BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,832
- 287,782
Kikwete aficha siri
na Charles Mullinda
Tanzania Daima
KATIKA hali ambayo haikutarajiwa na wengi, Rais Jakaya Kikwete, ameamua kuwa msiri katika utendaji kazi wake.
Hali hiyo ilidhihirika Alhamisi wiki hii wakati alipokutana na kuzungumza na wahariri wa vyombo vya habari, Ikulu, Dar es Salaam kuhusu maadhimisho ya kutimiza kwake miaka miwili akiwa madarakani.
Katika mkutano wake huo na wahariri, Rais Kikwete alisema taarifa zinazoelezwa kuwa ana mpango wa kufanya mabadiliko katika baraza lake la mawaziri ni uvumi usio na ukweli wowote, lakini atakaa chini na kuangalia iwapo kutakuwa na haja ya kupunguza au kuliacha baraza hilo likiwa katika muundo wake wa sasa.
Kauli hii ya Rais Kikwete inapingana na uhalisia wa mambo unaoonyesha kwamba kwa hali yoyote, na kwa kuzingatia staili yake ya utendaji kazi ya kurejesha matumaini kwa wananchi kuhusu uongozi wake na serikali yake kwa ujumla, atalazimika kulivunja baraza lake la mawaziri wakati wowote kuanzia sasa.
Ukweli huu unathibitishwa na hatua kadhaa ambazo Rais Kikwete amekuwa akizichukua tangu aliposhika madaraka, miaka miwili iliyopita katika kuhakikisha kuwa serikali yake inabaki na mvuto kama iliokuwa nao wakati akiingia madarakani.
Baadhi ya hatua zilizochukuliwa na Rais Kikwete ili kulinda hadhi ya serikali yake ni pamoja na kuunda tume ya kuchunguza mauaji ya wafanyabiashara watatu wa madini, wenyeji wa Mahenge, waliodaiwa kuuawa na polisi.
Kikwete aliunda tume hiyo baada ya malalamiko ya wananchi kuhusu taarifa iliyotolewa na polisi kuwa waliouawa walikuwa majambazi na si wafanyabiashara, jambo lililopingwa na wananchi na kulitia doa Jeshi la Polisi.
Katika hatua nyingine, Rais Kikwete alilazimika kuunda kamati ya kupitia upya mikataba ya madini, akiwajumuisha pia wabunge kutoka kambi ya upinzani, baada ya kuwepo kwa kelele nyingi kutoka kwa kambi ya upinzani, wanaharakati na baadhi ya wananchi kuhusu usiri uliogubika mikataba hiyo inayodaiwa kulitia hasara taifa, huku ikiwanufaisha zaidi wawekezaji.
Mwenendo huo wa Rais Kikwete, unaonyesha kuwa kamwe hataifumbia macho ripoti ya Utafiti wa Mpango wa Elimu ya Demokrasia (REDET) inayoeleza kuporomoka kwa umaarufu wake binafsi pamoja na ule wa serikali yake.
Ripoti hiyo ambayo yeye mwenye na hata baadhi ya wasaidizi wake wa karibu wameikubali, akiwemo mshauri wake wa masuala ya siasa, Kingunge Ngombale-Mwiru, ni moja ya mambo yatakayomlazimisha Rais Kikwete kufanya mabadiliko ya haraka katika baraza lake la mawaziri ili kurejesha umaarufu wake na serikali yake ambao umeelezwa kuporomoka kwa kiwango kikubwa katika ripoti hiyo ya REDET.
Aidha, hatua ya Rais Kikwete kukubaliana na ripoti hiyo na kutamka kwake kuwa anaangalia uwezekano wa kulipunguza au kuliacha kama lilivyo baraza lake la mawaziri, ni dalili kuwa ana tafakari kwa kina kuhusu mabadiliko atakayoyafanya, jambo ambalo limechelewesha hata kuteuliwa kwa mrithi wa kiti cha marehemu Salome Mbatia, aliyekuwa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.
Rais Kikwete ambaye utawala wake unaelekea kutimiza nusu ya muhula wake atasukumwa pia na kauli za watu mashuhuri, kama Paul Rupia, aliyepata kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais kwa miaka mingi, aliyekaririwa na vyombo vya habari akizungumzia kuhusu haja ya rais kuchukua hatua hiyo.
Pamoja na wadadisi wengi wa mambo kuona haja ya lazima ya kufanyika kwa mabadiliko ya mawaziri sasa, matukio mengine kadhaa ya hivi karibuni, mbali na ripoti ya Redet, yanatoa mwelekeo huo huo wa mambo kubadilika.
Matokeo ya uchaguzi wa ndani katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) ulioshuhudia kuondoka madarakani kwa baadhi ya viongozi waandamizi katika sekretarieti ya chama hicho ni moja ya mambo yanayoonekana kuwa sehemu ya sababu zitakazomfanya Kikwete alazimike kuchukua hatua hiyo ya kubadili mawaziri.
Baadhi ya watu wanaotajwa kuwa wanaweza wakaingia katika baraza hilo jipya ni pamoja na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Jaka Mwambi na mwenzake aliyekuwa akishikilia wadhifa wa Katibu wa Uenezi na Itikadi, Aggrey Mwanri, ambao wote waliachwa katika sekretarieti mpya.
Wanasiasa hao wawili ambao kuachwa kwao katika uongozi wa kisiasa hauhusishwi na kushindwa kwao kazi, wanapewa nafasi kubwa kutokana na ukaribu wa kihistoria wa kikazi waliojijengea kwa Kikwete kwa miaka mingi.
Wakati Mwambi akitajwa kuwa komredi wa miaka mingi wa Kikwete tangu miaka ya 1970, Mwanri yeye anapewa nafasi kubwa kutokana na uwezo wake binafsi na eneo anakotokea wilayani Hai, ambako wapinzani na hususan Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kina nguvu kubwa.
Mbali ya tukio hilo, tuhuma na kasoro zilizopata kuzikumba baadhi ya wizara kama ile ya Nishati na Madini, Afya na Ustawi wa Jamii na Maliasili na Utalii ni jambo jingine linaloonekana kuwapo kwa uwezekano wa mabadiliko hayo kutokea.
Matukio ya namna hii kwa mfano, ndiyo ambayo kwa sababu za wazi yanamweka Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, kushikwa na kihoro cha kuweza kukumbwa na mabadiliko hayo, lengo likiwa ni kuondoa kiwingu alichojengwa tangu Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, alipomuunganisha na utiaji saini tata wa mgodi wa Buzwagi miezi kadhaa iliyopita.
Ingawa bado haijathibitishwa kwa uhakika kabisa iwapo Karamagi alifanya kosa au la katika uamuzi huo, bado taswira yake kama waziri imekuwa na viulizo vingi, tangu suala hili lilipoibuka bungeni na baadaye kutumiwa na wapinzani kama turufu muhimu ya kujiimarisha.
Mbali ya hilo, kifo cha Mbatia aliyekuwa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na nafasi yake kuendelea kubakia wazi pasipo mtu mwingine kuteuliwa kuziba nafasi yake mapema, kunaongeza dalili za kuwapo kwa dhamira ya rais kufanya mabadiliko makubwa zaidi ya kuziba zaidi ya pengo hilo moja.
Historia ya utendaji wa Rais Kikwete tangu alipofariki aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge), Juma Akukweti, na baadaye kuondoka katika baraza kwa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dk. Asha - Rose Migiro, ni sehemu ya mambo yanayoonyesha kuwa hata safari hii anaweza kutumia kifo cha Mbatia kuwa sababu ya kulipangua na pengine kulibadili baraza lake la mawaziri.
Kama ilivyokuwa kwa kifo cha Akukweti na baadaye kuondoka kwa Migiro, Rais Kikwete alifanya mabadiliko madogo ya mawaziri kiasi cha kumfanya Bernard Membe, kwa mfano, kuguswa na matukio yote mawili, akihama kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani na kwenda Wizara ya Nishati na Madini, alikokuwa naibu waziri, kabla ya kuteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Wengine walioguswa na matukio hayo ni Emmanuel Nchimbi, Lawrence Masha, Batilda Burian, Karamagi, Daniel Nsanzugwanko, Dk. Ibrahim Msabaha, na David Mathayo ambao walihama kutoka wizara moja kwenda nyingine.
Aidha, katika matukio hayo mawili, wanasiasa, Gaudence Kayombo na William Ngeleja waliokuwa nje ya baraza waliweza kuingia wakiwa naibu mawaziri kuziba mapengo yaliyotokea.
Sura za wanasiasa zinazotarajiwa kuwemo katika baraza jipya ni pamoja na ile ya Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, ambaye kitaaluma ni mtaalamu wa sheria, au ile ya Mbunge wa Mbeya Vijijini, Richard Nyaulawa, mtaalamu wa uchumi.
Wanasiasa hawa wanapewa nafasi kubwa ya kuwamo katika baraza jipya kutokana na mwenendo wa mambo ulivyo katika serikali na joto la kisiasa nchini.
Hata hivyo iwapo Rais Kikwete atamchukua mmoja kati ya wanasiasa hawa katika baraza lake jipya, majaliwa ya kuendelea kubakia katika baraza hilo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Prof. Mark Mwandosya, na mwenzake, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Prof. David Mwakyusa, yanaweza kuwa shakani, kwa kuzingatia kuwa wanasiasa hao wanatoka katika mkoa na wilaya moja.
na Charles Mullinda
Tanzania Daima
KATIKA hali ambayo haikutarajiwa na wengi, Rais Jakaya Kikwete, ameamua kuwa msiri katika utendaji kazi wake.
Hali hiyo ilidhihirika Alhamisi wiki hii wakati alipokutana na kuzungumza na wahariri wa vyombo vya habari, Ikulu, Dar es Salaam kuhusu maadhimisho ya kutimiza kwake miaka miwili akiwa madarakani.
Katika mkutano wake huo na wahariri, Rais Kikwete alisema taarifa zinazoelezwa kuwa ana mpango wa kufanya mabadiliko katika baraza lake la mawaziri ni uvumi usio na ukweli wowote, lakini atakaa chini na kuangalia iwapo kutakuwa na haja ya kupunguza au kuliacha baraza hilo likiwa katika muundo wake wa sasa.
Kauli hii ya Rais Kikwete inapingana na uhalisia wa mambo unaoonyesha kwamba kwa hali yoyote, na kwa kuzingatia staili yake ya utendaji kazi ya kurejesha matumaini kwa wananchi kuhusu uongozi wake na serikali yake kwa ujumla, atalazimika kulivunja baraza lake la mawaziri wakati wowote kuanzia sasa.
Ukweli huu unathibitishwa na hatua kadhaa ambazo Rais Kikwete amekuwa akizichukua tangu aliposhika madaraka, miaka miwili iliyopita katika kuhakikisha kuwa serikali yake inabaki na mvuto kama iliokuwa nao wakati akiingia madarakani.
Baadhi ya hatua zilizochukuliwa na Rais Kikwete ili kulinda hadhi ya serikali yake ni pamoja na kuunda tume ya kuchunguza mauaji ya wafanyabiashara watatu wa madini, wenyeji wa Mahenge, waliodaiwa kuuawa na polisi.
Kikwete aliunda tume hiyo baada ya malalamiko ya wananchi kuhusu taarifa iliyotolewa na polisi kuwa waliouawa walikuwa majambazi na si wafanyabiashara, jambo lililopingwa na wananchi na kulitia doa Jeshi la Polisi.
Katika hatua nyingine, Rais Kikwete alilazimika kuunda kamati ya kupitia upya mikataba ya madini, akiwajumuisha pia wabunge kutoka kambi ya upinzani, baada ya kuwepo kwa kelele nyingi kutoka kwa kambi ya upinzani, wanaharakati na baadhi ya wananchi kuhusu usiri uliogubika mikataba hiyo inayodaiwa kulitia hasara taifa, huku ikiwanufaisha zaidi wawekezaji.
Mwenendo huo wa Rais Kikwete, unaonyesha kuwa kamwe hataifumbia macho ripoti ya Utafiti wa Mpango wa Elimu ya Demokrasia (REDET) inayoeleza kuporomoka kwa umaarufu wake binafsi pamoja na ule wa serikali yake.
Ripoti hiyo ambayo yeye mwenye na hata baadhi ya wasaidizi wake wa karibu wameikubali, akiwemo mshauri wake wa masuala ya siasa, Kingunge Ngombale-Mwiru, ni moja ya mambo yatakayomlazimisha Rais Kikwete kufanya mabadiliko ya haraka katika baraza lake la mawaziri ili kurejesha umaarufu wake na serikali yake ambao umeelezwa kuporomoka kwa kiwango kikubwa katika ripoti hiyo ya REDET.
Aidha, hatua ya Rais Kikwete kukubaliana na ripoti hiyo na kutamka kwake kuwa anaangalia uwezekano wa kulipunguza au kuliacha kama lilivyo baraza lake la mawaziri, ni dalili kuwa ana tafakari kwa kina kuhusu mabadiliko atakayoyafanya, jambo ambalo limechelewesha hata kuteuliwa kwa mrithi wa kiti cha marehemu Salome Mbatia, aliyekuwa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.
Rais Kikwete ambaye utawala wake unaelekea kutimiza nusu ya muhula wake atasukumwa pia na kauli za watu mashuhuri, kama Paul Rupia, aliyepata kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais kwa miaka mingi, aliyekaririwa na vyombo vya habari akizungumzia kuhusu haja ya rais kuchukua hatua hiyo.
Pamoja na wadadisi wengi wa mambo kuona haja ya lazima ya kufanyika kwa mabadiliko ya mawaziri sasa, matukio mengine kadhaa ya hivi karibuni, mbali na ripoti ya Redet, yanatoa mwelekeo huo huo wa mambo kubadilika.
Matokeo ya uchaguzi wa ndani katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) ulioshuhudia kuondoka madarakani kwa baadhi ya viongozi waandamizi katika sekretarieti ya chama hicho ni moja ya mambo yanayoonekana kuwa sehemu ya sababu zitakazomfanya Kikwete alazimike kuchukua hatua hiyo ya kubadili mawaziri.
Baadhi ya watu wanaotajwa kuwa wanaweza wakaingia katika baraza hilo jipya ni pamoja na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Jaka Mwambi na mwenzake aliyekuwa akishikilia wadhifa wa Katibu wa Uenezi na Itikadi, Aggrey Mwanri, ambao wote waliachwa katika sekretarieti mpya.
Wanasiasa hao wawili ambao kuachwa kwao katika uongozi wa kisiasa hauhusishwi na kushindwa kwao kazi, wanapewa nafasi kubwa kutokana na ukaribu wa kihistoria wa kikazi waliojijengea kwa Kikwete kwa miaka mingi.
Wakati Mwambi akitajwa kuwa komredi wa miaka mingi wa Kikwete tangu miaka ya 1970, Mwanri yeye anapewa nafasi kubwa kutokana na uwezo wake binafsi na eneo anakotokea wilayani Hai, ambako wapinzani na hususan Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kina nguvu kubwa.
Mbali ya tukio hilo, tuhuma na kasoro zilizopata kuzikumba baadhi ya wizara kama ile ya Nishati na Madini, Afya na Ustawi wa Jamii na Maliasili na Utalii ni jambo jingine linaloonekana kuwapo kwa uwezekano wa mabadiliko hayo kutokea.
Matukio ya namna hii kwa mfano, ndiyo ambayo kwa sababu za wazi yanamweka Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, kushikwa na kihoro cha kuweza kukumbwa na mabadiliko hayo, lengo likiwa ni kuondoa kiwingu alichojengwa tangu Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, alipomuunganisha na utiaji saini tata wa mgodi wa Buzwagi miezi kadhaa iliyopita.
Ingawa bado haijathibitishwa kwa uhakika kabisa iwapo Karamagi alifanya kosa au la katika uamuzi huo, bado taswira yake kama waziri imekuwa na viulizo vingi, tangu suala hili lilipoibuka bungeni na baadaye kutumiwa na wapinzani kama turufu muhimu ya kujiimarisha.
Mbali ya hilo, kifo cha Mbatia aliyekuwa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na nafasi yake kuendelea kubakia wazi pasipo mtu mwingine kuteuliwa kuziba nafasi yake mapema, kunaongeza dalili za kuwapo kwa dhamira ya rais kufanya mabadiliko makubwa zaidi ya kuziba zaidi ya pengo hilo moja.
Historia ya utendaji wa Rais Kikwete tangu alipofariki aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge), Juma Akukweti, na baadaye kuondoka katika baraza kwa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dk. Asha - Rose Migiro, ni sehemu ya mambo yanayoonyesha kuwa hata safari hii anaweza kutumia kifo cha Mbatia kuwa sababu ya kulipangua na pengine kulibadili baraza lake la mawaziri.
Kama ilivyokuwa kwa kifo cha Akukweti na baadaye kuondoka kwa Migiro, Rais Kikwete alifanya mabadiliko madogo ya mawaziri kiasi cha kumfanya Bernard Membe, kwa mfano, kuguswa na matukio yote mawili, akihama kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani na kwenda Wizara ya Nishati na Madini, alikokuwa naibu waziri, kabla ya kuteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Wengine walioguswa na matukio hayo ni Emmanuel Nchimbi, Lawrence Masha, Batilda Burian, Karamagi, Daniel Nsanzugwanko, Dk. Ibrahim Msabaha, na David Mathayo ambao walihama kutoka wizara moja kwenda nyingine.
Aidha, katika matukio hayo mawili, wanasiasa, Gaudence Kayombo na William Ngeleja waliokuwa nje ya baraza waliweza kuingia wakiwa naibu mawaziri kuziba mapengo yaliyotokea.
Sura za wanasiasa zinazotarajiwa kuwemo katika baraza jipya ni pamoja na ile ya Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, ambaye kitaaluma ni mtaalamu wa sheria, au ile ya Mbunge wa Mbeya Vijijini, Richard Nyaulawa, mtaalamu wa uchumi.
Wanasiasa hawa wanapewa nafasi kubwa ya kuwamo katika baraza jipya kutokana na mwenendo wa mambo ulivyo katika serikali na joto la kisiasa nchini.
Hata hivyo iwapo Rais Kikwete atamchukua mmoja kati ya wanasiasa hawa katika baraza lake jipya, majaliwa ya kuendelea kubakia katika baraza hilo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Prof. Mark Mwandosya, na mwenzake, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Prof. David Mwakyusa, yanaweza kuwa shakani, kwa kuzingatia kuwa wanasiasa hao wanatoka katika mkoa na wilaya moja.