Kilimo Cha nyanya

Kati ya nyanya aina ya DHAHABU F1 na tanzanite ni ipi Ina sifa nzuri?
Mkuu dhahabu inazaa watoto wengi kuliko Tanzanite japo hazipishani sana. shida ya dhahabu chenga ni nyingi ukichuma mara moja tu zinabaki goroli kwa upande wa Tanzanite ipo vzr haina chenga mkuu labda mwisho kabisa.

Hivyo kwa upande wangu ningechagua tanzanite na ndo nililima mkuu pamoja na hiyo dhahabu
 
we ni chawa wa epinav? Dhahabu inazaa saana inahitaji maji mengi sana na mbolea ndio mana ni nyanya ya masika na haina chenga, tanzanite nayo sio mbaya ina shida bei sana na mbegu chache 5g unaweza pata mbegu 1000 wakati 5g dhahab unapata 2000 na zaid. Mleta mada unalima sehemu gani?
 
Ok,Vipi Lakini kuhusu uwezo wa kukaa muda mrefu baada ya mavuno bila kuharibika?Ni ipi ni zaidi?,Namaanisha ni ipi Ina shelf life kubwa?
 
Bado hujasema unalima wapi Dakawa, Dodoma?
Nalima wilayani Mufindi mkoa wa Iringa,Mimi ni mgeni katika kilimo Cha nyanya,nililima Kwa mara ya kwanza mwaka Jana,na nilipanda DHAHABU F1,mavuno hayakiwa mabaya sana Kwa mtizamo wangu,Hivyo nataka kujifunza kuhusu mbegu tofuti Bora zaidi ya DHAHABU ili kuongeza tija, Asante
 
Mkuu hebu nipeni uzoefu kidogo. Tukiachana na mambo ya bei za nyanya, ekari moja ya nyanya iliyotunzwa vizuri nikipanda mbegu hizi za F1 kama Imara. Naweza kuvuna tenga ngapi? Huku mashambani tenga moja ni ndoo 3.
Nataka kujua wastani hizo ndoo tatu zitatoka mara ngapi kwa ekari moja?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…