Orketeemi
JF-Expert Member
- Feb 12, 2013
- 5,523
- 14,198
kwanza niseme Takwimu na maelekezo waliyonayo chadema katika wilaya 3 nilizofika ni dhahiri ukawa haipo kwa ubinafsi tu wa chadema, tayari nccr na cuf wamekubaliana katika maeneo mengi , mfano Arusha mjini chadema hawataki ushirikiano wa ukawa, hapa serengeti katibu Chacha Antony anasema hata makubaliano hayatambui ! Na ni fake ! Wakati nccr wanataka vitongoji 2 tu kati ya 23 vya hapa mjini, cuf wanataka 6 tu na chadema watapata 14 , na kwa sasa chadema wana kiti 1 tu, cuf wana vitongoji 4, na nccr hawana ! Mie nafikiri ni muhimu sasa kwa CUF Na NCCR Kuendelea na ushirikiano na hawa tuwaachie watz watawahukumu ! Mbaya zaidi arusha hawataki ushirikiano, hapa serengeti wanataka waachiwe viti 21 pamoja na 3 kati ya 4 vya CUF ! Sitaki kubeza hatua za mazungumzo kwenye ngazi ya Taifa kuhusu kuokoa jahazi ila watz bado wanataka umoja ! NCCR na CUF Tutatosha hawo waachieni waweke mgombea kila mtaa, kijiji na kitongoji !