iphone 18 promax
JF-Expert Member
- Nov 17, 2012
- 2,918
- 2,153
Hakuna Mwanaume Mkarimu tu burebure..Mwanaume mpole kama njiwa..Mwanaume very caring tu from nowhere..Mwanaume anayekusikiliza...Mwanaume anayekutafuta asubuhi hadi jioni kujua hali yako..Mwanaume anayehakikisha unasmile muda wote..Mwanaume anayejali na kukubembeleza ule chakula...Mwanaume anayejua hadi rangi ya chupi unazopenda,loh mashallah...Usicheze na Mwanaume anayewinda Kipochi manyoya kwa ustadi wa kunguru aliyeona kifaranga kinacheza peke yake....Yuko radhi afanye lolote kwa gharama yoyote ilimradi aweze kuchungulia hazina yako ya Taifa..
Muite hata saa 8 usiku mwambie ''Baby nna hamu ya Burger ya Vitunguu Swaumu'',wala hatalalamika,ataifuata hata Chalinze na atakuletea Bunju B..Sasa fanya kosa tu upanue kidooogo tuuu na kumpa tuzo za Grammy's kama Mwanaume bora wa mwaka uone shughuli..Utashangaa yule Mwanaume uliyeamini ni romantic amefariki lini..Hakuna rangi utaacha ona..Burger na Shopping zote zitafia pale Bandari ya Chumbe,Visiwa vya Pemba.
Ni heri ukosee Kutuma Salio la MPESA kwa mtu kuliko kuamini kuna Mwanaume aliye Too Sweet kwako wewe bila Sababu...