Kila ninavyoitafakari Mbingu

Huwa nafikiri mbinguni si huko juu tunakoangalia, ujue siku zote dunia inazunguka ulipokuwa Jana si ulipo Leo mkuu. Tuendelee kuamini, ila tusidadisi sana tutaziacha kabisa dini. Ni maoni tu
 
Unajua unaposema imani ni bayana ya mambo yasiyoonekana tayari ushatumialogic, kwa hiyo definition yakoya imani inatumia logic, na hivyo, ukisema kutaka kutumia logic kuthibitisha imani ni kufeli, wewe uliyeanza kui define imani kw alogic umeanza kufeli kabla yangu?

Unajua kwamba ninachotakakukithibitisha kwa logic si imani, imani unaweza kuamini chochote, bali ni imani ya kweli.

Kweli ndiyo inathibitishwa kwa logic,si imani.

Unaelewa tofauti?
 
Sayansi haichanganywi na dini, hakuna mahali sayansi inaelezea makazi huko angani ( universe)
 
kweli ni nini!!!
unatumia kigezo gani kusema kweli inathibitishwa na logic.
je kuna universally accepted definition ya kweli?
kwangu mimi kweli ni neno la Mungu.
 
kweli ni nini!!!
unatumia kigezo gani kusema kweli inathibitishwa na logic.
je kuna universally accepted definition ya kweli?
kwangu mimi kweli ni neno la Mungu.

Swali zuri.

Kweli ni kitu ambacho kinaweza kuelezewa bila ya kupatikana namna ya maelezo yake kujipinga (contradiction).

Mungu wako maelezo ya kuwepo kwake yanajipinga (the story of the existence of your God can be contradicted).

Hivyo, Mungu wako si wa kweli. Hayupo.

Kwa sababu maelezo ya kuwepo kwake yana contradiction.
 
Ee mungu nahitaji rehema zako siku moja niione mbingu
 
Nenda google "galaxies' Ndipo uweze kujua umbali toka hapa duniani mpaka kwenye galaxies. Na ukifika huko bado hujafika mbinguni. A human brain doesnt have the capacity to understand distances which are in terms of infinity
 
hiyo sio universally accepted maana ya kweli ni relative definition maana kwa mjadala huu maana yangu ya kweli ni tofauti.
Neno la Mungu ndio kweli.
kitu kudhaniwa kuwa kinajipinga wenda ni matokeo ya ufinyu wa muhusika kukielewa.
kwa maana yako hiyo mimi na wewe Tutaelewana at Infinity
 
Hata hiyo yako si universally accepted, so what is your point?

By the way, kitu kuwa universally accepted haimaanishi ni ukweli, na kitu kutokuwa universally accepted haimaanishi si kweli.
 
Kama ni kweli Yesu alipaa kuelekea juu mbinguni ambapo mashuhuda waliona kabisa kwa macho yao nadhani majibu kwa naswali ya mleta uzi yapo wazi tusiendelee kuumiza kichwa....!
 
Kwa mawazo yangu mbingu sio anga ila ni mahali popote. Utaniuliza popote wapi? Kupajua ni shida, ila siku mwili ukitengana na roho (kifo) utapajua. Ila yote hayo tumeletewa na wazungu, kama mwafrika zingatia jadi yako, Mungu wako unamjua mwenyewe
 
Usiumize kichwa.Kama unataka kufika mbinguni ishi maisha mema.

Tumia akili katika kufanikisha tanzania ya viwanda kuliko kutafakari mbingu.
 
Mkuu usiumize kichwa chako kutafuta mbinguni na alipo Mungu katika huu ulimwengu (universe) wetu. Mungu, mbingu, roho, peponi nk ni vitu vilivyopo kwenye ulimwengu wa kiroho na sio hii physical universe tunayoiona.

Kama unataka kujifunza anga letu na vitu tunavyoviona juu basi unaweza kuanza na uzi huu hapa chini ambako mimi pia nilichangia. Kuhusu somo la ulimwengu wa kiroho, tusubiri waliobobea. Hilo somo lipo nje ya uwezo wangu ( above my pay grade).

Kila la kheri.

Ufahamu kuhusu nyota za angani
 
mbinguni ni mahala halisi pa kugusika.
anga sio mbingu...
kwa waumini wa bibilia... wanaishi duniani kma wapangaji au wapitaji maana Yesu yuko anaandaa na kudesign maeneo ya wao kuishi milele

Kwa Mujibu wa Biblia wanadamu hawataishi mbinguni milele. Watakaa mbinguni kwa miaka 1000 tu. Baada ya hapo watarudi katika Dunia hii ikiwa mpya(Mungu ataiumba tena) tofauti na sasa. Then wataishi hapa duniani milele na milele ndani ya mji mtakatifu wa Yerusalemi, Mungu mwenyewe akiwa hapa hapa duniani. (See kitabu cha Ufunuo, sura za mwishoni)
 
Duuuh mnadanganywa km vichaa bhana
 
Halafu hivi huyu Yesu ni nani alimuona akipaa, au nani ana uthibitisho ya kuwa alitumwa kutuokoa, maana kama ndivo basi haina haja ya kwenda kuabudu maana tunasubiri tuu ukombozi wa Bwana Yesu.
Ule ni uongo mkuu wapo wanatudanganya danganya tu,inawezekana ukweli wa hatima yetu upo ila kuugundua ni shuhuri pevu
 
Mungu ameumba mazuri na mabaya ndio.Ila amempa mwanadamu utashi (intellect) ya kung'amua zuri lipi na baya lipi ili kuleta uwiano mzuri katika maisha.
Watakaochagua mabaya wataangamia na watakaochagua mema watadumu.In evolution tunaita natural selection in survival of the fittest.

Ila usinielewe vibaya.Sija kushurutisha kuamini mungu yupo kwa maana una uhuru wa kukata uwepo wa mungu.Hawa watu wanaitwa wapagani (atheists) na wana haki ya kufuata imani yao.
 
Ni bora ukaamini ili siku ya mwisho ata ikitokea yesu hayupo utakuwa haina cha kupoteza kuliko kutokuamini na mwisho ukakutana nae.
Alikuwa binadamu wa kawaida tu wala hastaabishi kwa chochote kwa nilivyofatilia stori yake,nyie mmemjua yesu akianza kuhubili wakt uo akiwa na miaka30 watu tupo tunamchipua nyuma uku toka miaka 6-na kuendelea alaf yesu alikua mweusi tii kama cc duniani tunafichana vingi sana asee siamini nayoyakuta.
 
WHO IS GOD?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…