Kwa muda sasa serikali imekuwa ikiendesha mpango wa kilimo kwanza ikilenga kuinua kilimo nchini. katika kutekeleza hili serikali imekuwa na mpango wa kugawa pembejeo za kilimo kwa wakulima.
Binafsi nafikiri kwa hali ilivyo kwa sasa katika nchi yetu kwa maana ya kwamba kwa kilimo chetu tunaweza kujitosheleza kwa chakula pembejeo si si kipaumbele cha kwanza bali soko la mazao ndio kipaumbele cha kwanza.
Inasikitisha kuona wapo watanzania wanaozalisha matunda yanaozea mashambani, inasikitisha pale tunapokuwa tunasafiri katika mikoa tofauti unakuta mtu anauza ndoo ya nyanya shilingi 700, mazao ya chakula wakulima wakizalisha kidogo bei zinapanda wakizalisha sana bei zinashuka hivyo kuongeza kwake mavuno kunakuwa hakuna maana bali kipato chao kinabaki palepale.
Kwa wakulima hawa tujiulize wanataka nini ili kuongeza ukubwa wa mashamba yao au kuongeza tija, pengine tuwahoji wakulima wenyewe watueleze kama atalima msimu mmoja akapewa ruzuku bila soko na kutafutiwa soko la uhakika bila ruzuku kipi angependa kitangulie.
Mimi napendekeza serikali kwanza kulifanya mamlaka inayosimamia gala la taifa kuwa inanunua mazao ya aina zote kutoka kwa wakulima hasa ya chakula, pili kufungua mipaka yote kwa watu wanaopeleka chakula nje ya nchi wanunue kutoka magala ya taifa na chakula kiondolewe ushuru ili kiuzwe nchi za jirani bure, ile fedha anayopata mkulima kutokana na kuuza chakula nje ni faida tosha kwa serikali yetu.
Kwa matunda zipo taasisi kama tirdo ambazo zinafanya utafiti wa technolojia washilikiane na SIDO kuunda vikundi au kutafuta wajasiliamali wa kuwakopesha au kuwafundisha ili waanzishe viwanda vidogo vidogo vya kusindika matunda na mboga mboga katika maeneo yenye kuzalisha vitu hivi kwa wingi huku serikali ikipandisha kodi kwa bidhaa za aina hiyo zinazotoka nje ili kulinda soko la viwanda hivi vidogo na sio shirika kama SIDO linalosimamiwa na serikali kusimamia miradi ya kipuuzi kama bidhaa za mianzi, vikapu na mambo mengine ambayo tija yake ni ndogo sana katika uchumi wa jamii zetu.
Tatizo kuwa la wajasiriamali wa Tanzania ni packaging ambapo ukienda SIDO kwa sasa chupa moja ya ml 350 yenye ubora kama wa chupa za maji na juisi ni shilingi 400 sasa mjasiliamali anayeweza kukamua machungwa atauza shilingi ngapi kama chupa tupu bila lebel wala juisi ni 400. Serikali iwekeze katika SIDO kuweka viwanda vya bei nafuu vya kuwasaidia wajasiliamali katika packaging za plastiki, maboksi na mengine.
Wananchi maeneo mbalimbali wana utaaramu wa kutengeneza gongo, hawa tunawakamata na tunaagiza gongo kutoka nje sasa kwa nini tusitafute kiwanda cha kununua gongo kutoka kwa watu na kuisafisha na kuiweka katika chupa ili tujiuzie na tupeleke na sisi nje na hili ni soko mojawapo la mazao ya kilimo.
Wapo viongozi wasiofaa kuwa viongozi wanaodhani wakiwazuia wakulima kuuza nje, wakapiga marufuku ya bidhaa zinazotokana na mazao ya kilimo kama gongo mazao yakawa mengi bei zikashuka ndio wanakuwa wameongoza vizuri kwani mfumuko mwa bei umebaki chini kumbe hao ndio wanatakiwa kufungwa mawe ya kusagia shingoni na kutoswa baharini kutokana na kuwapatia wakulima umasikini huku wakisimama kwenye majukwaa na kulalamika kuwa kilimo chetu kimendelea kuwa cha jembe la mkono.
Mabadiliko ndani ya sekita ya kilimo yataletwa na wakulima wenyewe pale wanapowekewa mfumo mzuri wa soko mambo mengine ya pembejeo wao wenyewe wanaweza kuyamudu pale wanapokuwa wanalima kibishara zaidi.
Binafsi nafikiri kwa hali ilivyo kwa sasa katika nchi yetu kwa maana ya kwamba kwa kilimo chetu tunaweza kujitosheleza kwa chakula pembejeo si si kipaumbele cha kwanza bali soko la mazao ndio kipaumbele cha kwanza.
Inasikitisha kuona wapo watanzania wanaozalisha matunda yanaozea mashambani, inasikitisha pale tunapokuwa tunasafiri katika mikoa tofauti unakuta mtu anauza ndoo ya nyanya shilingi 700, mazao ya chakula wakulima wakizalisha kidogo bei zinapanda wakizalisha sana bei zinashuka hivyo kuongeza kwake mavuno kunakuwa hakuna maana bali kipato chao kinabaki palepale.
Kwa wakulima hawa tujiulize wanataka nini ili kuongeza ukubwa wa mashamba yao au kuongeza tija, pengine tuwahoji wakulima wenyewe watueleze kama atalima msimu mmoja akapewa ruzuku bila soko na kutafutiwa soko la uhakika bila ruzuku kipi angependa kitangulie.
Mimi napendekeza serikali kwanza kulifanya mamlaka inayosimamia gala la taifa kuwa inanunua mazao ya aina zote kutoka kwa wakulima hasa ya chakula, pili kufungua mipaka yote kwa watu wanaopeleka chakula nje ya nchi wanunue kutoka magala ya taifa na chakula kiondolewe ushuru ili kiuzwe nchi za jirani bure, ile fedha anayopata mkulima kutokana na kuuza chakula nje ni faida tosha kwa serikali yetu.
Kwa matunda zipo taasisi kama tirdo ambazo zinafanya utafiti wa technolojia washilikiane na SIDO kuunda vikundi au kutafuta wajasiliamali wa kuwakopesha au kuwafundisha ili waanzishe viwanda vidogo vidogo vya kusindika matunda na mboga mboga katika maeneo yenye kuzalisha vitu hivi kwa wingi huku serikali ikipandisha kodi kwa bidhaa za aina hiyo zinazotoka nje ili kulinda soko la viwanda hivi vidogo na sio shirika kama SIDO linalosimamiwa na serikali kusimamia miradi ya kipuuzi kama bidhaa za mianzi, vikapu na mambo mengine ambayo tija yake ni ndogo sana katika uchumi wa jamii zetu.
Tatizo kuwa la wajasiriamali wa Tanzania ni packaging ambapo ukienda SIDO kwa sasa chupa moja ya ml 350 yenye ubora kama wa chupa za maji na juisi ni shilingi 400 sasa mjasiliamali anayeweza kukamua machungwa atauza shilingi ngapi kama chupa tupu bila lebel wala juisi ni 400. Serikali iwekeze katika SIDO kuweka viwanda vya bei nafuu vya kuwasaidia wajasiliamali katika packaging za plastiki, maboksi na mengine.
Wananchi maeneo mbalimbali wana utaaramu wa kutengeneza gongo, hawa tunawakamata na tunaagiza gongo kutoka nje sasa kwa nini tusitafute kiwanda cha kununua gongo kutoka kwa watu na kuisafisha na kuiweka katika chupa ili tujiuzie na tupeleke na sisi nje na hili ni soko mojawapo la mazao ya kilimo.
Wapo viongozi wasiofaa kuwa viongozi wanaodhani wakiwazuia wakulima kuuza nje, wakapiga marufuku ya bidhaa zinazotokana na mazao ya kilimo kama gongo mazao yakawa mengi bei zikashuka ndio wanakuwa wameongoza vizuri kwani mfumuko mwa bei umebaki chini kumbe hao ndio wanatakiwa kufungwa mawe ya kusagia shingoni na kutoswa baharini kutokana na kuwapatia wakulima umasikini huku wakisimama kwenye majukwaa na kulalamika kuwa kilimo chetu kimendelea kuwa cha jembe la mkono.
Mabadiliko ndani ya sekita ya kilimo yataletwa na wakulima wenyewe pale wanapowekewa mfumo mzuri wa soko mambo mengine ya pembejeo wao wenyewe wanaweza kuyamudu pale wanapokuwa wanalima kibishara zaidi.