Kuna jamaa Mmoja Wa Ghana aliwahi kusema Ukitaka kuwa masikini basi fanya hivi, Laumu kila kitu isipo kuwa wewe mwenyewe, Laumu mfumo mzima, Laumu Serikali, Laumu Mabenki kwa kukataa kukupa mkopo uanzishe biashara.
Hapa tutalaumu sana usiki na mchana but wewe mwenyewe chukua hatua huwezi kulaumu huku umekaa kweny keybord haiwezekani hata siku moja, Tuanapenda sana kulauma ila ukweli ni kwamba hata Serikali ifanye nini hakuna tutakacho weza.
Mfano: Migodi ya kule Kanda ya ziwa wanachukua mboga kutoka kenya za kuwalishiwa wafanya kazi wao. Si kwamba wana chuki na watanzania, no ni kwamba hakuna mwenye kuonyesha kuzalisha mboga za kiwango za kuwauzia, mtu unakuta ana mboga matuta matatu analaumu kwamba hapati soko,
Shoprite si kwamba walikuwa wanafanya makusudi kuagzia hadi Mchicha kutoka South, ni kwamba hakuna msambazaji wa uhakika Bongo wote usanii tupu unapewa contract unaanza kwenda kukusanya kwa wauzaji wengine ndo upelelek hilo haliwezekani.
Kuna soko kubwa sana la Matunda nje, But huwezi chuma matunda kwenye gunia upeleke Ulaya au Asia jamaa wanajali afya ni lazima wapime na waone kama yana kidhi ubora,
Ukienda kule Tanga kuna kipindi unakuta wanachuma machungwa mabichi na kuyababua na moto ili yaonekane yameiva kumbe hakuna,
Ni Lazima sisi wenyewe tuamke, tuwe wabunifu,tutafute masoko, tutafute partners wakufanya nao bioashara,