Kilimo cha pilipili

WADUDU
Pilipili hushambuliwa sana na vidukari ,mchwa nzi weupe na kadhalika.
Fanya palizi ya mapema kuondoa maficho ya wadudu hao
Tumia vuatilifu kulingana na mdudu aliye shambuliwa kuzinga tia ushauri wa Bwana shamba
MAGONJWA
Pilipili ina magonjwa kama ya Ukungu,Kuvu sawa na magonjwa mengine ya nyanya Tibu mmea kabla haijapata magonjwa kwa kufuata ushauri wa bwana shamba.
MAVUNO
Pilipili huvunwa kwa kuchuma na huanza kuvunwa baada ya miezi 2-3 baada ya kuitoa kwenye kitalu na
huvunwa kwa mfululizo wa Miezi 3 hadi 4 na inashauriwa kuvuna kila baada ya wiki mbili
Isivunwe pamoja na vikonyo vyake na isivunwe ile mbichi ya kijani vuna iliyoiva na iliyopitiliza kuiva isivunwe
MAPATO
Shamba lilitunzwa vizuri kwa kila hekari moja ia uwezo wa kutoa kilo 1000 hadi 3000 kutegemea na utunzaji
BEI YA PILIPILI SOKONI
leo tarehe 3-8-2016 inakadiriwa kuwa na bei ya shilingi 2500/-kwa kilo moja
UKAUSHAJI BAADA YA KUVUNA
Huchukua muda wa siku 3 hadi 4 kukauka na isianikwe kwenye jua kali au kwenye unyevunyevu chini ikapoteza ladha kwa kupigwa na jua na kota kuvu inatakiwe isambazwe juu ya kichanja kilicho inuliwa na kukauka taratibu sio kwa kurundikwa
Usiweke kwenye gunia za sandarusi weka kwenye gunia za katani au kikapu ukiweka kwnye sandarasi huchemka na kuharibu ladha ya pilipili.
CHANGA MOTO ZA UZALISHAJI
Uvunaji ndio changamoto kubwa wa kilimo cha pilipili usipande kiasi usichoweza kukivuna
Panda kiasi cha pilipili ambacho unaweza kupata vibarua wakutosha katika uvunaji
USHAURI KWA WANAOTAKA KULIMA
Ingia mkataba na mnunuzi kwanza kabla haujaaanza kulima ndipo ukishafunga mkataba ndipo anza kulima
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom