Miti inafaa sana kuwekeza japo yakupasa kuwa mvumilivu.
Wengi hawafanikiwi kutokana na sababu mbalimbali mfano,
1.kutokujua aina ya mti wa kupanda kulingana na aina ya udongo wa pahali husika
2. Kupanda miche iliyotokana na Mbegu hafifu aka zakuokoteza za cross pollination
3. Kutokujua muda sahihi wa kufanya silviculture management eg. Thining, pruning
4. Kukosa taarifa sahihi za Miti unayopanda ikiwa ni pamoja na kutumia data za zamani.
5. Kutokujua dhumuni mama la kupanda Mitiyako hapa kuna mengi sana ya kujifunza
Kwa sasa Miti nayoweza kushauri mtu kupanda ni pinus patula, cuprecesus lustanica, Cider/African black pencil sp, acacia and Teak.
Teak ni mti wa bei ya juu sana na huuzwa kulingana na current world market price mf. Mti 1 uliofikia rotation age unaweza kufikia 3m.
Teak imepandwa zaidi mkoa wa morogoro wilaya ya Ulanga kuna kampuni inaitwa KVTC
Soko la Miti hii zaidi ni nje ya nchi eg India, Canada, Vietnam & middle east
Kuna Miti yenye thamani zaidi mfano Mpingo /delbegia melanoxylon pterocarpus angolensis /Mninga pia kuna Melxia exelsa /mvule ina bei kubwa lakini inachukua muda zaidi kukua na kurudisha faida
Miti hii na mingine ina bei kubwa kwa sababu hutumika kutengenezea furniture za kifahari na mambo mengine mengi mfano kutengenezea meli, boat, na vitako vya bunduki.
Mkaa wa mti wa Mpingo una uwezo wa kutoboa ama kuyeyusha sufuria__--- has got very high calorific value however making charcoal from it could be termed as underutilization of resource!!!
Waweza kupata mkopo bank kutumia shamba lako lenye hati mililiki na miti ya teak