiyo kuwa na mantiki. Nisieleweke vibaya lakini Ndugu Kinanana ajaribu kuwapa somo wafugaji wanao hama hama ovyo ovyo wahachane na tabia yao yakufanya watu wasielewane, ikibidi Serikali igalimie baadhi ya wafugaji wakorofi waende Merikani, Ulaya, Argentina au Brazil kujifunza jinsi wafugaji wenzao wanavyo fuga ng'ombe wao, bila Serikali yetu Tukufu kuwa na msimamo thabiti na kuwaeleza ukweli wafugaji wakorofi basi Taifa letu linaweza kujikuta linaingizwa kwenye migogoro hisiyo kuwa na kichwa wala miguu. Mungu ibariki TANZANIA.
 
13.jpg


Kama naanza kumkubali Nape na hule msemo wake maarufu ukitaka kua Panya unainamisha Mtungi akitoka ua haaa haaa.Hapana sababu ya kuvunja mtungi nadhani ndio kazi inayoenda kufanywa na Kinana na Nape.
 
So wameanza kutembea na basi ili wapate gia ya kupiga kampeni stendi za mabasi kijanja au? Na anafanya kikao na wafugaji km nani? Na kwa nini iwe muda huu?
 
Ifike wakati watu wanaoishangilia ccm wajiulize wanatofauti gani na MTU mwenge HIV then anasambaza kwa wengine. Ccm ni hatari jamani, nchi inakwisha.!
 
Bado kuna watu wajinga huko kumbe? Nikimuona mama yangu anakatika mbele ya viongozi hao, nasitisha msaada ili akaishi nao huko. Huu ni upuuzi kukata mauno mbele ya watu tena walio na mambo ya ajabu
 
Huo mgari wote huo watu wawili - Nape na KM - wa nini? Wanabebea mizigo gani humo ukanda wenyewe huo ulivyo na matukio ya kutisha.
 
Hivi hayo mabasi ndo fasion ya ccm? Maana 6 naye yuko na basi. Tutaona mengi.
 
ifike wakati watu wanaoishangilia ccm wajiulize wanatofauti gani na mtu mwenge hiv then anasambaza kwa wengine. Ccm ni hatari jamani, nchi inakwisha.!

hapo ndipo tunapojikwaa, hawa wanashngiliwa ndio hao hao tunatakiwa kuwashawishi warudi upande wa pili, ila atuwezi kuwashawishi kwa kuwakejeli namna hiyo bali ni kwa hoja na kumwonyesha tofauti yako na ccm,
 
Back
Top Bottom