Kimbia by Babuu (Langa Verse)

Kimbia by Babuu (Langa Verse)

Lyrics Master

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2016
Posts
482
Reaction score
681
Kimbia, Polisi maskani wakivamia
Wakikudandia, hakika hawatakuachia
Wakukute umetulia, au kipisi unamalizia
Au labda kuna mchizi tu ulikuja kumuulizia
Wanapoingia, nakushauri kimbia
Wakikudandia, ujue watakuharibia
Na kama huna mshiko, kukuacha ni ndoto
Watakupa kesi ya kukudaka na gunia la msokoto
Wakikumind kichizi wanakupa kesi ya chamoto
We kimbia, kimbia acha kusinzia
Maskani sio sehemu ya kuja kusikilizia
Ka wewe ni mchizi wa kitaani au wewe unakula jani
Unapokuja maskani usifikiri upo nyumbani
Maskani kama vitani, kuwa makini sio utani
Kama unaweka roho ubaoni au kama kidume unyagoni
Maskani hakuna ujirani, ukidandiwa peke yako usitaje ulikuwa na nani
We kimbia tu kimbia,polisi mshikaji nyumbani
Unapofika nae kituoni anakuacha kama hakuoni
Mwisho wa siku unajikuta viatu na mkanda ubaoni
Na wewe mwenyewe ndani.
 
Hii beat ya huu wimbo ni ya kibabe sana...

Binafsi naikubali verse ya langa sana

"Mabuti ya kijeshi uyaone mafupi mepesi yani toka nduki toka lesi"
Kabisa yani langa alifanya balaa Sana humo jinsi ya mdundo ulivyokuwa na mitambao yake ni habari nyingine.
 
Back
Top Bottom