Kimei mpaka sasa ameanza vizuri Vunjo

SautiYaMnyonge

JF-Expert Member
May 13, 2018
439
742
Jimbo la Vunjo lilishuhudia mabadiliko ya mbunge aliyekuwepo Ndg James Mbatia ambaye alikataliwa na wananchi kwa sababu ya kuwatelekeza na kushindwa kuwasemea masuala yao ndani ya bunge.

Uchaguzi huo ulipelekea kupatikana kwa mbunge mwingine ambaye ni msomi, mchumi na mtaalam aliyebobea kwenye masuala ya kifedha Dkt Charles Stephen Kimei ambaye aliiongoza kwa mafanikio makubwa benki ya CRDB kutoka kuwa na tawi moja na kuiacha ikiwa na matawi zaidi ya 250 ndani na nje ya Tanzania kwa pamoja. Rekodi yake bora kwenye utendaji na masuala ya uongozi iliyoakisiwa na mafanikio makubwa kwenye benki ya CRDB na ushiriki wake kwenye maendeleo jimboni Vunjo pamoja na sera au ahadi zake wakati wa kampeni zilikuwa kichocheo cha yeye kuaminiwa na umma wa wananchi wa Vunjo.

Ikiwa ni takribani siku 100 tangu achaguliwe na kula kiapo kuwa Mbunge wa bunge la Tanzania Mhe Dkt Kimei amethibitisha kuwa wanavunjo walifanya chaguo sahihi kwani ametekeleza ahadi zake nyingi ikiwemo ya kusikiliza kero za ardhi, umeme na maji. Kubwa zaidi ni michango yake ndani ya bunge imekuwa ya viwango vya juu kwani imegusa mahitaji ya wananchi wa jimbo la Vunjo.

Siku sio nyingi aliahidi kuanza kuanzisha mfuko wa wajasiriamali au uwezeshaji wananchi ambao unalenga kutoa fursa kwa wanavunjo kujiajiri na kujipatia au kukuza kipato chao.

Hakika ameanza vizuri Mhe Mbunge Dkt Charles KIMEI.View attachment 1708094
IMG-20210208-WA0044.jpg
 
Mwmbie hilo zee listaafu liwaachie vijana nafasi.
Ile ndoto yake ya kutaka kuwa waziri wa fedha imekufa kibudu,wala asidhani Jiwe atamchagua mchaga mjanja kwenye hiyo nafasi ,atabaki na Muha wake
 
Mleta uzi umeanza kufatilia VIKAO VYA CCM (BUNGE) lini? Nani alikwambia kusemea kero (kupiga piga kelele ) kwa kutaja kero ndiyo kutatuliwa! Chato umewahi kusikia Mbunge wao anapiga piga kelele kusema kero, mbona bajeti inaenda tu kinyume hata na sheria za Bunge!
Kuna wabunge wapo humo na miaka yote wanapiga kelele kwa kusemea kero ila hakuna utatuzi, majimbo yao yana kero kubwa sana.

Kasome nyaraka za Bajeti kwanza ujue jinsi ni HEWA tupu katika utekelezaji. Kwa sasa utatuzi wa kero kwa majimbo ni HISANI ya Kinjekitile, yani anaamua yeye siyo maelekezo ya Wizara.

Hii nchi tulikuwa robbed from the very first day Kinjekitile anaapishwa kuwa Rais. Hakuna mambo tangible amefanya ya kugusa maisha ya watanzania (masikini ni almost 70%) zaidi ya kufanya walio chini yake wafanye mambo kwa HOFU na UCHAWA ili kumpendeza.

Hii nchi mkombozi ni sekta ya KILIMO tu, ila ndiyo kipo hoi kuliko sekta zote. Apatikane mtu mwenye akili ku-link sekta ya Kilimo na viwanda ambavyo vitakuwa ndiyo soko la kwanza la uhakika kwa mazao yetu. Huko ndiyo kuna almost 70% ya Watanzania ambao ndiyo mliwapora kura zao kwa nguvu, hawakuelewa mambo ya ndege na flyover kwa the past 5 years huku sekta yao ipo HOI kabisa.

CCM hata kama hawataki kung'oka madarakani, basi watu wa vetting watafute mtu ambaye anafaa kuwa RAIS wa nchi, siyo KUMSUKUMIZA mtu ambaye hakuwa hata na DHAMIRA wala NIA ya kuwa Rais.

We are the failed STATE.
 
Huyo mchaga wako mwambie anywe mbege. Nimetokea kuwachukia hawa viumbe kwa sababu walimbagua mke wangu majuzi alipoenda kuripoti kazi ya ualimu kisa kabila la Anko magu.


Wachaga wabaguzi sana, na mitano iliyopo mtapelekewa chuma hatari, 10 tena kinaachwa chombo nyoko kuzidi kilichopo kiendelee kuwalaza njaa. Maninaaaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom