Nina uhakika tutalalama mpaka atamaliza muda wake, atahakikisha mfuasi wake anampa pumziko lisilo na matatizo huku akifaidi mali alizochuma kwa miaka 10 kama siyo 30 akiwa kiongozi wa nchi hii wa aina moja au nyingine. Unajua atahakikisha vipi atakayechukua nafasi yake atampa pumziko la salama kama alomhakikishia aliyemrisisha kiti? Kwa kucheza na katiba, katika mchezo ambao ameuanza kwa kuteka nyara mswada wa katiba. Katiba itakayotengenezwa itamuwezesha mrithi wake kushinda uchaguzi ujao. Au yeye atagombea kwa mara ya tatu? Kama nimesoma mahala kwamba hilo nalo linaweza kutokea. Na usije ukashangaa Ridhiwani anaweza akawa raisi wa awamu ya tano kwa katiba hiyo hiyo itakayoongezewa kifungu kuwa mtoto kipenzi wa rais anaweza kurithi kiti cha baba.