haya yalisemwa hadi kwenye vyombo vya habari mkuu au hukusoma habari hiyo labda tuvilaumu vyombo vya habari vinavyoleta umbeya sio ss tunaoquote
pili kuna mtu jana ametupa dondoo za masharti ya wachina kujenga bandari ya bagamoyo, ulisoma au hukusoma, kama una hakika tupe mikataba hiyo tusome ss wenyewe tuone hayo masharti endapo jamaa aliyosema si ya kweli
tatu epuka matusi mm ni gt hata kama hutaki, ndiyo maana nimetumia neno tumesikia, pia serikali ilishindwa kutoa majibu muafaka kuhusu kashfa ya mtoto wa kigogo kukamatwa na madawa ya kulevya china na serikali kuweka commitment ili kunusuru maisha yake. ni wakati huo huo meli ya kinana iliyobeba meno ya tembo iliripotiwa kukamatwa china, kinana akakiri huoni hizi habari zina mtiririko unaoendana na ukweli kabisa?
nne je hukuona ile picha riz akiwa katikati ya rias wa china na mkewe badala ya wote, mtu wa kawaida unafikiri atatafsiri nn wakati alitajwa bayana kuwa yy ndiye aliyekamatwa na ili kumuokoa commitment zilifanyika kimaandishi
kama kila alilofanya riz/serikali lingewekwa hewan kwa vielelezo nchi ingepasuka vipande vipande hata unyasi huenda usingesalia
chunga comments zako kama ww ni gt toa habari mbadala zilizo sahihi kuhusu hoja iliyochangiwa na mdau kt jukwaa na sio kutumia lugha ya matusi na dharau bila kujibu hoja kwa ushahidi ulio wazi wa kumfanya kila mtu kujua ukweli juu ya jambo husika
msingi wa jukwaa hili ni kuelimishana na kusahihishana pale mtu anapokuwa na habari isiyokamilika