nameless girl
JF-Expert Member
- Apr 22, 2012
- 4,195
- 2,685
Mnaendeleaje? 😛
Leo ninaomba tuongelee juu ya KILA MTU NA FUNGU LAKE.
Mara kwa mara nikipita kwenye jukwaa hili kunakuwa na mada nyingi sana tofautitofauti. Wengine wanaleta mada hizo kutokana na miemko fulani ambapo ninaamini kwa namna moja au nyingine zinawaathiri baadhi ya watu kwa namna moja au nyingine.
Mfano mtu anapokuja na mada ya "Kurudiana na ex ni ulimbukeni wa hali ya juu." Kuna watu ambao waliachana na sasa wapo kwenye ndoa na upendo mkubwa ukitawala.
Kuna mada kama "Kuoa single mother..." , "Kuoa bikra..." nakadhalika.
Hapa ndugu zangu tunapaswa kufahamu kuwa kila mmoja na FUNGU LAKE. Kwa kuwa mimi siwezi kurudiana na ex basi ipitishwe kuwa kurudiana na ex ni ujinga. Hii inatokana na kuwa maisha yangu mimi hayawezi kufanana na ya mtu mwingine.
Hakuna haja ya kusikitika au kujiona mnyonge kuwa umeoa mtu mwenye mtoto au asiye bikra. Huyo aliyeoa hivyo, hilo ndilo FUNGU LAKE.
Ni sawa na mama ambaye anawajua vema watoto wake. Anajua Mwajuma nikimpa hiki atakifurahia, Asha nikimpa kile, kitamsumbua nakadhalika.
Tufurahi tukiwa hai kwa kuheshimu MAFUNGU YA WATU.
Nawasilisha.
Leo ninaomba tuongelee juu ya KILA MTU NA FUNGU LAKE.
Mara kwa mara nikipita kwenye jukwaa hili kunakuwa na mada nyingi sana tofautitofauti. Wengine wanaleta mada hizo kutokana na miemko fulani ambapo ninaamini kwa namna moja au nyingine zinawaathiri baadhi ya watu kwa namna moja au nyingine.
Mfano mtu anapokuja na mada ya "Kurudiana na ex ni ulimbukeni wa hali ya juu." Kuna watu ambao waliachana na sasa wapo kwenye ndoa na upendo mkubwa ukitawala.
Kuna mada kama "Kuoa single mother..." , "Kuoa bikra..." nakadhalika.
Hapa ndugu zangu tunapaswa kufahamu kuwa kila mmoja na FUNGU LAKE. Kwa kuwa mimi siwezi kurudiana na ex basi ipitishwe kuwa kurudiana na ex ni ujinga. Hii inatokana na kuwa maisha yangu mimi hayawezi kufanana na ya mtu mwingine.
Hakuna haja ya kusikitika au kujiona mnyonge kuwa umeoa mtu mwenye mtoto au asiye bikra. Huyo aliyeoa hivyo, hilo ndilo FUNGU LAKE.
Ni sawa na mama ambaye anawajua vema watoto wake. Anajua Mwajuma nikimpa hiki atakifurahia, Asha nikimpa kile, kitamsumbua nakadhalika.
Tufurahi tukiwa hai kwa kuheshimu MAFUNGU YA WATU.
Nawasilisha.