A
Anonymous
Guest
Ndugu zangu, hali ya upatikanaji wa maji katika Kijiji cha Mayonje, Kata ya Milepa katika Halmashauri ya Sumbawanga Vijijini, imekuwa ya kusikitisha sana, tangu mwezi wa 11, 2025 mwanzoni baada ya Uchaguzi Mkuu mpaka sasa, tumekuwa tukiishi bila huduma ya maji safi.
Chanzo cha tatizo ni bomba kubwa linalosambaza maji kijijini kwetu ambalo limepata hitilafu na kupasuka, lakini hadi leo halijatengenezwa.
Kibaya zaidi, kuna maneno yanayoenea kuwa tatizo hili linatokana na siasa za chuki; inasemekana baada ya diwani aliyepita kushindwa kwenye uchaguzi, ametuma vijana wake kukata bomba hilo kwasababu yeye ndio alisaidia bomba hilo kuunganishwa, akisema huyo diwani aliyeshinda (wa upinzani) ndio arejeshe huduma hiyo.
Hivi sasa, hali ni mbaya sana, tunaishi kwa kutegemea maji ya mvua, jambo ambalo sio sio sawa. Wakala wa Usambazaji Maji Vijijini (RUWASA) mje mtusaidie.
Mamlaka za chini zinasema zimefikisha suala hilo ngazi za juu, lakini kutokana na uhasama huo wa wakisiasa hata wao wanasema hakuna kingine wanachoweza kufanya zaidi ya kusubiri, na kila kitu ndio imeishia hapo, hakuna tena juhudi zinazofanyika kuhakikisha huduma hiyo inarejea.
Sisi Wananchi tulikuwa tayari hata kuchangia ili turejeshewe huduma hiyo lakini hatuoni juhudi zozote kutoka kwa viongozi wetu.
Tunaomba Serikali itusaidie, maji ni uhai na hatuwezi kuendelea hivi kwa sababu ya malumbano ya kisiasa.
Pia soma ~ Waziri Aweso atoa maelekezo mabomba ya Kijiji cha Mayonje - Sumbawanga yatangenezwe na huduma ya maji irejee
Kibaya zaidi, kuna maneno yanayoenea kuwa tatizo hili linatokana na siasa za chuki; inasemekana baada ya diwani aliyepita kushindwa kwenye uchaguzi, ametuma vijana wake kukata bomba hilo kwasababu yeye ndio alisaidia bomba hilo kuunganishwa, akisema huyo diwani aliyeshinda (wa upinzani) ndio arejeshe huduma hiyo.
Hivi sasa, hali ni mbaya sana, tunaishi kwa kutegemea maji ya mvua, jambo ambalo sio sio sawa. Wakala wa Usambazaji Maji Vijijini (RUWASA) mje mtusaidie.
Mamlaka za chini zinasema zimefikisha suala hilo ngazi za juu, lakini kutokana na uhasama huo wa wakisiasa hata wao wanasema hakuna kingine wanachoweza kufanya zaidi ya kusubiri, na kila kitu ndio imeishia hapo, hakuna tena juhudi zinazofanyika kuhakikisha huduma hiyo inarejea.
Sisi Wananchi tulikuwa tayari hata kuchangia ili turejeshewe huduma hiyo lakini hatuoni juhudi zozote kutoka kwa viongozi wetu.
Tunaomba Serikali itusaidie, maji ni uhai na hatuwezi kuendelea hivi kwa sababu ya malumbano ya kisiasa.
Pia soma ~ Waziri Aweso atoa maelekezo mabomba ya Kijiji cha Mayonje - Sumbawanga yatangenezwe na huduma ya maji irejee