Kiingereza cha Rais Samia

Kiingereza siyo lugha yetu ya kuzaliwa,kwa hiyo mtanzania akikosea kuongea hiyo lugha usimhukumi.
 
Hio fluent yao imesaidia nini kuiletea maendeleo tz!!?hivi waitaliano kama kina Anceloti wanaongeaje kiingereza umewahi kumsikia!!?ulisikia mzungu yeyote anamkosoa pale England!!?si walimwelewa na hakuna shida yeyote!!?kwanini mumkosoe mswahili anapooongea kiingereza kwa lafudhi ya kiswahili!!?kama sio ushamba ni nini!!!?NI UJINGA WETU TU KUDHANI KUONGEA KWA KUBANA PUA KAMA WAO NDIO MAENDELEO NA PERFOMANCE YA KUKUZA MAENDELEO KUMBE USHAMBA NA U DUNI WA KUFIKIRI!!!HATA NYERERE HAKUONGEA KWA LAFUDHI YA WAZUNGU BALINLAFUDHI YA KISWAHILI KAMA WENGINE TU!!!
Wapo vijana wamesoma nje ya Nchi na ndani kwenye shule za michepua ya English wako very fluent
 
So what?
Acheni fyoko fyoko.

Samia mbele kwa mbele
 
Kinachokusumbua ni chuki kwa kua wewe ni sukuma gang.....kubali na ukatae wewe na push gang wenzio ndo jamii primitive kuwahi kutokea duniani
 
KKw
Mama yupo vizuri sana na nikajua labda hajaeleweka kwenye pronouncing na grammar kumbe hapo hapo kwenye last 60 years umepaona ww. Madam Vice president mwenyewe ameelewa na kaeleweshwa hadi kaelewa na hajawahi kucheka akiwa na marais wengine wapuuzi wapuuzi kwakuwa anapata shida sana kuelewa matamshi yao.
Ila raia wangu alikuwa very loud and clear nna tone pia kuna mda nikahisi namsikiliza Michelle Obama au Hillary Clinton kumbe Mh Samia.
 
Sa itakuaje
 
Huyu alizaliwa na kukulia Butiama huko.

Hebu mcheki hapo. Super impressive.

Hasomi popote.

Ni sawa Nyerere alikuwa yuko vizuri kwa Kiingereza ila aliharibu hadi leo wachache wanaweza kuwa fluent kwenye hiyo lugha,ni hao hao awamu ya kwanza kwa ubinafsi wao wakapindua mitaala ya elimu mara elimu ya UPE,mara masomo yote kwa kiswahili utadhani ndio kilikuja na hayo masomo nchi tunazopakana nazo ambazo nazo zilitawaliwa na Mwingereza zikayahifadhi masomo hayo kwa lugha ile ile,iliyokuja na hayo masomo,Athari za kubadilisha lugha kwenye mitaala ni kufeli kwa wanafunzi wengi wa sekondari kwani lugha ya mawasiliano hawaijui.
 
Amenyosha nyosha ila hajaongea kama rais na hata utokaji aliotoka nao hapo utadhani form one kwenye morning speech na point zake 5 za laboratory rules.
Samia amekuwa very composed and confident when talking or giving speech ni mtu wa kuigwa huyu hado wadhungu wa ulaya wanamwita soft magician and locomotive speaker
 
Nilimsikia Zelensky akiongea kiingereza. Kinampa shida sana. Huwezi kuwa fluent wa lugha ambayo hutumii kila siku. Inasikitisha kuwa watz bado wanaamini anayejua kiingereza ndiye ana akili.
 
Ndugu "ujui"
Kwa hivyo mzizi wa neno ni ‘’ujui’’ !? Na mnyumbuliko wake Ndio ‘haujui’ 🤣
Mkuu bora ungekausha tu kuliko kuanza kukosoa watu na kujifanya mwalimu wa Kiswahili!
Tuchangie Mada tu muhimu content imeeleweka !
 
Tahila wewe, kwahiyo dunia nzima kila mtu anaijua lugha ya Taifa lingine kwa ufasaha, sukuma gang mmevurugwa wapuuzi nyie
Tz bila kienglish unaonekana wewe ni mtu wa ajabu sana lakin ulimwengu mzima hawatumii hii lugha lakin maisha yanaenda
 
Kwa hivyo mzizi wa neno ni ‘’ujui’’ !? Na mnyumbuliko wake Ndio ‘haujui’

Mkuu bora ungekausha tu kuliko kuanza kukosoa watu na kujifanya mwalimu wa Kiswahili!
Tuchangie Mada tu muhimu content imeeleweka !
Hayo umesema wewe! Wewe ndiye unadhani hivyo. Hata neno ulilotumia mwanzo umeondoa "H". Ndiyo sababu nimeweka unavyotumia wewe "ujui" "apana" "ongela"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…